Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,441
- 7,780
Aliyewahi kuwa katibu mkuu wa Chama cha demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) na baadae kuhamia CCM, Dkt. Mashinji amesema Tanzania ni nchi changa na haiitaji kuwa na mabadiliko ya haraka ghafla kwa sababu kila mabadiliko yana athari.
Amesema yakifanyika mabadiliko na yakaja na athari, bado Tanzania halijawa Taifa linaloweza kujitanua kuhimili vishindo vya mabadiliko akitolea mfano mataifa yaliyofanikiwa kufanya mabadiliko kama Zambia na Malawi na kuyumba.
"Wameyumba sana, mpaka Zambia sasa hivi kuna watu wanaisema mtaani imekuwa kama imeuzwa kwa wachina, sasa sielewi kama ni kweli kwa sababu hivi karibuni sijaenda Zambia lakini ni kwa sababu ya haraka ya mabadiliko" Alisema Mashinji
UTAYARI VYAMA VYA SIASA
MASHINJI: Chama cha mapinduzi kimekuwepo siku nyingi kikifanya kazi pamoja na dola, chama ndio kinaongoza serikali na sehemu yake ni dola. Huku nje tunaweza kukaa na kudanganyana wawe huru!
Hakuna kitu ambacho kinatofautisha hivi vitu, huwezi ukawatofautisha executive, mahakama na Bunge. Ni mawazo tu ya kufikirika hata kule Mbinguni kuna baba, mwana na roho lakini maamuzi ni yaleyale kwa sababu hawa wote lengo lao ni kufikia kitu kimoja
CHAMA KUMTEUA MGOMBEA URAIS AMBAE HAKUWEPO
MASHINJI: Mfano uchaguzi ulioisha ambao umeisha na tunasonga mbele na maisha yetu, chama kinakuja na mgombea ambae hakuwepo kwa miaka mitatu. Hakujua shida za watu ni nini zaidi ya kujua kwenye mitandao, mimi naweza kuandika kwenye mtandao huo huo, naweza kusema tu nilikuwa Morogoro wakati niko hapa.
Amekuja hapa, chama makini kilitakiwa kwanza kijitafakari kwamba kweli umekuja, wewe ni maarufu, umefanya kazi nzuri lakini tunachokwenda kuangalia mbele ni kuweka mkuu wa nchi, mtu ambae ana mamlaka ya kusaini hati mtu akanyongwa, kutangaza vita. Juzijuzi hapa tulipigiwa kelele na Malawi kuhusiana na mpaka wa ziwa, tulikuwa na Rais Jakaya Kikwete, mliona utulivu wake, hakupika makelele, tumelimaliza salama.
Umeingia unatangaza upanga kwa upanga, nani atakupigia kura? Ni ngumu. Watanzania unajua ni wajanja, atakusikiliza vizuri wakishakuona unachokisema sio wanachokihitaji kwa wakati huo hawawezi
MASWALI NA MAJIBU
MWANDISHI: Wewe umekuwepo kwenye ofisi kubwa, ulikuwa na nafasi ya kubadilisha mitazamo hii, ulifanya nini?
MASHINJI: Kulikua na hali ya tamaa kwa sababu ukishatengeneza mfumo, mfumo wa maamuzi ambao unatoka chini kuja juu maana yake unatengeneza Taasisi na mara nyingi taasisi hauamua kulingana na mahitaji ya wakati ule na ikija kufanya maamuzi huwa haiangalii umaarufu wa mtu.
Huwa inaangalia nani atatuvusha wakati huu, ukiangalia kwa mfano CCM ni taasisi. Wakati hayati Mkapa anapewa Urais sidhani kama kuna mtu alikuwa anazunguka mtaani anawaza Mkapa atakuwa Rais, kulikuwa na majina ambayo watu walikuwa wanayawaza lakini kwa kuwa ni Taasisi wakayachuja, wakasema anaetuvusha sasa ni huyu na kwa sababu ni kwenye taasisi watu wanaelewana.
Hivyohivyo Kikwete, vivyo hivyo huyu Rais tulienae sasa hivi, mheshimiwa Magufuli ameenda mle na watu maarufu tu, wanajulikana lakini kwa sababu ile ni taasisi na ina ajenda ilijua kabisa kwa ajenda na mfumo tulionao, mtu pekee ambae atatuvusha hapa ni John Magufuli.
Hakuna biashara yeyote utaifanya bila kujua wateja wako ni kina nani, kwa mfani biashara kubwa ya chama cha siasa ni kushinda uchaguzi na uchaguzi utaushindaje? Uchaguzi unaushinda kwenye kituo cha kupigia kura, huushindi uchaguzi kwa kuandamana barabarani wala kwenda kwenye mitandao ya kijamii, kule hamna uchaguzi sanasana utaenda kukera watu na kujinesha wewe ni mtu wa namna gani.
Kushinda uchaguzi unahitaji mambo manne, wagombea, ajenda na tulifanikiwa kupewa ajenda na wapinzani wetu kwamba ni kupinga kila kitu na tulishindwa kuiondoa na mpaka leo wananchi wanajua ajenda yetu ni kupinga kila kitu.
Amesema yakifanyika mabadiliko na yakaja na athari, bado Tanzania halijawa Taifa linaloweza kujitanua kuhimili vishindo vya mabadiliko akitolea mfano mataifa yaliyofanikiwa kufanya mabadiliko kama Zambia na Malawi na kuyumba.
"Wameyumba sana, mpaka Zambia sasa hivi kuna watu wanaisema mtaani imekuwa kama imeuzwa kwa wachina, sasa sielewi kama ni kweli kwa sababu hivi karibuni sijaenda Zambia lakini ni kwa sababu ya haraka ya mabadiliko" Alisema Mashinji
UTAYARI VYAMA VYA SIASA
MASHINJI: Chama cha mapinduzi kimekuwepo siku nyingi kikifanya kazi pamoja na dola, chama ndio kinaongoza serikali na sehemu yake ni dola. Huku nje tunaweza kukaa na kudanganyana wawe huru!
Hakuna kitu ambacho kinatofautisha hivi vitu, huwezi ukawatofautisha executive, mahakama na Bunge. Ni mawazo tu ya kufikirika hata kule Mbinguni kuna baba, mwana na roho lakini maamuzi ni yaleyale kwa sababu hawa wote lengo lao ni kufikia kitu kimoja
CHAMA KUMTEUA MGOMBEA URAIS AMBAE HAKUWEPO
MASHINJI: Mfano uchaguzi ulioisha ambao umeisha na tunasonga mbele na maisha yetu, chama kinakuja na mgombea ambae hakuwepo kwa miaka mitatu. Hakujua shida za watu ni nini zaidi ya kujua kwenye mitandao, mimi naweza kuandika kwenye mtandao huo huo, naweza kusema tu nilikuwa Morogoro wakati niko hapa.
Amekuja hapa, chama makini kilitakiwa kwanza kijitafakari kwamba kweli umekuja, wewe ni maarufu, umefanya kazi nzuri lakini tunachokwenda kuangalia mbele ni kuweka mkuu wa nchi, mtu ambae ana mamlaka ya kusaini hati mtu akanyongwa, kutangaza vita. Juzijuzi hapa tulipigiwa kelele na Malawi kuhusiana na mpaka wa ziwa, tulikuwa na Rais Jakaya Kikwete, mliona utulivu wake, hakupika makelele, tumelimaliza salama.
Umeingia unatangaza upanga kwa upanga, nani atakupigia kura? Ni ngumu. Watanzania unajua ni wajanja, atakusikiliza vizuri wakishakuona unachokisema sio wanachokihitaji kwa wakati huo hawawezi
MASWALI NA MAJIBU
MWANDISHI: Wewe umekuwepo kwenye ofisi kubwa, ulikuwa na nafasi ya kubadilisha mitazamo hii, ulifanya nini?
MASHINJI: Kulikua na hali ya tamaa kwa sababu ukishatengeneza mfumo, mfumo wa maamuzi ambao unatoka chini kuja juu maana yake unatengeneza Taasisi na mara nyingi taasisi hauamua kulingana na mahitaji ya wakati ule na ikija kufanya maamuzi huwa haiangalii umaarufu wa mtu.
Huwa inaangalia nani atatuvusha wakati huu, ukiangalia kwa mfano CCM ni taasisi. Wakati hayati Mkapa anapewa Urais sidhani kama kuna mtu alikuwa anazunguka mtaani anawaza Mkapa atakuwa Rais, kulikuwa na majina ambayo watu walikuwa wanayawaza lakini kwa kuwa ni Taasisi wakayachuja, wakasema anaetuvusha sasa ni huyu na kwa sababu ni kwenye taasisi watu wanaelewana.
Hivyohivyo Kikwete, vivyo hivyo huyu Rais tulienae sasa hivi, mheshimiwa Magufuli ameenda mle na watu maarufu tu, wanajulikana lakini kwa sababu ile ni taasisi na ina ajenda ilijua kabisa kwa ajenda na mfumo tulionao, mtu pekee ambae atatuvusha hapa ni John Magufuli.
Hakuna biashara yeyote utaifanya bila kujua wateja wako ni kina nani, kwa mfani biashara kubwa ya chama cha siasa ni kushinda uchaguzi na uchaguzi utaushindaje? Uchaguzi unaushinda kwenye kituo cha kupigia kura, huushindi uchaguzi kwa kuandamana barabarani wala kwenda kwenye mitandao ya kijamii, kule hamna uchaguzi sanasana utaenda kukera watu na kujinesha wewe ni mtu wa namna gani.
Kushinda uchaguzi unahitaji mambo manne, wagombea, ajenda na tulifanikiwa kupewa ajenda na wapinzani wetu kwamba ni kupinga kila kitu na tulishindwa kuiondoa na mpaka leo wananchi wanajua ajenda yetu ni kupinga kila kitu.