Deogratias Mutungi
Senior Member
- Oct 1, 2019
- 137
- 179
Nawasalimu wana JF,
Nimekuwa mfatiliaji wa karibu sana wa siasa za upande wa Tanzania Visiwani kwa maana ya Zanzibar, nimegundua falsafa na maono makubwa ya Dkt. Hussein Mwinyi juu ya mipango yake ya uendeshaji wa serikali ya SMZ katika nadharia ya "Uchumi wa watu na vitu" Nimegundua Dkt. Mwinyi anatambua kuwa maendeleo ni watu kulingana na mifumo ya vitu vilivyopo katika uzalishaji, Ukimsikiliza vyema Dkt. Mwinyi unagundua mawazo yake katika falsafa ya uchumi wa watu ni sawa na yale mawazo na fikra alizokuwa nazo Mwl. Nyerere "Mjamaa" Kwa mantiki hiyo unaweza kusema wote wawili mawazo yao yanashahabiana pale inapokuja hoja ya uchumi wa watu na vitu, Kwenye dhana hii sioni tofauti ya Dkt. Hussein Mwinyi na Mwl. Nyerere.
Dkt. Mwinyi anaamini kukuza kipato cha Wazanzibar kupitia maliasili na mapato mengine yatokanayo na vitu vilivyo chini ya serikali ya SMZ, Kwa lugha ya kimaendeleo Mwinyi anaguswa sana na kuendeleza uchumi wa watu ambao ndio waajiri wake na watakao mtuma kwenda ikulu kuwatumikia, mawazo ya Dkt. Mwinyi ni mapana na yenye maslahi na yakiungwana kwa Wazanzibar, Kwa mantiki hiyo Dkt. Mwinyi ni mzalendo na kiongozi anayetanguliza utu kwanza katika utumishi wa watu.
Ni Rai ya andiko hili fupi kwa Wazanzibar kumpa kura za ndio kwa wingi Dkt. Hussein Mwinyi ili aweze kuwatumikia Wazanzibar na kuwaletea neema za maendeleo, aidha Dkt. Mwinyi anayabeba maono ya Mwl. Nyerere juu ya dhana ya maendeleo ya watu dhidi ya uchumi wa vitu, tumtume na kumpa ridhaa ya kuonyesha hiki anachokiamini kwa vitendo, Wazanzibar msikosee hata kidogo tumpe kura za ndio kwa wingi hapo tarehe 28/10/2020 ili atuonyeshe radha ya maendeleo tunayohiitaji sisi kama wananchi.
Nimekuwa mfatiliaji wa karibu sana wa siasa za upande wa Tanzania Visiwani kwa maana ya Zanzibar, nimegundua falsafa na maono makubwa ya Dkt. Hussein Mwinyi juu ya mipango yake ya uendeshaji wa serikali ya SMZ katika nadharia ya "Uchumi wa watu na vitu" Nimegundua Dkt. Mwinyi anatambua kuwa maendeleo ni watu kulingana na mifumo ya vitu vilivyopo katika uzalishaji, Ukimsikiliza vyema Dkt. Mwinyi unagundua mawazo yake katika falsafa ya uchumi wa watu ni sawa na yale mawazo na fikra alizokuwa nazo Mwl. Nyerere "Mjamaa" Kwa mantiki hiyo unaweza kusema wote wawili mawazo yao yanashahabiana pale inapokuja hoja ya uchumi wa watu na vitu, Kwenye dhana hii sioni tofauti ya Dkt. Hussein Mwinyi na Mwl. Nyerere.
Dkt. Mwinyi anaamini kukuza kipato cha Wazanzibar kupitia maliasili na mapato mengine yatokanayo na vitu vilivyo chini ya serikali ya SMZ, Kwa lugha ya kimaendeleo Mwinyi anaguswa sana na kuendeleza uchumi wa watu ambao ndio waajiri wake na watakao mtuma kwenda ikulu kuwatumikia, mawazo ya Dkt. Mwinyi ni mapana na yenye maslahi na yakiungwana kwa Wazanzibar, Kwa mantiki hiyo Dkt. Mwinyi ni mzalendo na kiongozi anayetanguliza utu kwanza katika utumishi wa watu.
Ni Rai ya andiko hili fupi kwa Wazanzibar kumpa kura za ndio kwa wingi Dkt. Hussein Mwinyi ili aweze kuwatumikia Wazanzibar na kuwaletea neema za maendeleo, aidha Dkt. Mwinyi anayabeba maono ya Mwl. Nyerere juu ya dhana ya maendeleo ya watu dhidi ya uchumi wa vitu, tumtume na kumpa ridhaa ya kuonyesha hiki anachokiamini kwa vitendo, Wazanzibar msikosee hata kidogo tumpe kura za ndio kwa wingi hapo tarehe 28/10/2020 ili atuonyeshe radha ya maendeleo tunayohiitaji sisi kama wananchi.