Ndege ya watalii yapokelewa Uwanja wa Kimataifa Kilimanjaro (KIA)

Trubarg

JF-Expert Member
Jan 8, 2020
4,256
6,893
Kwa waliokaribu na TV tune in TBC 1

======



Ndege ya kwanza ya watalii imewasili nchini ikiwa ni baada ya Rais John Magufuli kuruhusu kuendelea kwa shughuli za utalii nchini baada ya kupungua kwa kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya Corona Tanzania.

Tarehe 20, Mei 2020, Mkurugenzi Mwendeshaji wa TTB Devota Mdachi aliahidi ya kuwa mwishoni mwa Mei ndege ya kwanza ingetua nchini.

Waziri Kigwangala

“Tuna matarajio makubwa kuwa sekta ya utalii na usafiri wa anga itafunguka vizuri kadiri tunavyoelekea”

“Hii ni ndege ya kwanza ya abiria ni ya Ethiopian Airlines, marafiki zetu.”

“Kwa kuanzia Ethiopian Airlines watatua Jumatatu, Alhamis na Jumamosi kwa ndege za abiria. Watatua hapa lakini pia Zanzibar. Kwa sasa wameshusha abiria na mizigo Zanzibar wanashusha na hapa Kilimanjaro, wanaenda Addis na nchi nyingine”

“Kwa siku tano za wiki tutakuwa na ndege zinazotua nchini, lakini zinazotuhusu zaidi watu wa utalii zitatua kwa siku tatu -- Jumatatu, Alhamisi na Jumamosi -- ambazo purely ni ndege za abiria wote lakini kwa kiasi kikubwa tunatarajia itakuwa ni watalii”

“Dunia inajifunza namna ya kupambana na janga zito kama hili la mlipuko wa Covid 19 bila kufunga shughuli za kiuchumi na maisha ya watu”

Tumejipanga vizuri na tuna uhakika kutakuwa na usalama wa wageni na wahudumu. Tumefanya ziara ya kukagua mifumo na tumejiridhisha kwamba

Naibu Waziri wa Afya, Dr Godwin Mollel

“Ndani ya nchi maambukizi ya Corona kila siku yanapungu, hii ni kumaanisha kuwa kuna mabo yanafanyika”

“Tumehakikisha kuwa miongozo ya Shirika la Afya Duniani na Wizara ya Afya imefuatwa katika kuchukua tahadhari dhidi ya Covid 19”

Meneja Uwanja wa KIA

“Tupo tayari kuipokea kuutangazia dunia kuwa tupo tayari kupokea wageni.”

“Leo tumefurahi kuona tumepokea ndege ya kwanza”

“Kabla ya corona tulikuwa tunapokea abiria wengi sana. Mwaka jana tulikuwa na abiria 28,000 kwa mwezi na hadi kufikia kipindi cha Corona tulikuwa na wastani wa abiria 19,000”

“Tumejipanga vizuri kuwalinda wageni na wageni dhidi ya Covid 19”
 
Kwa mustakabali na maslai mapana ya Taifa letu John Pombe Joseph Magufuli, haifai kupewa hata dakika moja, au nafasi nyingine ya kuongoza taifa letu, ametutia aibu Sana , ameturudisha nyuma Kama taifa kwa miaka zaida ya 10, hasara aliyotupa wajukuu zetu hawataweza kulipa
 
Kwa mustakabali na maslai mapana ya Taifa letu John Pombe Joseph Magufuli, haifai kupewa hata dakika moja, au nafasi nyingine ya kuongoza taifa letu, ametutia aibu Sana , ameturudisha nyuma Kama taifa kwa miaka zaida ya 10, hasara aliyotupa wajukuu zetu hawataweza kulipa
Hasara ipi?
 
Ni ndege ya shirika la Ethiopia. Imeleta watalii zaidi ya 200. Ni ndege ya abiria.

Corona imeisha tuchape kazi
Du ukisikia kufilisika ndiyo huku. Awamu zote watalii wanakuja lakini awamu hii kuja kwa watalii imekuwa ni habari kubwa kabisa. Ukweli ni kwamba itachukuwa muda mrefu ili hali irudie kama zamani. Nchi kama Thailand zinazoongoza kwa utalii mpaka sasa hali siyo nzuri halafu waje huku ambako takwimu zinafichwa? Watalii 200 ni wachache sana na itachukuwa muda hali ya zamani kurudi.
 
Du ukisikia kufilisika ndiyo huku. Awamu zote watalii wanakuja lakini awamu hii kuja kwa watalii imekuwa ni habari kubwa kabisa. Ukweli ni kwamba itachukuwa muda mrefu ili hali irudie kama zamani. Nchi kama Thailand zinazoongoza kwa utalii mpaka sasa hali siyo nzuri halafu waje huku ambako takwimu zinafichwa? Watalii 200 ni wachache sana na itachukuwa muda hali ya zamani kurudi.
Huwa wanakuja wangapi kwa siku boss?
 
Du ukisikia kufilisika ndiyo huku. Awamu zote watalii wanakuja lakini awamu hii kuja kwa watalii imekuwa ni habari kubwa kabisa. Ukweli ni kwamba itachukuwa muda mrefu ili hali irudie kama zamani. Nchi kama Thailand zinazoongoza kwa utalii mpaka sasa hali siyo nzuri halafu waje huku ambako takwimu zinafichwa? Watalii 200 ni wachache sana na itachukuwa muda hali ya zamani kurudi.
Watalii watakuja tu maana Corona lazima tujifunze kuishi nayo kama yalivyo magonjwa mengine.
 
Kwa mustakabali na maslai mapana ya Taifa letu John Pombe Joseph Magufuli, haifai kupewa hata dakika moja, au nafasi nyingine ya kuongoza taifa letu, ametutia aibu Sana , ameturudisha nyuma Kama taifa kwa miaka zaida ya 10, hasara aliyotupa wajukuu zetu hawataweza kulipa
Mbona unaleta habari nusunusu? Jpm hafai Sasa tuambie Nani anafaa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom