Dkt. Lwaitama: Hawa jamaa (CCM) wakiendelea hivi, hata mwakani chama pinzani chenye kujiheshimu kitajitoa

Napingana sana na watu kama hawa, wanaotaka kutuaminisha kuwa siasa za Mwl Nyerere zilikuwa bora sana kuliko za leo.
Nyerere aliye binya uhuru wa kupata habari kiasi cha kutulazimisha kusikia mapambio ya siasa za ujamaa kupitia RTD pekee. Kulazimisha wote tutumie radio zisizo na masafa ya kupata taarifa toka nje ya Tanzania (177) maarufu Mkulima na ukibahatika kuipata yenye masafa hayo unasikilizia kwenye uvunguni.
Watu binafsi walinyimwa uhuru wa kuzalisha mali kwa kutengenezewa taswira ya ubepari na kutiwa kizuizini, kiasi wenye hasira waliua wakuu wa mikoa na kunyongwa. Ukiingia bar unahesabiwa vizibo vikizidi unadakwa ukaeleze umepata wapi pesa ya kununua chupa 24 na huwezi kumnunulia rafiki yako isije kuwa kesi.
Tulilazimishwa kutumia baiskeli hata kama una uwezo wa kuwa Peargot lazima ujadiliwe na Kamati kuu ya TANU kama unastahili sifa za kuwa na gari hiyo vinginevyo tumia baiskeli ya Swala.
Hatukuwa na uhuru wa kujumuika na kuongea juu ya serikali na mkiipata mnaongea kwa kunong'onezana tukiaminishwa Ikulu inasikia lolote linaloongelewa juu ya serikali.

Lwaitama usitukumbushe ya Nyerere
Huyo mzee atawapata hawa wadogo zetu ambao hawakuwa wamezaliwa enzi za awamu ya kwanza.

Meza za magazeti pale posta mpya Jumatatu mpaka ijumaa zilikuwa na magazeti mawili tu Daily News na Uhuru, Jumamosi linaongezeka mfanyakazi.

Enzi zetu meza za magazeti zimejaa ya kila sina, kwenye mitandao kila mtu anaandika anachotaka.

Anachosahau huyo mzee ni kwamba kuna maisha ya wanaharakati yapo mtandaoni na kuna maisha halisi huko mikoani, awamu hii inapambana ili maisha halisi yaboreshwe.
 
Huyo mzee atawapata hawa wadogo zetu ambao hawakuwa wamezaliwa enzi za awamu ya kwanza.

Meza za magazeti pale posta mpya jumatatu mpaka ijumaa zilikuwa na magazeti mawili tu daily news na uhuru, jumamosi linaongezeka mfanyakazi.

Enzi zetu meza za magazeti zimejaa ya kila sina, kwenye mitandao kila mtu anaandika anachotaka.

Anachosahau huyo mzee ni kwamba kuna maisha ya wanaharakati yapo mtandaoni na kuna maisha halisi huko mikoani, awamu hii inapambana ili maisha halisi yaboreshwe.
Na yeye na wenzake ndio waliokuwa waalimu wa Siasa, wakituaririsha zidumu fikra za Mwalimu. Wakimaanisha wao na usomi wao walikuwa hawana uwezi wa kufikiri kama JKN.
 
Sawa Ila unamwamini Doctor wa maganda ya korosho
Yaani Lwaitama "Commedian" naye wakumwamini kiasi hicho? Kwali mmechanganyikiwa na hammjui Lwatama! Hana lolote huyo mnapoteza muda wenu tena huwa anataka kuwaaminisha yeye kuwa ni Prof. wakati ni uongo hajafikia level hiyo!
 
Na yeye na wenzake ndio waliokuwa waalimu wa Siasa, wakituaririsha zidumu fikra za Mwalimu. Wakimaanisha wao na usomi wao walikuwa hawana uwezi wa kufikiri kama JKN.
Kingine anachopotosha jamii ni ukweli kuwa kuanzia awamu ya kwanza nchi imekuwa ikisomesha wataalam, ni lazima ufike muda wale waliosomeshwa wakatumia maarifa yao kwa faida ya wote.

Hatuwezi kuwa na mindset ya siasa tu wakati taifa linavidai vizazi maendeleo yenye kuonekana.
 
Hahaha..lwaitama bhana, anapiga ngumi za uso kama anafanya mzaha vile

Huko aliko meko anaugulia. Hajalala leo usiku.

Yaani meko bhana, sijui kwa nini aliamua aanze udikteta. Aliyofanya yanajitosheleza tu kugombea na kupewa kura.

Ila anayemshauri ni mtu mmoja stupid sana na arrogant... more than stupid
 
Aisee huyu mzee ni mkweli kabisa lkn hata pendwa na na viongozi wa serikali hii.
Anaweza kuuawawa kwa kauli kama hizi tu za kusema ukweli, uovu unapata nguvu sana siku hizi.

Pia utaona wasaidizi wa mhimili huu watamtolea maneno ya kumtukana ili kumfurahisha mkuu wao. MUNGU tu atusaidie harafu dini kumbe haisaidii hao hao wanajifanya kusali sana wenye unyenyekevu sana machoni pa watu. Halafu ndiyo waovu sana wasio na huruma wenye kuchukua haki za watu kwa nguvu.

Ukiona na kushuhudia wanayo fanya waliochini yao mpk maskio yana kuwasha.

MUNGU mlinde mzee huyu angalau twaweza sikia au kupata punje ya maneno ya haki kutoka kwake.
Cha ajabu viongozi wa dini wananwanyenyekea na kuungana na hao wengine kutukana watu wanaosema ukweli

Nchi imeoza hii mkuu
 
Napingana sana na watu kama hawa, wanaotaka kutuaminisha kuwa siasa za Mwl Nyerere zilikuwa bora sana kuliko za leo.

Nyerere aliye binya uhuru wa kupata habari kiasi cha kutulazimisha kusikia mapambio ya siasa za ujamaa kupitia RTD pekee. Kulazimisha wote tutumie radio zisizo na masafa ya kupata taarifa toka nje ya Tanzania (177) maarufu Mkulima na ukibahatika kuipata yenye masafa hayo unasikilizia uvunguni.

Watu binafsi walinyimwa uhuru wa kuzalisha mali kwa kutengenezewa taswira ya ubepari na kutiwa kizuizini, kiasi wenye hasira waliua wakuu wa mikoa na kunyongwa. Ukiingia bar unahesabiwa vizibo vikizidi unadakwa ukaeleze umepata wapi pesa ya kununua chupa 24 na huwezi kumnunulia rafiki yako isije kuwa kesi.

Tulilazimishwa kutumia baiskeli hata kama una uwezo wa kuwa Peargot lazima ujadiliwe na Kamati kuu ya TANU kama unastahili sifa za kuwa na gari hiyo vinginevyo tumia baiskeli ya Swala.

Hatukuwa na uhuru wa kujumuika na kuongea juu ya serikali na mkiipata mnaongea kwa kunong'onezana tukiaminishwa Ikulu inasikia lolote linaloongelewa juu ya serikali.

Lwaitama usitukumbushe ya Nyerere
Wewe jamaa bhana umesikiliza audio kweli

Hadi nyerere kamponda na kusema ukweli
 
Wewe jamaa bhana umesikiliza audio kweli

Hadi nyerere kamponda na kusema ukweli
Labda aanze leo, huyu ndie Lwaitama nimsikiae kila leo. Nyerere na demokrasia???
 
Labda aanze leo, huyu ndie Lwaitama nimsikiae kila leo. Nyerere na demokrasia???
Nmesema kwenye hyo video

Hivi una akili wewe?
 
Mimi naishangaa serikali ya CCM. Juzi kati wametoka kutoa matamko kwamba Zimbabwe iondolewe vikwazo bila kujiuliza ilikuwaje Zimbabwe imefika hapo ilipofika.Naiona Tanzania inaendakuwa kama Zimbabwe, na serikali ya CCM ndio itaifikisha hapo!
 
Sisi hatujaomba atukopeshe fedha tunasikiliza alichokisema na kimeeleweka sasa kama hutaki tumwamini lete yako kwako tuamini kua alichosema hakipo.kwani hakuna uhuni kwenye chaguzi hata mrema mpendwa wa Rais amelalamika,Kwani hakuna maandamano yaliyotekea Sudani,Tunisia, Algeria, unataka tuone lipi la uwongo.
Yaani Lwaitama "Commedian" naye wakumwamini kiasi hicho? Kwali mmechanganyikiwa na hammjui Lwatama! Hana lolote huyo mnapoteza muda wenu tena huwa anataka kuwaaminisha yeye kuwa ni Prof. wakati ni uongo hajafikia level hiyo!
 
Back
Top Bottom