Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Magufuli amesema kwa miaka mitano ijayo wakipata ridhaa kutoka kwa wananchi watakata bima ya afya kwa kila Mwananchi.
Amesema kwanza walikuwa wanaboresha miundombinu na kwa miaka mitano anayoimaliza tayari wameshajenga hospitali na vituo vya afya vya kutosha zoezi linalofuata ni kuwakatia bima watu wote mili60 waliopo Tanzania.
Amesema jambo la kumpa bima kila mwananchi linawezekana kwa kuwa wanafahamu hela za kutimiza hilo watakapozitoa.
Amesema hadi sasa wameshaajiri madaktari zaidi ya 1,000 na watumishi wa afya zaidi ya 14,000. Anasema wamepanga kwa kuwa wanajua watakavyotekeleza.