Hii movie ndo kwanza imeanza tusubiri kuna mengi ya kujifunza,Kamanda Mambosasa anatamani iishe
UmenifilisiNakubaliana na wewe. Dr kuna kitu hajakisema na hajakiweka wazi.
1. Alipata wapi mtaji wa kuanzisha a very successful business within a short period of time baada ya kumaliza shule?
2. Ilikuaje ubalozi wa marekani wajihusishe kumtorosha kutoka urusi tena kwa ndege ya malkia wa uholanzi hadi Armsterdam na kisha kuja Dar kama anavyosema.
3. Baada ya kufika hapa nchi alipata wapi nauli ya kumpeleka Malaga Hispania na akaweza kuishi huko kwa miaka 8 hafi aliporudi nchini mwaka 2013.
4. Kwa nini baada ya kutoroka toka Urusi bado amekua na wasiwasi kua warusi watamtafta popote alipo wamuue, wasiwasi wake ni wa nini? Kweli vibaka wanaweza kukufuatilia hadi nje ya nchi wakuue?!
5. Anasema warusi wana chuo cha kufundisha jinsi ya kuua, tena anataja KGB ambayo ni taasisi ya serikali, je alitekwa na KGB au alitekwa na vibaka, vibaka gani wanaweza kusomea chuo kikuu jinsi ya kuua mtu na jinsi ya kumtesa?
6. Anasema hataki kuwasiliana na mke wake wasije kumtambua alipo, kwamba simu zote zinarekodiwa ziazotoka nje, hao ambao anahofu kua watamjua alipo ni wale vibaka waliomteka au watu wengine, vibaka wanawezaje kurekodi au kuingilia mawasiliano ya watu toka nje ya nchi?
7. Dr alikimbilia hispania ili kupoteza ushahidi wa uwepo wake, kisha akarudi Tanzania ili kuwapoteza tena kama wanadhani yuko hispania, ni kina nani hao ambao dr anawakimbia kiasi hicho, wale vibaka waliomteka au wengine?
Dr ana kitu hataki kukisema. Kuna kitu kimejificha nyuma yake.
Zaidi Dr ni loser, huwezi kwenda kusoma ukalowea huko ukasahau hata wazazi wako.
Hihihiiii..jamaa anafunga mwaka huyu.mpaka nimemkumbuka babu wa samunge alivyotikisa enzi zake,mwaka huu ni wa Dr