Dkt. Ndumbaro sababu hizi hazitoshi kuhamisha FITI-Moshi

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
13,991
20,282
Dkt. Ndumbaro sababu hizi hazitoshi kuhamisha FITI-Moshi

Mnamo Julai 05, 2021 waziri wa Utalii na maliasili Mhe. Dkt. Ndumbaro [Wakili na mmiliki/Partner wa Meleta and Ndumbaro Advocates iliyopo Dar es salaam ] alipotembelea Taasisi ya Mafunzo ya Viwanda vya Misitu (Forest Industries Training Institute FITI) iliyoko katika manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro aliitaka iwe tayari kuhamia Iringa. Uhamisho huo ndiyo mjadala wa makala hii.

FITI-Moshi
, ni taasisi ya mafunzo iliyoanzishwa mwaka 1975 kwa msaada wa Shirika la Maendeleo la Sweden SIDA kwa malengo ya kuandaa nguvukazi yenye ujuzi kwa ajili ya viwanda vya mazao ya misitu.
FITI-Moshi inaongozwa na Dkt. Joseph Makero na Bodi yake ya ushuri iko chini ya Prof. Reuben Mwamakimbula.
Chuo hiki kiliweza kudahili wanafunzi 250 (2019-2020) kwa mujibu wa hotuba ya Waziri mwenye dhamana bungeni (Aprili 2021). Mafunzo katika chuo hiki ni ngazi ya Stashahada, Cheti na ya Muda mfupi.

Uamuzi wa kuihamisha FITI-Moshi kwa maelezo ya Mheshimiwa waziri yanaibua maswali mengi kuliko majibu. Kwa nini Taasisi hiyo ihamishwe?

Hoja ya ukaribu na viwanda vingi vya misitu ni hoja dhaifu sana. Mheshimiwa waziri Dkt. Ndumbaro unajua fika nguvukazi inatembea. Kote duniani watu wenye ujuzi wanahama maeneo na vituo vya kazi kila uchao. Hata hivyo hakuna uwezekano kuwa viwanda vya misitu vilivyopo Mafinga kuajiri wahitimu wote wa Taasisi hii. FITI-Moshi ikiwa taasisi ya mafunzo inawajibika kuandaa wahitimu wake kufanya kazi popote ndani na nje ya Tanzania. Mkoani Kilimanjaro kuna misitu ya West Kilimanjaro na Rongai ambamo kuna shughuli nyingi za kiuchumi za viwanda vya misitu.

Hoja ya vifaa vya mafunzo kuwa vya zamani: uhamisho wa taasisi kutoka Moshi kwenda Mafinga hautengenezi vifaa vya kisasa. Vifaa vinanunuliwa na kufungwa. FITI-Moshi wanazo tayari karakana za kufunga vifaa vya kisasa kwa kuondoa vya kizamani. Serikali imekarabati shule kongwe nchi nzima na kuzipa vifaa vya kisasa, haikuzihamisha. Kwa nini FITI-Moshi iwe tofauti?
Hoja ya Wanafunzi kupata sehemu za mafunzo kwa vitendo: hii inaleta utata zaidi. Muda wa mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi huwa kwa mujibu wa mtaala wao na hutengewa kipindi maalum katika mwaka wa masomo, ambapo wanafunzi hupata uzoefu halisi wa mahala pa kazi. Hili hufanyika kwa wanafunzi wa vyuo na vyuo vikuu vyote nchini. Wanafunzi wananyimwa au kushindwa kwenda Mafinga kuhudhuria mafunzo kwa vitendo? Kama wanashindwa sababu ni nini? Kuhamisha Taasisi ndiyo suluhu? Hilo tawi litakalobaki Moshi wanafunzi hawatakwenda mafunzo kwa vitendo? Ikumbukwe mafunzo haya ni ya mara moja tu kwa mwaka wa masomo.​


Hoja hii inataka kutuaminisha mafunzo kwa vitendo hayawezekani hadi chuo kihamie Mafinga. Je, vyuo vya madini viko migodini? (mfano Cho cha Madini Dodoma). Taaluma ya mafuta na gesi, vyuo viko bahari kuu? Taasisi ya Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP- Dodoma) iko Vijijini? Vyuo vya Mafunzo ya Fedha vingapi viko benki? Taasisi ya FITI kuwa Moshi tatizo nini hadi ihamishwe?

Kama Hoja ni eneo finyu kwa upanuzi wa chuo, waziri hakusema ila FITI-Moshi haizuiliwi kuanzisha kampasi za mafunzo mahali pengine. Taasisi ya Teknolojia Dar Es Salaam (DIT) imeanzisha kampasi Mwanza, Taasisi ya Usimamizi wa Fedha (IFM) imeanzisha kampasi Simiyu, Dodoma na Mwanza, Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) kimeanzisha kampasi Katavi, Chuo Kikuu Mzumbe kina kampasi Dar Es Salaam na Mbeya. Vyuo vyote hivyo havikuhamisha makao makuu yake bali vilianzisha matawi na vyote ni vya serikali. Kwa nini FITI Moshi iwe tofauti?

Mhe. Dkt. Ndumbaro, kuongeza taasisi ya Mafunzo ya Viwanda vya Misitu Mafinga ni jambo jema, ila kuhamisha Taasisi iliyopo mahali pengine unaturudisha kwenye Operesheni Vijiji. Anzisha taasisi ya Mafunzo pale Mafinga na yaweza kabisa kuwa tawi la Chuo Kikuu chochote sii lazima hata kuwa tawi la FITI-Moshi. Kama kuna sababu nyingine tushirikishe wananchi tutafakari pamoja.​

ANGALIZO RAIS SULUHU:
Ndumbaro ni zao la Mwendazake, ana mengi kinyume na spirit yako ya kujenga nchi kwa pamoja na upendo.
https://twitter.com/SuluhuSamia:-
 
Mhe. Dkt. Ndumbaro, kuongeza taasisi ya Mafunzo ya Viwanda vya Misitu Mafinga ni jambo jema, ila kuhamisha Taasisi iliyopo mahali pengine unaturudisha kwenye Operesheni Vijiji. Anzisha taasisi ya Mafunzo pale Mafinga na yaweza kabisa kuwa tawi la Chuo Kikuu chochote sii lazima hata kuwa tawi la FITI-Moshi. Kama kuna sababu nyingine tushirikishe wananchi tutafakari pamoja 👍 👍 👍
 
Hizi ndizo hoja za kuendeleza nchi. Tunarudi kule kule. Viongozi wetu wanalala kwa vimada wanapewa ushauri asubuhi wanakwenda kutoa tamko. Hii gharama yote ya kuhamisha chuo kwa sababu za kijinga namna hii imetolewa na waziri?

Fedha zenyewe hatuna na tunaishi kwa kuomba omba halafu mtu anakwenda kuongezea gharama kwa maamuzi mabovu kabisa. Huku ni kutumia madaraka vibaya.

Wahusika wakatae huu ujinga. Wengi wanasema ufukara nchini mwetu unaletwa na mipangilio na maamuzi mabovu huu ni ushahidi mwingine.
 
Hizi ndizo hoja za kuendeleza nchi. Tunarudi kule kule. Viongozi wetu wanalala kwa vimada wanapewa ushauri asubuhi wanakwenda kutoa tamko. Hii gharama yote ya kuhamisha chuo kwa sababu za kijinga namna hii imetolewa na waziri? Fedha zenyewe hatuna na tunaishi kwa kuomba omba halafu mtu anakwenda kuongezea gharama kwa maamuzi mabovu kabisa. Huku ni kutumia madaraka vibaya. Wahusika wakatae huu ujinga. Wengi wanasema ufukara nchini mwetu unaletwa na mipangilio na maamuzi mabovu huu ni ushahidi mwingine.
ndio wale wale walifuta michezo shuleni alafu baadae wakaja kuirudisha UMISSETA , walifuta kwa kisingizio inashusha kiwango cha elimu. Maprofesa hao.
 
Kuna wakati huwa nawaelewa Sana msukuma na kibajaji wanapowaamba ukweli hawa professors and PhD holders sijui wanatumia nn kufikiri

Wakat dunia inaenda kasi katika elimu wao wanairudisha dunia kuwa kuwa ya mwaka 1990

Kifupi hakuna haja ya kuhamisha chuo badala yake waongeze fursa ya elimu ya misitu maeneo mengine Zaid ili tuwe na vyuo vingi

Kama hali n hyo bas hata chuo cha OLMOTONYI ARUSHA hakitakiwi kuwa pale kiende iringa maana misitu s ndio ipo huko

Kozi ya mifugo haikutakiwa kuwa CHUO CHA MIFUGO TEMEKE ..LITA.sababu wafugaji wakubwa hawapo huko TEMEKE

Hizi PhD jaman tuwe nazo makini Sana Kuna siku watafanya Jambo la kushangaza tutakuwa tumechelewa kubaini
 
Kuna wakati huwa nawaelewa Sana msukuma na kibajaji wanapowaamba ukweli hawa professors and PhD holders sijui wanatumia nn kufikiri

Wakat dunia inaenda kasi katika elimu wao wanairudisha dunia kuwa kuwa ya mwaka 1990

Kifupi hakuna haja ya kuhamisha chuo badala yake waongeze fursa ya elimu ya misitu maeneo mengine Zaid ili tuwe na vyuo vingi

Kama hali n hyo bas hata chuo cha OLMOTONYI ARUSHA hakitakiwi kuwa pale kiende iringa maana misitu s ndio ipo huko

Kozi ya mifugo haikutakiwa kuwa CHUO CHA MIFUGO TEMEKE ..LITA.sababu wafugaji wakubwa hawapo huko TEMEKE

Hizi PhD jaman tuwe nazo makini Sana Kuna siku watafanya Jambo la kushangaza tutakuwa tumechelewa kubaini
Ndiyo maana tulisema MLIMA KILIMANJARO UNGEFAA kuhamishwa KIGWA angesha-uhamishia CHATO , maana alihamisha Simba wa Serengeti, kila kitu, TRA, Makao Makuu ya WANYAMAPORI , etc.
 
Kuna wakati huwa nawaelewa Sana msukuma na kibajaji wanapowaamba ukweli hawa professors and PhD holders sijui wanatumia nn kufikiri

Wakat dunia inaenda kasi katika elimu wao wanairudisha dunia kuwa kuwa ya mwaka 1990

Kifupi hakuna haja ya kuhamisha chuo badala yake waongeze fursa ya elimu ya misitu maeneo mengine Zaid ili tuwe na vyuo vingi

Kama hali n hyo bas hata chuo cha OLMOTONYI ARUSHA hakitakiwi kuwa pale kiende iringa maana misitu s ndio ipo huko

Kozi ya mifugo haikutakiwa kuwa CHUO CHA MIFUGO TEMEKE ..LITA.sababu wafugaji wakubwa hawapo huko TEMEKE

Hizi PhD jaman tuwe nazo makini Sana Kuna siku watafanya Jambo la kushangaza tutakuwa tumechelewa kubaini
Wafanye jambo la kushangaza mara ngapi ?
1. Wewe hujashangaa professor mwenye GPA ya 4.8 kuita chuo kikuu jalala ?

2. Wewe hukushangaa Dk wa sheria kutaka mtu asifunge ndoa bila cheti cha kuzaliwa.

3. Wewe hushangai Dk wa Sayansi ya siasa kusema atatumia dola kubaki madarakani na kusababisha maafa na vilema kwa watu wengi tu.

4. Wewe hushangai Dk wa uchumi kupandisha kodi ya mafuta halafu akashusha kodi kwenye bia kisa anataka kuboresha barabara za vijijini ?

5. Wewe hukushangaa Dk Kigwangalla a professional MD kuwa na msimamo A dhidi ya corona juu ya utawala wa jiwe na kuwa na msimamo B kwenye utawala wa sasa ?

6. Wewe hukushangaa Muhimbili kujenga banda la kujifukiza chini ya utawala uliopita baada ya hapo waliokwenda kujifukiza hapo wakiwemo wataalamu wa Afya kutaka livunjwe tupate chanjo ??


Kuna mengi ya kushangaza ila huwa hatutaki kushangaa tu yawezekana tumeshachoka kushangaa.
 
Siku zote mwanamk hata akiwa malaya vipi hawezi kuwa na ujasiri wa kumtongoza mwanaum bila kupitia rafiki yake na huyo mwanaume, afu baadae ndo vitimbwi vya kuvaa vimini na kujipitisha mbele ya yule mwanaume huanza ili kumteka . Hapa namaanisha mleta mada umeona hauwezi kuandika unachoandika kikasapotiwa bila kumuhusisha hayati Magufuli au Mataga. Lkn sikulaumu ww kwa sababu ikiwa mwenyekiti wako aliishia form 4, nina imani basi ww msukule wake hauna elimu hata ya darasa la saba. Kazana dada yang huenda mwenyekiti atakugeuza nyumba ndogo yake ya kupumulia.
 
Kuhamishwa Kwa chuo cha FITI kilichopo huko Moshi Kilimanjaro,Litakuwa ni pigo la kwanza la kumuondoa ubunge mbunge mwaka 2025 aliyeko madarakani bila kupepesa macho. Mbunge huyo alihaidi miradi kibao ikiwepo hospital ya wilaya,mikopo Kwa Boda Boda, mafunzo Kwa wapangazi wa mlima Kilimanjaro, ujenzi wa ofisi za chama wilaya, mikopo Kwa vikundi , kugufua viwanda karibua 20 vilivyo kufa, Ila hadi Leo hajafanya Chocho te amekuwa msindikizaji huko bungeni Sasa anasimamia chuo kinahamishiwa iringa.
 
Kuhamishwa Kwa chuo cha FITI kilichopo huko Moshi Kilimanjaro,Lita ni pigo la kwanza la kumuondoa ubunge mbunge mwaka 2025 aliyeko madarakani bila kupepesa macho. Mbunge huyo alihaidi miradi kibao ikiwepo hospital ya wilaya,mikopo Kwa Boda Boda, mafunzo Kwa wapangazi wa mlima Kilimanjaro, ujenzi wa ofisi za chama wilaya, mikopo Kwa vikundi , kugufua viwanda karibua 20 vilivyo kufa, Ila hadi Leo hajafanya Chocho te amekuwa msindikizaji huko bungeni Sasa anasimamia chuo kinahamishiwa iringa
 
Wafanye jambo la kushangaza mara ngapi ?
1. Wewe hujashangaa professor mwenye GPA ya 4.8 kuita chuo kikuu jalala ?

2. Wewe hukushangaa Dk wa sheria kutaka mtu asifunge ndoa bila cheti cha kuzaliwa.

3. Wewe hushangai Dk wa Sayansi ya siasa kusema atatumia dola kubaki madarakani na kusababisha maafa na vilema kwa watu wengi tu.

4. Wewe hushangai Dk wa uchumi kupandisha kodi ya mafuta halafu akashusha kodi kwenye bia kisa anataka kuboresha barabara za vijijini ?

5. Wewe hukushangaa Dk Kigwangalla a professional MD kuwa na msimamo A dhidi ya corona juu ya utawala wa jiwe na kuwa na msimamo B kwenye utawala wa sasa ?

6. Wewe hukushangaa Muhimbili kujenga banda la kujifukiza chini ya utawala uliopita baada ya hapo waliokwenda kujifukiza hapo wakiwemo wataalamu wa Afya kutaka livunjwe tupate chanjo ??


Kuna mengi ya kushangaza ila huwa hatutaki kushangaa tu yawezekana tumeshachoka kushangaa.
Mkuu umeua

Hofu yangu mmoja wao anaweza akawa prezidaa Kama Dr stone halafu akauza nchi kabisa

Hivi yule wazir wa elimu wa Tanzania lakn n mkenya kiasili ambaye alifuta michezo mashuleni na kuunganisha masomo hivyohovyo alikuwa anaitwa Nani vile?

Nchi hii hata waziri anaweza akashauri tule mavi na mamlaka zikaafki tu
 
Mleta mada kiukweli bado ile hangover ya wasukuma bado inaitesa hii serikali tulivu na isiyo na mambo ya hovyo kama mtangulizi wake.
lazima ieleweke kuwa FITI imekuwa pale kwa miaka mingi na ina manufaa mengi hata kwa ustawi wa Mt Kilimanjaro.
Haya maamuzi ya kipuuzi ya viongozi wetu ni ya ajabu na ya kupigwa vita, sidhani kama mama Samia atakubali huu upuiuzi.
Huenda Ngumbaro anataka kuisogeza karibu na kwao au hajui mchezo ulio nyuma yake.
 
Mkuu umeua

Hofu yangu mmoja wao anaweza akawa prezidaa Kama Dr stone halafu akauza nchi kabisa

Hivi yule wazir wa elimu wa Tanzania lakn n mkenya kiasili ambaye alifuta michezo mashuleni na kuunganisha masomo hivyohovyo alikuwa anaitwa Nani vile?

Nchi hii hata waziri anaweza akashauri tule mavi na mamlaka zikaafki tu
Nchi iuzwe mara ngapi mkuu,

Walishauza Madini yote.

Wameuza gesi yote.

Wakajiuzia makaa ya mawe yote.


Wamebaki kutuuza na sisi wenyewe japo nina mashaka kama bado hatujauzwa pia.
 
Mkuu umeua

Hofu yangu mmoja wao anaweza akawa prezidaa Kama Dr stone halafu akauza nchi kabisa

Hivi yule wazir wa elimu wa Tanzania lakn n mkenya kiasili ambaye alifuta michezo mashuleni na kuunganisha masomo hivyohovyo alikuwa anaitwa Nani vile?

Nchi hii hata waziri anaweza akashauri tule mavi na mamlaka zikaafki tu
Mungai
 
Nchi iuzwe mara ngapi mkuu,

Walishauza Madini yote.

Wameuza gesi yote.

Wakajiuzia makaa ya mawe yote.


Wamebaki kutuuza na sisi wenyewe japo nina mashaka kama bado hatujauzwa pia.
Dah so sad ndumbaro n mbunge wangu huko nyumbani songea town
 
Back
Top Bottom