Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Mchagueni Jah people kwa sababu hatuchagui digrii, mkiniletea wale wa alama ya "manati" sitawaelewa!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,779
141,667
Dkt. Magufuli amewataka wananchi wa Makambako wamchague Mgombea Ubunge wa CCM Jah people kwa sababu kwenye ubunge hatuchagui degree bali mtu.

Dkt. Magufuli amesema Jah people salamu yake ni Kidumu chama cha mapinduzi hivyo wakimleta bungeni wataelewana ila wakimleta yule anayesalimia kwa alama ya manati sitawaelewa.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
 
JPM yeye keshapita anachofanya sasa ni kuwaomba wananchi wampe wagombea wote wawe wa CCM ila iwe rahisi kutekeleza ilani ya CCM.
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Unatofautishaje mtu na degree, au siku hizi degree ni kitu kinachojitegemea? huyu mtu hafai kuwa kiongozi.
 
Mzee anakosea.
Kwahiyo wamchague tu huyo Jah hata kama hawamtaki!?

Kavurugwa huyu alidhani mambo yatakuwa mepesi, ndio maana anatumia vitisho kulazimisha watu wamchague mtu ambaye ni wa Chama chake.
Siasa za Chuki na roho mbaya hazitakiwi kwa Nchi yetu ambayo imetawaliwa na Amani na upendo.
 
Dkt. Magufuli amewataka wananchi wa Makambako wamchague mgombea ubunge wa CCM Jah people kwa sababu kwenye ubunge hatuchagui degree bali mtu.

Dkt. Magufuli amesema Jah people salamu yake ni Kidumu chama cha mapinduzi hivyo wakimleta bungeni wataelewana ila wakimleta yule anayesalimia kwa alama ya manati sitawaelewa.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Lini amenza kuona wasio na Elimu wanauwezo mbona kawatoa walimu na wakufunzi wetu vyuoni. Huyu.hafai hata kuliwa na ugali mkavu
 
Mungu tuondolee mtu mwenye Chuki, roho mbaya na ubaguzi kwa sababu ya kiti cha uraisi
Mungu wetu ana kazi nyingi za kuumba binadamu wenye roho safi wa kuchagua badala ya shetani tunayemwona na kumbeba anayepaswa kutupiliwa
mbali tuchague binadamu aliyeshinda mauti kwa uweza wa Mungu mwenyewe na tumwombe ampake mafuta na kumbariki. Tuachane na msema uongo mpenzi wa shetani!
 
Back
Top Bottom