Dkt. Ndumbaro: Raia alietendewa vibaya na askari wa hifadhi wakaripoti ili hatua zichukuliwe

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,005
9,872
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro amesema hadi sasa kuna askari 61 wamefukuzwa kazi baada ya kuthibitika kuwa wamekuwa wakiwatendea vibaya wananchi wanaoingia hifadhini

Amewataka watu wengine wenye ushahidi wa wananchi kutendewa vibaya na askari wa hifadhi wapeleke ushahidi ili askari husika wachukuliwe hatua

Kutokana na changamoto ya wananchi kupeleka mifugo yao hifadhini na kusababisha mapambano kati ya wananchi na polisi. Waziri amewataka viongozi kuwaelimisha wananchi ili waache tabia ya kupeleka mifugo hifadhini
 
Ivi ng'ombe wakiingia hifadhini,wanaharibu nini zaid ya kula tu majani
 
Siyo kwenye Mali asili tu tunataka kila sehemu kuwepo na usawa hawa polisi wanatumia madaraka yao vibaya sana, tunamtaka IGP aje mpaka vilaya ya tarime hapa nyamongo aone jinsi polisi wake wanavyofanya matukio na kuwanyanyasa raia wanaozunguka mgodi kisa tu madili ya mawe ya dhahabu
 
Back
Top Bottom