VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mwaka 2015, aliyekuwa Mgombea wa Urais wa CHADEMA Edward Lowassa aliteseka sana. Alisemwa vibaya, alikejeliwa, alidhihakiwa, 'alitukanwa' alidhalilishwa na kutwezwa vya kutosha na kutisha. Lowassa alikosa ushawishi katika jukwaa la kampeni. Alikosa maneno ya kuongea. Aliishia kupata kigugumizi na kutoa salamu ya CHADEMA tu. Watu walijaa kwenye mikutano yake lakini hakuwa na cha kuwaambia kilichowavutia. Ulikuwa mwaka wake!
Mwaka huu, CHADEMA wana mgombea (Tundu Lissu) anayejua kusema, kusimanga, kunanga, kujenga hoja, kukera, kutangaza sera, kushawishi na kutupa vijembe. Mwaka huu makombora yanaelekezwa kwa Dkt. Magufuli, mgombea wa CCM. Yanaelekezwa kwake kwakuwa kwa miaka yote mitano ya awamu yake, ni yeye tu ndiye aliyekuwa akitajwa kwenye kila jambo linalohusu Serikali. Sifa zote alipewa yeye. Sasa apokee na kukosolewa yeye mwenyewe.
Mwaka huu, kwa nilivyomfuatilia, Dkt. Magufuli ameishiwa cha kuzungumza. Ameishiwa hoja. Hana jipya kwenye kampeni zake. Sasa imebaki 'kukopi' na 'kupesti' kutoka kwa Lissu. Mfano, jana tu ameahidi Bima ya Afya kwa kila mtanzania. Ni ahadi na sera ya Lissu tangu mwanzo. Nani kampa Dkt. Magufuli sera hii ya kuiga? Nasema, Dkt. Magufuli aseme mambo mapya; si abaki na yale yale na kuyasema vilevile.
Aseme alichoahidi mwaka 2015; alichofanikiwa na alichoshindwa. Halafu, aseme atawezaje kutimiza kile alichoshindwa. Wakati huohuo, avumilie 'madongo' ya mpnzani wake uchaguzini Lissu na kujibu kwa kutulia. Ajibu kwa kueleweka. Ajibu kwa hoja za haja. Mwaka huu ni mwaka wake, ni zamu yake katika kukosa cha kushawishi ingawa umati wa wananchi 'hukusanywa' na 'kuandaliwa' kutoa tafsiri ya kukubalika kwake.
Abadili santuri. Hakuna kipindi redioni au runingani kinachopiga wimbo mmoja tu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Shinyanga Mjini)
Mwaka huu, CHADEMA wana mgombea (Tundu Lissu) anayejua kusema, kusimanga, kunanga, kujenga hoja, kukera, kutangaza sera, kushawishi na kutupa vijembe. Mwaka huu makombora yanaelekezwa kwa Dkt. Magufuli, mgombea wa CCM. Yanaelekezwa kwake kwakuwa kwa miaka yote mitano ya awamu yake, ni yeye tu ndiye aliyekuwa akitajwa kwenye kila jambo linalohusu Serikali. Sifa zote alipewa yeye. Sasa apokee na kukosolewa yeye mwenyewe.
Mwaka huu, kwa nilivyomfuatilia, Dkt. Magufuli ameishiwa cha kuzungumza. Ameishiwa hoja. Hana jipya kwenye kampeni zake. Sasa imebaki 'kukopi' na 'kupesti' kutoka kwa Lissu. Mfano, jana tu ameahidi Bima ya Afya kwa kila mtanzania. Ni ahadi na sera ya Lissu tangu mwanzo. Nani kampa Dkt. Magufuli sera hii ya kuiga? Nasema, Dkt. Magufuli aseme mambo mapya; si abaki na yale yale na kuyasema vilevile.
Aseme alichoahidi mwaka 2015; alichofanikiwa na alichoshindwa. Halafu, aseme atawezaje kutimiza kile alichoshindwa. Wakati huohuo, avumilie 'madongo' ya mpnzani wake uchaguzini Lissu na kujibu kwa kutulia. Ajibu kwa kueleweka. Ajibu kwa hoja za haja. Mwaka huu ni mwaka wake, ni zamu yake katika kukosa cha kushawishi ingawa umati wa wananchi 'hukusanywa' na 'kuandaliwa' kutoa tafsiri ya kukubalika kwake.
Abadili santuri. Hakuna kipindi redioni au runingani kinachopiga wimbo mmoja tu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Shinyanga Mjini)