Dkt. Mwele Malecela awataka wataalam kufanya kazi bila woga

Acha kudanganya jamii kwani hakuna Mwaipopos anayeweza kuwa na hata robo ya Mweles IQ na kama kuna hata mmmoja unayemjua tuambie tukusaidie kuchambua

Sizungumzii any other Mwaipopo nazungumzia IQ ya Ezelina Mwaipopo; Former Senior State Attorney, mama yake Mwele!!! Umeelewa? Hao wengine unawajua wewe!!
 
Mabeberu wanataka kumtumia waje kuotesha ugonjwa mwingine tena kama walivyotaka kuleta zika na ebola...wakadunda kwa jemedari.
 
Hayati alianza na mke halafu akaenda kwa binti na cha kushangaza akawa anamsifia wazi kabisa mzee mwenyewe bila kujali akiwa na hao watu wake wawili wanakuwa wanamzungumzia vipi.
 
Yule Dr. Aliyekuwa maabala ya Taifa - Mama Samia tunaomba umrudishe kazini - mwendazake alimwonea bila huruma.
 
Nyamaza huko tunajua unatumika ulitaka kuleta taharuki ya Zika wakati haikuwepo Mwendaze akala kichwa chako.Waliokutuma wakakupa kazi.
Kwani wamekuambia wametishwa?
 
Mwele sijawahi kumwelewa kwa mambo mawili.

1. Kutoheshimu mamlaka yake hata kama ana kitu anakijua na hii inafanya niamimi pengine anatumika. Kwenye Zika alitaka kutupotezea watalii na hadi sasa Zika haijulikani tena. Kiufupi huyu ameshazoea kula pesa za kigeni.
2. Kwa sasa yeye ni WHO anatakiwa afanye kazi ki professional. Hatakiwi kuonesha chuki kwa viongozi wa serikali (Kiongozi Yeyote) maana hii inapunguza mashirikiano ya Serikali na WHO. Pengine tungeppata mtu wa kujivunia sana lakini badala yake tunapata mtu wa kuzodoana na wafanya kazi wa serikali na serikali kwa ujumla. Na kuongeza tu ni kwamba hana mandate ya kutoa mashinikizo wala matamko kwa serikali yeyote, yeye ana mandate ya kushauri tu na kushhawishi. Kwa vile WHO ni ya wazungu anatafanya matamko na migogoro kwa nchi za Kiafrica lakini sio kwa nchi za kizungu kwa sababu anajua kwamba hatakiwi kufanya hivyo.
 
Mkurugenzi wa Magonjwa ya kitropiki kutoka WHO , Dr Mwele Malecela amesema wataalamu wa sekta mbalimbali wafanye kazi kwa kuzingatia weledi bila woga

Dr Mwele kwa sasa anafanya kazi Makao Makuu ya WHO Geneva Uswisi , amesema wataalamu waachwe wafanye kazi kwa weledi ili kupata matokeo chanya dhidi ya ugonjwa wa corona .

Amempongeza Rais Samia kwa hatua anazochukua katika kudhibiti ugonjwa wa Corona .

Chanzo : Mwananchi .

Pia soma;

Thread 'Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi NIMR Dr. Mwele Malecela' Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi NIMR Dr. Mwele Malecela

Thread 'Rais Magufuli amnyooshea kidole Mwele Malecela asema alitumiwa na mabeberu kutangaza ugonjwa 'hewa' wa Zika' Rais Magufuli amnyooshea kidole Mwele Malecela asema alitumiwa na mabeberu kutangaza ugonjwa 'hewa' wa Zika
mtishaji kishajiondokea.
 
Ndivyo mtaalamu anavyotakiwa kuisimamia, kuifafanua, kuelekeza na pia kushauri bila woga.
Tatizo WHO inatumiwa na mabeberu ili kukidhi haja yao! Kwa mabeberu Mwele hana ujanja wala tusidanganyane! Wanamlipa mshahara kupitia michango yao mikubwa kwa WHO! Linapokuja suala lenye maslahi kwa mabeberu hapo hakuna cha weledi wala baba yake na weledi!
 
Tatizo WHO inatumiwa na mabeberu ili kukidhi haja yao! Kwa mabeberu Mwele hana ujanja wala tusidanganyane! Wanamlipa mshahara kupitia michango yao mikubwa kwa WHO! Linapokuja suala lenye maslahi kwa mabeberu hapo hakuna cha weledi wala baba yake na weledi!
Mabeberu ni akina nani ?
 
Wataalam wa bongo kibongobongo....hivi tuna wataalamu wakuweza kuwaweka jukwaa moja na wataalamu let say hata wa hapo kenya kweli...yaani ukaweka hoja mezani halafu uweke mpambano wa uchambuzi kabisa yaaani. Tuache kuzinguana bana.
 
Wataalam wa bongo kibongobongo....hivi tuna wataalamu wakuweza kuwaweka jukwaa moja na wataalamu let say hata wa hapo kenya kweli...yaani ukaweka hoja mezani halafu uweke mpambano wa uchambuzi kabisa yaaani. Tuache kuzinguana bana.
Hapo kenya kuna wataalamu kuwazidi wabongo, kafanye utafiti wako upya....
 
Amerithi kichwa cha marehemu mama yake binti Mwaipopo!!! DNA ya BANYAMBALA.
Kwakweli huyo ni kichwa cha kurithi kutoka kwa marehemu mama yake aliyetokea Tukuyu - Mbeya. Ana tabia/DNA zoote za BANYAMBALA such as; akili nyingi kichwani, kujiamini, hulka yake ya uongozi ni nzuri, kutoyumbishwa, kutokuwa mnafiki, kutojipendekeza n.k

Huyo ana tabia za Kutoka kwenye kabila la mama yake na SIO kutoka Ugogoni.

Keep it up Ntuli!!
 
Back
Top Bottom