Dkt. Kipilimba, sasa yatosha!

My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,283
Kwa mara ya tatu tena nakuandikia Mzee wangu Dr Modestus Kipilimba, mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa taifa, TISS.

Natamani sana, Rais Magufuli awe wa kwanza kusoma hii mada kabla yako.

Nimeshindwa kuendelea na kazi niliyokuwa naifanya usiku huu kwenye Computer, moyo wangu umekosa amani kabisa hadi niandike hii mada.

Dr. Kipilimba, unadhani bado unastahili kuongoza Idara nyeti na muhimu Kama hii ya TISS?

Kwanini mikononi mwako serikali ya awamu ya tano inadhalilika sana kimataifa?

Kwanini Idara yako imeruhusu uwepo wa watu Kama Musiba wanaokashifu viongozi wakubwa hadharani?

Sikufundishi kazi, ila nashangaa kwanini hujui kuwa idara kama TISS ndo Roho kamili ya Tanzania.

Kifo cha TISS ni kifo cha Tanzania, kwanini hujifunzi magumashi ya CIA, MI5, Mossad na mashirika mengineyo kama TISS?

Ninaposema magumashi nadhani umeelewa vizuri kabisa, maana nikielezea itahitaji kitabu.

Uimara wa TISS ndo Uimara wa Tanzania, na udhaifu wa TISS ndo udhaifu wa Tanzania.

Tunajua ya kwamba dawa ya Deni ni kulipa, lakini ilikuwaje TISS ikashindwa kubaini kuwa Steyn kafungua shauri mahakamani dhidi ya Tanzania kudai mali yoyote ya nchi ikamatwe?

TISS ingeitaarifu serikali basi, ndege isingeenda SA, na hivyo wangetafuta namna nyingine ya ku-solve tatizo.

Ni aibu kubwa mno nchi kudaiwa na raia mmoja Halafu mali ya nchi kukamatwa kwa Deni nje ya nchi, hii fedheha kubwa.

TISS mngeweza kuepusha hii fedheha. Kama TISS, ilishindwa kubaini njama za kutaifisha mali ya nchi, je itaweza kujua nini kinapangwa Somalia na Alshabab kwa mfano juu ya nchi?

Dr Kipilimba, TISS chini yako ni dhaifu mno, nakushauri u resign tu. TISS chini ya Dr Hansy Kitine na hayati Imran Kombe ilikuwa imara kupindukia.

Nakumbuka Tukio moja (siwezi kulitaja) nilikuja kushtuka mission accomplished muda mrefu kumbe yule jamaa alikuwa TISS na akapotea kama jini.

TISS ya leo imejaa vijana wa UVCCM, wasiojua lolote kuhusu intelligence wala miiko yake. Idara hii imegeuzwa kuwa ya kisiasa ili CCM itimize ndoto zake za alinacha za kutawala milele. Inashangaza sana, yaani Idara haikuweza hata kuzuia maandamano ya kuharibu Diplomasia yetu na SA.

Watumishi wa Idara hii wanatakiwa wawe wafia nchi (wazalendo kweli kweli) siyo wafia CCM au CHADEMA.

CCM itakufa, CHADEMA itakufa, lakiniTanzania ipo tu!
 
Usichokijua ni bora tu kukaa kimya. Una uhakika gani kuwa hizi allegations zako TISS walikuwa hawazifahamu?

Una uhakika gani kuwa TISS hawakushauri lolote kabla ya haya kutokea?

Tanzania tuna bahati ya kuwa na taasisi imara. Hata wewe wakiamua kudeploy resources na kukufikia usiku huu wanakupata.

Usiku mwema!!
 
Ungeendelea na hiyo kazi yako ya kuchafua serikali na taasisi zake. Mkurugenzi wa TISS atakuwa mtu wa mwisho kabisa kupokea lawama na kuwajibika, in fact Dr. Kipilimba anafanya kazi kutokana na mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na uongozi wa awamu ya tano.
 
Dah umeandika uzi wa kutoka moyoni mwangu kabisa.

Sio siri TISS wanatuangusha sana watanzania nimewai kueleza huko nyuma kuwa TISS ipo kisiasa zaidi kuliko kiuchumi.

Kama Magufuli anataka kweli nchi ya viwanda wauangalie mfumo wote wa hiyo I Dara, ila kama anatamani yeye au CCM yake mpya kutawala milele waiache ilivyo, lla kwa maoni yangu TISS ifumuliwe na kuundwa upya.
 
Usichokijua ni bora tu kukaa kimya. Una uhakika gani kuwa hizi allegations zako TISS walikuwa hawazifahamu?

Una uhakika gani kuwa TISS hawakishauri lolote kabla ya haya kutokea?

Tanzania tuna bahati ya kuwa taasisi imara. Hata wewe wakiamua kudeploy resources na kukufikia usiku huu wanakupata.

Usiku mwema!!
Kama walishauri na watawala wenye vichwa ngumu wakapotezea hakuna haja ya kuwa na chombo hiki,usitetee utumbo hapa watu tuna hasira
 
Mkuu asante sana kwa hili, ila kwa sasa na vile tiss ya leo iko huwezi ilinganisha hata kidogo na mabigwa kaa CIA, M15, au the dreaded and most feared spy agency in the world, the israel MOSSAD.

Hapo miaka ya nyuma, TISS ilikuwa imara kabisa, hata huko Kenya tiss ilikuwa inaheshimiwa kabisa, lakini TISS ya leo imejaa wanafiki wa UVCCM, na wewe unajionea vile mambo inakwenda.

Hii TISS ya leo imekuwa kazi yake ni kuteka na kuua, haswa wapizani au watu ambao CCM haiwataki, kumbuka Zachariah kule Mara mkuu?

Hii tiss ya leo ni A BRANCH OF CCM PERIOD,
 
Kwani Serikali inalazimika kufuata ushauri wa TISS? lakini pia serikali haikujua kuwa kuna kesi SA, yaani tuseme mahaka ya huko SA haikutuma 'court notice'?

Hapa swala tu ni serikali imepuuzia kulipa deni, tumekuwa na vipaumbele vingi vikubwa kiasi kwamba tunashindwa hata kutimiza wajibu wetu barabara.
 
Umeongea kwa busara ya Hali ya juu ndugu na maneno yako yamebeba uzalendo sana..Mara nyingi sana ambao hawana maono ndio wanaongoza wenye maono na wenye maono wanabaki kudharauliwa.

Tuombe Mungu sana atuvushe kwenye hili maana tumetikiswa na tukatikisika kweli kweli..maana pigo ni moja lkn limeweza kutikisa kila idara na kutuacha uchii kbs
 
Usichokijua ni bora tu kukaa kimya. Una uhakika gani kuwa hizi allegations zako TISS walikuwa hawazifahamu?

Una uhakika gani kuwa TISS hawakishauri lolote kabla ya haya kutokea? Tanzania tuna bahati ya kuwa taasisi imara.

Hata wewe wakiamua kudeploy resources na kukufikia usiku huu wanakupata.

Usiku mwema!!

Nakuonea huruma, looh, endapo kama ungejua!!
Acha mimi niishie hapa, ili nisije nikasema na visivyotakiwa kusemwa.
 
kwani serikali inalazimika kufuata ushauri wa TISS? lakini pia serikali haikujua kuwa kuna kesi SA, yaani tusema mahaka ya huko SA haikutuma 'court notice'?
hapa swala tu ni serikali imepuuzia kulipa dena, tumekua na vipaombele vingi vikubwa kiasi kwamba tunashindwa hata kutimiza wajibu wetu barabara.
Na aliyependekeza idea ya kumpiga PI mkulima INA maana jiwe aliona wamemkomesha.nadhani walihisi kazi imeisha.maumivu aliyopata kwa sasa anachekelea huko aliko kwani mkuki kwa nguruwe mtamu sana ukigeuzwa kwako?
 
Ungeendelea na hiyo kazi yako yakuchafua serikali na taasisi zake,mkurugenzi wa TISS atakuwa mtu wa mwisho kabisa kupokea lawama na kuwajibika,in fact Dr.Kipilimbi anafanya kazi kutukana na mabadiliko makubwa ya kisiasa,kiuchumi na uongozi wa awamu ya tano.

Inamaana ungekuwa ni mpango wa kuilipua ndege kutoka kwa waharifu na idara ikajua/isijue na ndege ikalipuka je wakulaumiwa angekuwa ni Nani? Hapa idara haiwezi kukwepa lawama
 
Kwa kweli hali inayoendelea hapa nchini na duniani kote kwa ujumla kuhusiana na hii taasisi, Inasikitisha Sana kupita kiasi, tena inakatisha tamaa kwa kweli.

Wao badala ya kujikita zaidi na kuelekeza nguvu zaidi kwenye ECONOMIC ESPIONAGE wamebaki kuhangaika na ku-deal na vijitu vidogo vidogo vinavyokosoa Serikali, kutwa kucha wanashinda kwenye Facebook, twitter, JF, WhatsApp, n.k. kuangalia nani anaikosoa Serikali jambo ambalo hakuna tija yoyote kwa maslahi mapana ya umma.
 
Back
Top Bottom