Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Hamasishaneni mkapige kura kesho. Ukimaliza rudi nyumbani ili kuitunza tunu ya amani na mshikamano tulionao

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
RAIS Dk. John Magufuli amewataka Watanzania kutumia utashi wao kuchagua viongozi wanaowafaa, watakapokwenda kwenye vituo vya kupigia kura kesho.

Akizungumza jana wakati wa uzinduzi wa msikiti uliojengwa katika Wilaya ya Chamwino jijini Dodoma, aliwataka Watanzania kuhamasishana kwenda kupiga kura kisha kurudi nyumbani.

“Tarehe 28 tuitumie kujenga mazuri, tuitumie katika kujenga umoja wa Tanzania, tukapige kura kulingana na utashi wa mioyo yetu.

“Naomba muhamasishane wote kapigeni kura, ukimaliza nenda nyumbani, fujo hazijengi nchi, Tanzania ni ya amani, pakiwa na fujo huwezi ukafanya biashara, huwezi ukaenda hata msikitini, kanisani.

“Tunataka amani ikatawale baada ya uchaguzi kwa sababu kuna maisha baada ya uchaguzi,” alisema Dk. Magufuli.

Aliwataka Watanzania kuendelea kudumisha umoja na mshikamano, na kamwe wasikubali kuvivuruga kwa misingi ya dini, kabila, rangi au itikadi za kisiasa kwani ni tunu ambayo waasisi wameiacha.

“Sifa kubwa inayoitofautisha Tanzania na mataifa mengine ni umoja na mshikamano uliopo nchini, zipo baadhi ya nchi zimeingia kwenye vita sababu ya dini, makabila, rangi, lakini Tanzania imejaliwa kuwa na umoja na wananchi hawabaguani.

“Unaweza kwenda kwenye familia utakuta mume Mchaga, mke Mgogo au wazazi Waislamu, mtoto ni Mkristu na wanaishi kwa upendo.

“Sifa hii tuliyonayo haikutokea bahati mbaya, ni matokeo ya kazi kubwa iliyofanywa na waasisi wa taifa hili, hayati Mwalimu Nyerere na (Abeid Amani) Karume kwa kujenga taifa lenye umoja na mshikamano, ambalo leo tunafurahia matunda yake,” alisema Dk. Magufuli.

Mtanzania
 
Neno Haki siku hizi limekuwa marufuku kutamkwa Lumumba.

Wanazungumzia amani kama vile ni bahati tuliyopendelewa na Mungu, kumbe imetokana na uoga wa watanzania kudai haki zao hata pale wanapoonewa wazi.

Safari hii wanasisitiza haki kwanza, amani itafuata yenyewe baadae.
 
Haki Inaenda Kutendeka Zanzibar. Je, Kuna sababu gani ya Kufanya uchaguzi kama unataka chama chako na watu wako ndio wachaguliwe tu. Kuamasisha watu kupiga kura ni jambo moja , Kuwapa haki yao ni jambo la muhimu sana katika kulinda Amani. Otherwiae hakuna sababu ya kupiga kura.. kama ukiporwa ushindi ni kulidhika tu na kusema sawa. Haki....Haki...Haki!
 
Siendi KUPIGA KURA.
Bora nilale tu..
Mimi masuala ya kutishana tishana siyataki.
 
Watanzania wenzengu nawasihi kesho kwa mamilioni yetu tukapige kura kwa amani na utulivu. Tutii sheria na maelekezo yote tutakayopewa ili zoezi hilo liishe kwa amani na utulivu. Tukumbuke kuna maisha baada ya uchaguzi. Asitokee yeyote kutushawishi na tukakubali kuvunja sheria. Maumivu yake yatakuwa mwakubwa kwetu huku aliyetushawishi akitazama runinga kwa raha na familia yake.

Tujiongeze, akili za kuambiwa tuongeze na zetu. Kwa wale wapenda maendeleo kama mimi naomba kwa unyenyekevu kabisa tumchague Dkt Magufuli na wabunge na madiwani wa CCM. Usifanye makosa katika uchaguzi wako. Mungu atubariki sote, Mungu aibariki mama yetu Tanzania, nchi tunayoipenda kuliko maelezo.
 
Turudi nyumbani ili mpate fursa ya kuhujumu mawakala eti? HATUDANGANYIKI, tutapiga kura na kuzilinda hadi pale matokeo yatakapobandikwa vituoni na washindi watakapotangazwa. Mjulishe hivyo ndugu JIWE.
 
Time fikia tamati ya kipindi cha uchaguzi. Kipindi hiki sio cha ku nenepesha ng'ombe siku ya mnada wala kutumia wafuasi vibaya bali ni muda wa ku kubali matokeo na ku heshimu maoni ya watanzania wote.

Watanzania wafahamu kwamba wana siasa wana weza kuwa tumia kwa njia moja au nyingine ku kamilisha mipango yao au ku wasilisha hoja zao kwa njia ambazo sio sahihi. Njia hizi mara nyingi zinaweza ku sababisha vifo vya watu wasio na hatia na ku sababisha uharibifu mkubwa wa mali na mazingira.

Kabla ya kufanya chochote jua kwamba wana siasa wataishia kupunga upepo kwenye ufukwe wa bahari ila wewe utaishia kutumikia kifungo ambacho ungeweza ku kwepa kiurahisi

Tafakari,
Jumatano njema.
 
Neno HAKI sijaliona kwny hio story yote.
Haki Inaenda Kutendeka Zanzibar.. Je Kuna sababu gani ya Kufanya uchaguzi kama unataka chama chako na watu wako ndio wachaguliwe tu. Kuamasisha watu kupiga kura ni jambo moja , Kuwapa haki yao ni jambo la muhimu sana katika kulinda Amani. Otherwiae hakuna sababu ya kupiga kura.. kama ukiporwa ushindi ni kulidhika tu na kusema sawa. Haki....Haki...Haki.
Mnataka UHURU na HAKI wakati ndio msingi wa kila mtu.

Kwa UHURU wako unajiandikisha kupiga kura ambayo ni HAKI yako

Wakati wa kampeni umetumia UHURU wako kwenda kusikiliza na kutimiza HAKI yako

Leo uko HURU kwenda kumpigia kura mgombea unayempenda ambayo ni HAKI yako

Baada ya kupiga kura kwa UHURU na kutimiza HAKI yako, ili usivuruge UHURU na HAKI ya mwenzako kupiga kura rudi nyumbani ili AMANI itamaraki
 
Zee linafiki sana hili. Watu wanakaa kulinda kura 200m from the station, wametulia, polisi wake aliowatuma ndiyo wanakua wa kwanza kuleta fujo. Kukaa kusubiri matokeo ni fujo? Dikteta ushenzi, no wonder hata internet wamechakachua.
 
Neno HAKI sijaliona kwny hio story yote.
Hakuna haki duniani ila Kuna utawala washeria.
Ajabu ni kwamba aliyewamezesha neno haki ni wakili na kawaida ya wakili ni kuminya haki ya mwingine kwa kumtetea mteja wake.
Mfano Jambazi limeuwa na kuiba, likiwa na pesa na wakili mzuri linaweza kumshinda ktk kesi yule aliyeuwawa na kuibiwa. Je hii ndio HAKI?
 
Hakuna haki duniani ila Kuna utawala washeria.
Ajabu ni kwamba aliyewamezesha neno haki ni wakili na kawaida ya wakili ni kuminya haki ya mwingine kwa kumtetea mteja wake.
Mfano Jambazi limeuwa na kuiba, likiwa na pesa na wakili mzuri linaweza kumshinda ktk kesi yule aliyeuwawa na kuibiwa. Je hii ndio HAKI?
Ulivyo zuzu haujui hata hilo neno HAKI askofu Bagonza ndiye aliyekua analisisitiza kila mara.
JamiiForums-1874524951_428x320.jpg
 
Back
Top Bottom