Dkt. Ndungulile, hutaki kujiuzulu au unasubiri usaidiwe kazi?

Prof Koboko

JF-Expert Member
Aug 15, 2020
350
2,549
Haiwezekani waziri unakaa na wamiliki wa mitandao ya simu mnakubaliana kitu ambacho unajua kabisa kitaiumiza jamii hasa wananchi wa hali ya chini tena zaidi wewe kama kiongozi unapigilia msumari.

Kwanza umeudanganya umma kwamba mapendekezo yenu yalikuwa ña unafuu kuliko ilivyokua zamani hali ambayo ndani ya siku hizi mbili imeonekana tofauti kabisa.

Waziri unataka kuwa chanzo cha serikali kukosa mapato kwa sababu wananchi kukata tamaa na matumizi ya vifurushi pamoja na kushindwa kufanya biashara hasa za mitandaoni.

Waziri ubunifu mzuri wa kuwasaidia wananchi imekosekanana kabisa ukiona hii hali ya unyonyaji ni sawa?
Kiongozi unajua wewe unawekewa vocha kila siku na serikali ikiwa ni pamoja vifurushi vya kutosha lakini hawa wa hali ya chini hujui ilivyo shida kuipata.

Kilio kikubwa cha awali kwa wananchi ilikua ni matumizi ya vifurushi kutokua na mipaka ya muda inayoeleweka au kusemana uwiano sawa wa muda pamoja na na na kiwango cha pesa kilichotumika kujiunga. Badala ya kuja na suluhisho hili matokeo yake mmekuja na maumivu zaidi.

Tunaishukuru serikali chini yaRais Mama yetu mpendwa sana Mhe Samia Suluhu Hassan wameliona hili na kuelekezwa mpango huo usitishwe. Hapa ndi dalili za kwamba unatakiwa kusaidiwa kazi, kabla ya kusaidiwa ingeanza kuikabidhi ofisi mapema kujiuzulu.
 
Huyu angerudishwa kule kwenye Naibu Waziri wa Afya. Hana msaada kwa hili, yupo yupo tu yaani.

Ametochosha mno!
 
Tatizo ni Katiba mbovu. Ilifaa wananchi wa Kigamboni wapige chini huyu mtu fasta.

Afadhali kukosa mbunge kuliko kuwakilishwa na huyo ndugu-lile
 
Mama yetu aifute tu hii wizara,hizo kazi zifanywe na TCRA manake toka imeanzishwa ndo tunaletewa mara bei hatari za vifurushi mara aseme anazuia whatsapp call sijui serikali inapoteza mapato!we ulisikia wapi?

Ivunjwe hiyo huyo waziri arudi afya afterall ndo taaluma yake ilipo!
 
Kwani huyu waziri Dr anaelimu gani? Unaweza kuta anaelimu ya kutibu binadamu hafu anaenda kuwa waziri wa ICT.

Hata ukimuuliza 1MB Ni sawa na kilobite ngapi hajui , hata ukimuuliza one 1GB ni Mb ngapi hajui, unaweza kutwa kadanganywa akijua bei inashuka kumbe inapanda. Na hii bei imepanda tofauti na 2017 kurudi nyuma, imepanda Mara mbili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hadi sasa sielewi

Anayepanga bei za vifurushi ni waziri?
Kampuni za simu zinakuwa regulated na TCRA! TCRA ipo chini ya Wizara ya Mawasiliano na...." Wizara ya Mawasiliano inaongozwa na Ndungulile. Kutokana na mlolongo huo, kampuni za simu haziwezi kupandisha gharama za vifurushi pasipo na baraka ya TCRA! Na TCRA haiwezi kutoa baraka kwa kampuni za simu pasipo na baraka za waziri husika!
 
Huyu angerudishwa kule kwenye Naibu Waziri wa Afya. Hana msaada kwa hili, yupo yupo tu yaani

Ametochosha mno..!
Kwani ni lazima awe Waziri? Wizara itakayowaumiza wananchi, Watendaji wake wakionekana Mitaani wazomewe.
 
Itakuwa anasubiri Kwanza Kampuni zote za Simu zimalize Kurejesha Vifurushi vile nafuu vya Awali ( kama ilivypamriwa Jana jioni na TCRA ) ndipo nae afungashe Virago vyake.
 
Wizara hii ni ya kumdhibiti Kigogo na moja ya njia zake ni kuwafanya watu wasipate mtandao kwa kuifanya kuwa ya gharama kubwa maana kuzuia kumeshindikana baada ya kigogo kutoa VPN.
 
Back
Top Bottom