Dkt. Kimei ashauri kuanzishwa kwa mfuko wa wajasiriamali

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
May 13, 2018
439
742
Mbunge wa jimbo la Vunjo Mhe Dkt. Charles Stephen Kimei akizungumza na Azam TV ameeleza umuhimu wa serikali kuanzisha mfuko maalum wa kuwawezesha wajasiriamali na wafanyabiashara wa kati kwa mikopo ya masharti nafuu, riba ndogo na ujuzi katika kuendesha na kusimamia biashara zao au kuziongezea thamani.

Anasema biashara ndogondogo na zile za kati zimeajiri idadi kubwa ya watu wanaojipatia kipato, wanachangia mapambano ya kuondoa umaskini na hata maendeleo ya nchi.

Amesema duniani leo asilimia karibu 80 ya ajira katika mataifa mbalimbali zinatokana na biashara hizi.

Amesisitiza kwa kasi hii ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amejipambanua kama mchumi kwa kutaka ustawi kwenye uwekezaji na biashara mfuko huu utamuandikia historia ya kipekee.

Kazi Iendelee.


IMG-20210621-WA0025.jpg
 
Afadhali huyu ametoa mawazo ya kukwamua vijana.

Mbona ni rahisi tu, watu mikataba yao ikiisha, au akiamua kuacha kazi...apewe Fully FAO LA KUJITOA, hasa sekta binafsi NSSF
 
Mbunge wa jimbo la Vunjo Mhe Dkt. Charles Stephen Kimei akizungumza na Azam TV ameeleza umuhimu wa serikali kuanzisha mfuko maalum wa kuwawezesha wajasiriamali na wafanyabiashara wa kati kwa mikopo ya masharti nafuu, riba ndogo na ujuzi katika kuendesha na kusimamia biashara zao au kuziongezea thamani.

Anasema biashara ndogondogo na zile za kati zimeajiri idadi kubwa ya watu wanaojipatia kipato, wanachangia mapambano ya kuondoa umaskini na hata maendeleo ya nchi.

Amesema duniani leo asilimia karibu 80 ya ajira katika mataifa mbalimbali zinatokana na biashara hizi.

Amesisitiza kwa kasi hii ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amejipambanua kama mchumi kwa kutaka ustawi kwenye uwekezaji na biashara mfuko huu utamuandikia historia ya kipekee.

Kazi Iendelee.


View attachment 1825194
Kwahiyo asili ya CRDB imesahaulika
 
Back
Top Bottom