Dkt. Lwaitama atoa somo kuntu kuhusu demokrasia ya Tanzania, awaonya vijana wa CHADEMA

Rasterman

JF-Expert Member
Feb 24, 2015
33,905
44,011
Akitoa maoni yake Dr. Azavel Lwaitama mdau mkubwa katika harakati za kutafuta nchi yenye demokrasia iliyo stawi yenye maridhiano, umoja, uhuru na maendeleo amesikika huko Clubhouse kwenye mjadala wa moto unaohudhuriwa na watu wengi kuliko jukwa lingine lolote la kijamii.

Dr Lwaitama amewataka watawala na wadau woote wa siasa za tanzania kuwa wapole na wavumilivu ili kila raia achague upande wake anaopendezwa nao.

Kuhusu swala la katiba mpya Dr Lwaitama amesema kuwa Maridhiano ni serikali kuruhusu vyama na wadau mbali mbali kila upande utangaze sera na itikadi zake bila kufukuzana.

Lwaitama ambaye alikamatwa Mwaka jana akiwa katika kongamano la kutoa elimu ya Katiba mpya kwa vijana huko Mwanza amesema kuwa kuwindana na kufukuzana ni jambo la ajabu na linatia aibu.

Ameshauri vijana, wazee, matajiri kwa maskini kila mtu aachwe atafakari. Wanaotaka katiba mpya wahamasishane na wasio taka pia waachwe wahamasishane na mwisho wa siku Wananchi wataamuwa wenyewe badala ya kile kinachofanykka sasa.

Amewataka vijana wa chadema waache kupoteza muda kujibizana na vijana wa ACT kuhusu matakwa yao ya Tume huru ya uchaguzi kwanza na kwamba hiyo ndio demokrasia ya vyama vingi kuwa na mawazo huru.


Wito kwa serikali na vyombo vyake pia umetolewa kwa kuruhusu wananchi wafanye na kutekeleza wajibu wao wa kikatiba bila kusumbuliwa na mwisho wa siku Wananchi wenyewe wataamuwa kama wanataka katiba mpya au la! badala ya kutumia malungu.

Msikilize Mwanazuoni Huyu hapa.

 
Anasema anayetaka aendelee kutawala aendelee kutawala na wananchi nao waachwe wafanye wanachotaka.
 
Kujibishana kuna ubaya gani, kama hakusababishi rabsha. Kujibishana huko ndiko kunakoleta uelewa wa pande zote mbili zinazojibishana, na hatimaye kushawishiana kuhusu misimamo yao.

Aseme watu wawe na utayari wa kusikiliza maoni ya wengine, kuyapima na kukubaliana nayo au kuyakataa kwa kueleza sababu za kukubali au kukataa.

Nchi isiyojibishana, labda itakuwa ni China.
 
Eeeh Heee, naona umemwelewa vizuri, kama kweli aliyoeleza ni kama hayo yaliyoandikwa hapo juu.
Amefafanua vizuri sana. Pitia hiyo link ya Youtube.

Hakuna haja ya kupigana mawe. Madai ya Katiba Mpya hakuna haja ya kugombana. Shida ni nini?? Dr amenikosha sana.
 
Kujibishana kuna ubaya gani, kama hakusababishi rabsha. Kujibishana huko ndiko kunakoleta uelewa wa pande zote mbili zinazojibishana, na hatimaye kushawishiana kuhusu misimamo yao.

Aseme watu wawe na utayari wa kusikiliza maoni ya wengine, kuyapima na kukubaliana nayo au kuyakataa kwa kueleza sababu za kukubali au kukataa.

Nchi isiyojibishana, labda itakuwa ni China.
Ndio kuwe kubishana kwa kuelimishana mwisho wa siku tukubaliane tunataka nini.
 
Amefafanua vizuri sana. Pitia hiyo link ya Youtube.

Hakuna haja ya kupigana mawe. Madai ya Katiba Mpya hakuna haja ya kugombana. Shida ni nini?? Dr amenikosha sana.
"Shida ni nini"?
Dokta anauliza swali lilo wazi. Hajui kwa nini CCM haitaki Katiba mpya?
 
"Shida ni nini"?
Dokta anauliza swali lilo wazi. Hajui kwa nini CCM haitaki Katiba mpya?
Swali analilejea akijuwa na wao wanajua. Wao waendelee kutawala. Sisi tuendelee kufundishana kuhusu umuhimu wa katiba mpya
 
Somo zuri ila sijui kama vijana wa Chadema watamuelewa maana huko nyuma baadhi ya viongozi waliopingana na mawazo ya vijana wa Chadema waliambiwa kuwa wamenunuliwa.
 
Somo zuri ila sijui kama vijana wa Chadema watamuelewa maana huko nyuma baadhi ya viongozi waliopingana na mawazo ya vijana wa Chadema waliambiwa kuwa wamenunuliwa.
Wataelewa kwa sababu ni Somo kweli kweli na limefundishwa kinaga ubaga. Shida itakuja kwa hao wasiotaka katiba Mpya watasikia?
 
Kujibishana kuna ubaya gani, kama hakusababishi rabsha. Kujibishana huko ndiko kunakoleta uelewa wa pande zote mbili zinazojibishana, na hatimaye kushawishiana kuhusu misimamo yao.

Aseme watu wawe na utayari wa kusikiliza maoni ya wengine, kuyapima na kukubaliana nayo au kuyakataa kwa kueleza sababu za kukubali au kukataa.

Nchi isiyojibishana, labda itakuwa ni China.
🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom