TANZIA Dkt. Peter Mamiro afariki dunia zikiwa zimepita siku mbili tokea mkewe(Prof. Delphina Mamiro) afariki dunia

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,075
4,111
Habari mbaya ya kusikitisha ni kuwa Dkt. Peter Mamiro amefariki dunia usiku wa kuamkia leo mkoani Morogoro ikiwa zimepita siku mbili tokea mkewe, Profesa Delphina Mamiro afariki dunia. Dkt. Peter Mamiro na Profesa Delphina Mamiro walikuwa wanafundisha Chuo cha Kilimo Sokoine - SUA.

Habari za kuaminika kutoka kwa ndugu wa karibu zinasema kwamba siku chache zilizopita, Dkt. Peter na Profesa Delphina walitoka Kilimanjaro kuwazika wazazi wawili (Mchungaji Kessy na mkewe) wa Profesa Delphina ambao nao vifo vyao vilifuatana.

Inadaiwa baada ya kurudi Morogoro hali ikuwa mbaya mpaka umauti unawakuta.

Mwenyezi Mungu aipe nguvu na faraja familia hii inayopitia majaribu haya yote.

Pia soma: TANZIA - Profesa Delphina Mamiro wa Chuo Kikuu cha Kilimo(SUA) afariki dunia

Mamiro.JPG
 
Whichever we wanna call whatever is happening. Taasisi husika inabidi ziangalie kwanini vifo vimeongezeka?

Kwa opinion yangu nadhani ni bora kama wangesema wanajua kinachotokea (COVID au lolote lile) kuliko wanajua sio COVID, sasa ni nini? Yaani ni bora kujua kinachotokea kuliko kutokujua, hence hata kukiepuka hauwezi.

The only good thing ni kwamba (Kama ni COVID) itafikia peak alafu itashuka / pungua na kuacha ila issue ni kwamba peak imefika, imeshafika au haijafika (hopefully imeshafika na kupita)
 
Aiseee. Mungu atulinde jamani. Hali imekuwa tete sana jamani. Bila shaka yule saizi yupo happy anashushia na kapepsi barid akiona wananchi wake tunateseka
 
Back
Top Bottom