Dkt. Kigwangalla: Mashine ya nyungu iliyo Muhimbili ivunjwe, viongozi wavae barakoa

Mbunge wa Nzega Mjini, Dkt. Hamis Kigwangalla ameshauri mashine ya kujifukizia iliyowekwa Hospitali ya Muhimbili ivunjwe na watu wafauate hatua za kujikinga na #COVID19 ikiwemo kupata chanjo.

Kigwangwalla amesema wataalamu wa Afya wanajukumu la kumshauri Rais Samia na yeye kama mbunge watalizungumza bungeni ili kuanza kufuata njia za kisayansi.

Amesema si sawa kwa taasisi kubwa kama muhimbili kuwa na mashine za kupiga nyungu, ni muhimu watu kufuata hatua a afya kama kuvaa barakoa nk.

===
Siku nikisukumiziwa kwenye uraisi hivi viumbe jamii ya kigwangala nitavianzishia mahakama ya unafiki na nitajenga ZOO (si jela) kubwa ya kuwaweka wakishahukumiwa maana unafiki wao ni kero kwa maendeleo ya binadamu😁😁😁😁😁
 
Mbunge wa Nzega Mjini, Dkt. Hamis Kigwangalla ameshauri mashine ya kujifukizia iliyowekwa Hospitali ya Muhimbili ivunjwe na watu wafauate hatua za kujikinga na #COVID19 ikiwemo kupata chanjo.

Kigwangwalla amesema wataalamu wa Afya wanajukumu la kumshauri Rais Samia na yeye kama mbunge watalizungumza bungeni ili kuanza kufuata njia za kisayansi.

Amesema si sawa kwa taasisi kubwa kama muhimbili kuwa na mashine za kupiga nyungu, ni muhimu watu kufuata hatua a afya kama kuvaa barakoa nk.

===
Anaongea kama mtaalamu au mwanasiasa? Kama ni utalaamu na yeye kama mwana taaluma husika kwanini hakuyasema siku zote?!
 
Hamis hanakosa alifahamu tangia mwanzoni kuwa Sayansi ndio kila kitu ila yeyote kati yetu angekua Hamiss kipindi cha magu tungesifia mitazamo yake
 
Ili lijamaaa si ndio lilikua la kwanza kupiga nyungu ili kumfurahisha mwenda zake et leo lememgeuka, ama kweli njaa mbaya.
 
Dah Magu amka uone waganga njaa hawa walivyo wanafiki. Huu unafiki wa kiwango cha juu sana sana.
Hivi Magu angekuwa hai ungethubutu hata kuacha mdomo wako wazi?

Hawa ndio viongozi wanaongoza watanzania.
Hivi mnajua hayo manyungu na unafiki wenu umeuza watu wangapi hadi sasa?
Magu alizungukwa na wanafki. na akawachekea sana.
wakimsifia kwa maneno matamu akawachagua.
haya ni matunda yake mwenyewe
 
Kazi ya wanasiasa ni unafiki huyu si ndo alikalishwa na waganga ambao hata STD 1 hawajafika ambae ni MD kabisa.

Swali Je Mecco angekuwa hai angemwambia aivunje na alete chanjo ?
 
Duhh..
Kifo mwanaharamu aisee...
Magu huko uliko unaona!??
Pole sana ..hata siku 21 hazijaisha..
Mbunge wa Nzega Mjini, Dkt. Hamis Kigwangalla ameshauri mashine ya kujifukizia iliyowekwa Hospitali ya Muhimbili ivunjwe na watu wafauate hatua za kujikinga na #COVID19 ikiwemo kupata chanjo.

Kigwangwalla amesema wataalamu wa Afya wanajukumu la kumshauri Rais Samia na yeye kama mbunge watalizungumza bungeni ili kuanza kufuata njia za kisayansi.

Amesema si sawa kwa taasisi kubwa kama muhimbili kuwa na mashine za kupiga nyungu, ni muhimu watu kufuata hatua a afya kama kuvaa barakoa nk.

===
 
Msimshambulie Hamis. Alichofanya ni kujitoa muhanga tu na "kumfunga panya kengele" maana members wengi kwenye cabinet wana mawazo kama yake ilia hawana guts za kutoka na kusema. Hamis kwa kuwa sasa sio Waziri, he dont have much to lose, atleast for now
 
Back
Top Bottom