Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Miaka mitano ijayo tutawakatia bima ya Afya Wananchi wote wa Tanzania

CCM Damu

Member
Oct 29, 2007
15
28
39C70803-AAB3-4201-B84B-F47125245C70.jpeg


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Magufuli amesema kwa miaka mitano ijayo wakipata ridhaa kutoka kwa wananchi watakata bima ya afya kwa kila Mwananchi.

BC69D08D-69DE-4993-8BB9-615A9728D708.jpeg

Amesema kwanza walikuwa wanaboresha miundombinu na kwa miaka mitano anayoimaliza tayari wameshajenga hospitali na vituo vya afya vya kutosha zoezi linalofuata ni kuwakatia bima watu wote mili60 waliopo Tanzania.

EB8CC244-23B0-4639-AB63-55020C8655BE.jpeg

Amesema jambo la kumpa bima kila mwananchi linawezekana kwa kuwa wanafahamu hela za kutimiza hilo watakapozitoa.

Amesema hadi sasa wameshaajiri madaktari zaidi ya 1,000 na watumishi wa afya zaidi ya 14,000. Anasema wamepanga kwa kuwa wanajua watakavyotekeleza.
9A636AC3-7F1A-4179-B97B-B131E85051AB.jpeg
 
Uongo mwengine hata hauhitaji mtu kukuambia unaongopewa. Mwaka 2015 alisema atavifufua viwanda vilivyokufa, miaka mitano imepita kuna viwanda lukuki vimefungwa kutokana na ugumu wa uzalishaji pamoja na gharama za uendeshaji kuwa juu, leo hii anasema tena atafufua viwanda vilivyokufa.

Ikifika 2025 watasema watahakikisha wanawahakikishia wananchi wenye bima ya afya wanapatiwa huduma hospitali yoyote nchini mana kuna mahospitali nina uhakika yatakuwa hayatoi huduma kwa wanachama wa bima ya Taifa kutokana na malipo kudorora kama ilivyo sasa.
 
Hizi comments zinaonyesha ni namna gan hawa CCM wamechokwa,, ukiwauliza wanasema hili ni kundi dogo la mitandaon sasa najiuliza ukienda twitter hapafai hamna anaetaka sikia neno CCM, ukija hapa ndio kabisa, ukipita vijiwen hapafai kabiss, ukienda vijijin wazee wanatoa machoz waonapo upinzani sasa najiuliza hilo kundi lao kubwa liko waap?
 
Hizi comments zinaonyesha ni namna gan hawa ccm wamechokwa,, ukiwauliza wanasema hili ni kundi dogo la mitandaon sasa najiuliza ukienda twitter hapafai hamna anaetaka sikia neno ccm, ukija hapa ndio kabisa, ukipita vijiwen hapafai kabiss, ukienda vijijin wazee wanatoa machoz waonapo upinzani sasa najiuliza hilo kundi lao kubwa liko waap?

Kundi lao lipo kwenye vyombo vya dola Mkuu.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom