BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,365
- 8,097
Makamu wa Rais Dkt. Phili Mpango amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Camillus Wambura, kuangazia malalamiko yanayotolewa na #Wananchi kwa Jeshi la Polisi na kuwachukulia hatua askari wachache wanaoharibu taswira yake.
Dkt. Mpango amelitaka Jeshi hilo kutenda haki pasipo kuonea mtu yeyote na kwa yeyote anayekwenda kinyume na taratibu za nchi achukuliwe hatua kwa mujibu wa Sheria na sio vinginevyo.
IGP Wambura alimtembelea Makamu wa Rais kwa lengo la kujitambulisha mara baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Rais Samia kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania.
Dkt. Mpango amelitaka Jeshi hilo kutenda haki pasipo kuonea mtu yeyote na kwa yeyote anayekwenda kinyume na taratibu za nchi achukuliwe hatua kwa mujibu wa Sheria na sio vinginevyo.
IGP Wambura alimtembelea Makamu wa Rais kwa lengo la kujitambulisha mara baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Rais Samia kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania.