Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,499
- 9,279
RAIS Dk. John Magufuli amewataka Watanzania kutumia utashi wao kuchagua viongozi wanaowafaa, watakapokwenda kwenye vituo vya kupigia kura kesho.
Akizungumza jana wakati wa uzinduzi wa msikiti uliojengwa katika Wilaya ya Chamwino jijini Dodoma, aliwataka Watanzania kuhamasishana kwenda kupiga kura kisha kurudi nyumbani.
“Tarehe 28 tuitumie kujenga mazuri, tuitumie katika kujenga umoja wa Tanzania, tukapige kura kulingana na utashi wa mioyo yetu.
“Naomba muhamasishane wote kapigeni kura, ukimaliza nenda nyumbani, fujo hazijengi nchi, Tanzania ni ya amani, pakiwa na fujo huwezi ukafanya biashara, huwezi ukaenda hata msikitini, kanisani.
“Tunataka amani ikatawale baada ya uchaguzi kwa sababu kuna maisha baada ya uchaguzi,” alisema Dk. Magufuli.
Aliwataka Watanzania kuendelea kudumisha umoja na mshikamano, na kamwe wasikubali kuvivuruga kwa misingi ya dini, kabila, rangi au itikadi za kisiasa kwani ni tunu ambayo waasisi wameiacha.
“Sifa kubwa inayoitofautisha Tanzania na mataifa mengine ni umoja na mshikamano uliopo nchini, zipo baadhi ya nchi zimeingia kwenye vita sababu ya dini, makabila, rangi, lakini Tanzania imejaliwa kuwa na umoja na wananchi hawabaguani.
“Unaweza kwenda kwenye familia utakuta mume Mchaga, mke Mgogo au wazazi Waislamu, mtoto ni Mkristu na wanaishi kwa upendo.
“Sifa hii tuliyonayo haikutokea bahati mbaya, ni matokeo ya kazi kubwa iliyofanywa na waasisi wa taifa hili, hayati Mwalimu Nyerere na (Abeid Amani) Karume kwa kujenga taifa lenye umoja na mshikamano, ambalo leo tunafurahia matunda yake,” alisema Dk. Magufuli.
Mtanzania
Akizungumza jana wakati wa uzinduzi wa msikiti uliojengwa katika Wilaya ya Chamwino jijini Dodoma, aliwataka Watanzania kuhamasishana kwenda kupiga kura kisha kurudi nyumbani.
“Tarehe 28 tuitumie kujenga mazuri, tuitumie katika kujenga umoja wa Tanzania, tukapige kura kulingana na utashi wa mioyo yetu.
“Naomba muhamasishane wote kapigeni kura, ukimaliza nenda nyumbani, fujo hazijengi nchi, Tanzania ni ya amani, pakiwa na fujo huwezi ukafanya biashara, huwezi ukaenda hata msikitini, kanisani.
“Tunataka amani ikatawale baada ya uchaguzi kwa sababu kuna maisha baada ya uchaguzi,” alisema Dk. Magufuli.
Aliwataka Watanzania kuendelea kudumisha umoja na mshikamano, na kamwe wasikubali kuvivuruga kwa misingi ya dini, kabila, rangi au itikadi za kisiasa kwani ni tunu ambayo waasisi wameiacha.
“Sifa kubwa inayoitofautisha Tanzania na mataifa mengine ni umoja na mshikamano uliopo nchini, zipo baadhi ya nchi zimeingia kwenye vita sababu ya dini, makabila, rangi, lakini Tanzania imejaliwa kuwa na umoja na wananchi hawabaguani.
“Unaweza kwenda kwenye familia utakuta mume Mchaga, mke Mgogo au wazazi Waislamu, mtoto ni Mkristu na wanaishi kwa upendo.
“Sifa hii tuliyonayo haikutokea bahati mbaya, ni matokeo ya kazi kubwa iliyofanywa na waasisi wa taifa hili, hayati Mwalimu Nyerere na (Abeid Amani) Karume kwa kujenga taifa lenye umoja na mshikamano, ambalo leo tunafurahia matunda yake,” alisema Dk. Magufuli.
Mtanzania