Dkt. Kikwete: Watanzania wanatakiwa wazidi kuiombea Nchi pamoja na Rais Samia ili aweze kutafuta Majibu ya Vikwazo vinavyowakabili!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,897
141,833
imageresize.jpg

Rais Mstaafu Mzee Kikwete amewaomba Watanzania waendelee kuiombea Nchi iendelee kuwa tulivu na pia Rais Samia Suluhu Hassan aweze kutafuta Majibu ya Vikwazo vinavyowakabili.

========

RAIS mstaafu Dk. Jakaya Kikwete, amesema Watanzania wanatakiwa kuendelea kuiombea nchi iendelee kuwa tulivu na pia Rais Samia Suluhu Hassan aweze kutafutia majibu ya vikwazo vinavyowakabili wananchi.

Alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na waumini wa dini ya kiislamu, viongozi wa serikali, watoto yatima, wajane na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Pwani katika ifutari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge.

Kunenge, aliandaa futari hiyo Ikulu ndogo mjini Kibaha kwa niaba ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Kikwete, alimshukuru Rais Samia kwa kuwakumbuka watoto yatima na wajane kwa kuwapa futari hiyo kwakuwa jamii hiyo inapaswa kutunzwa na watu wote.

Alisema, kitendo cha kuandaa futari hiyo ni kumtukuza Mungu hasa kuwasaidia yatima ambao mahitaji yao yanategemea misaada ya wahisani mbalimbali.

Nipashe

Jumaa kareem.
 
Yeye kipindi cha utawala wake hakua anaombewa ama nchi haikua inaombewa? Kama ilikua inaombewa na anaombewa alishindwa nini kutafta suluhisho la matatizo yanayowakabili wanachi na nchi kwa ujumla.

Kama hakua anaombewa ama nchi haikua inaombewa, anataka kusingizia failure ya utawala wake kwenye maombi? Kwamba alikosa maombi?

Vikwazo ama matatizo hayawezi kuisha kwa maombi.

Wachina hana wala hawaombi hii miungu ya mashariki ya kati na wako mbali sana.
 
Mzee wangu Kikwete namheshimu sana na kumpenda, ila kasema
Watanzania waendelee au
Watanzania tuendelee... Mbona yeye kajitoa katika kauli hiyo..

Nilitegemea angesema watanzania tuendelee kuiombea nchi yetu na kumuombea Rais wetu Mama Samia, sbb Mh. JK ni mswahili, hapa kakosea kabisa.
 
JK mtu wa watu! Sio shabiki wa siasa zake lakini life style yake ni ya kinyamwezi sana. Hachukulii mambo serious sana ndio maana hazeeki.

Kipindi nchi imesimama, bunge linataka kuvunjika kisa Escrow akaita waandishi! wote tukajua mzee anapiga msumari wa moto!

Akawa anacheka zake na kuanza soga jinsi alivyoenda Marekani, alivyopokelewa na daktari, kipimo cha tezi dume na matibabu yake. Hadi jina la daktari wake tukatajiwa ( mzee kwa soga ni kiboko) Mwisho kwa jokes akagusia kwa mbaliii escrow , waandishi wakacheka!

Akatuzindua Watanzania ukubwa wa tatizo la tezi dume hadi kampeni ikaanzishwa! Dude la escrow likafia pale
 
Back
Top Bottom