SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Mbunge wa Jimbo la Vunjo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, CCM Mheshimiwa Dkt Charles Stephen Kimei amesema chanjo ni salama na chanjo ni kinga. Kukubali kuchanja ni kuonesha kujali afya na uhai wako pamoja na wengine.
Mimi pamoja na familia yangu tumekubali kuunga mkono mapambano dhidi ya ugonjwa huu hatari wa UVIKO-19 kwani zaidi ya kuathiri afya, kukatisha maisha ya wengi umeathiri sana uchumi wa mtu mmoja mmoja, Taifa na dunia kwa ujumla.
Naunga mkono na kupongeza uamuzi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuruhusu chanjo itolewe hapa nchini na kuwa hiyari kwa wananchi kuipata. Nawashauri wananchi wenzangu wa Vunjo kukubali kuchanja na kuzingatia hatua zingine za tahadhari zilizoshauriwa na wataalam wetu wa afya.
Mimi pamoja na familia yangu tumekubali kuunga mkono mapambano dhidi ya ugonjwa huu hatari wa UVIKO-19 kwani zaidi ya kuathiri afya, kukatisha maisha ya wengi umeathiri sana uchumi wa mtu mmoja mmoja, Taifa na dunia kwa ujumla.
Naunga mkono na kupongeza uamuzi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuruhusu chanjo itolewe hapa nchini na kuwa hiyari kwa wananchi kuipata. Nawashauri wananchi wenzangu wa Vunjo kukubali kuchanja na kuzingatia hatua zingine za tahadhari zilizoshauriwa na wataalam wetu wa afya.