CHEF
JF-Expert Member
- Nov 4, 2013
- 222
- 122
Hapo chini nimewaorodhesha wabunge na mkoa wa Tabora, wabunge wa kuchaguliwa na wabunge wa viti maalum, awali wabunge tegemezi wa mkoa wa Tabora walikuwa ni Dkt Hamis Andrea Kigwangala na Hussein Mohammed Bashe, Uhodari wao wa kusemea wananchi na kujitolea kidogo wanachokipata kugawana na wananchi kuliwafanya kuonekana viongozi imara na shupavu kwa maendeleo ya Tabora na Tanzania kwa ujumla, lakini kwa sasa amebaki Hussein Bashe tu ambaye anaonekana kuwa kiongozi mwenye maono na Maendeleo ya Tabora, Kingwangala naweza kusema amelisahau jimbo kwa sasa.
Dkt Kigwangala nakuita amka kaka, anza mchaka mchaka, oga maji ya baridi halafu uanze nguvu mpya kuiinua Tabora kulingana na dunia inavyotaka, Wabunge wafuatao wanahitaji kuamshwa na kupewa amsha amsha ili wafanye kazi kwa ajili ya wananchi kwani wamelala sana na hakuna wakuwapa changamoto, hawana mawazo mbadala ya kuleta maendeleo tofauti na mipango ya serikali kuu,
1. Mh. Margaret Simwanza Sitta mbunge wa jimbo la Urambo Mashariki
2. Mhe. Emmanuel Adamson Mwakasaka Mbunge wa Jimbo la Tabora mjini
3. Mhe. Munde Abdallah Tambwe mbunge wa viti maalum mkoa wa Tabora
4. Mhe. Joseph George Kakunda Mbunge wa Jimbo la Sikonge
5.Mhe. Selemani Jumanne Zeddy mbunge wa jimbo la Bukene
6. Mhe. Mussa Rashid Ntimizi mbunge wa jimbo la Igalula
7. John Peter Kadutu mbunge wa jimbo la Ulyankulu
8. Mhe. Seif Khamis Said Gulamali mbunge wa jimbo la Manonga
9. Mhe. Almas Athuman Maige Jimbo la Tabora Kaskazini
10 Mhe. Dkt Dalali Peter Kafumu Mbunge wa jimbo la Igunga
11. Mwanne Ismail Mchemba Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tabora
12. Mhe. Magdalena Hamis Sakaya mbunge wa jimbo la Kaliua
Ndugu wabunge niwakumbushe tu sisi warugaruga tunataka kwenda na kasi ya maendeleo ya Dkt John Pombe Magufuli, sisi warugaruga tunataka kwenda na maendeleo kutokana na dunia inavyotaka, hatujawachagua ili mpumzike, tumewachagua ili muwe chachu ya maendeleo, mpambane kutuonesha njia ya kuitambaua dunia inataka nini na tufanye nini, tunataka Tabora ya leo inayoendana na sayansi na teknolojia. Tusome kwa teknolojia, tulime kwa teknolojia, tufanye biashara kwa teknolojia, tutibiwe kwa teknolojia na tule kwa teknolojia.
Ujumbe uwafikie ndugu wabunge na viongozi wote kwa ujumla
Dkt Kigwangala nakuita amka kaka, anza mchaka mchaka, oga maji ya baridi halafu uanze nguvu mpya kuiinua Tabora kulingana na dunia inavyotaka, Wabunge wafuatao wanahitaji kuamshwa na kupewa amsha amsha ili wafanye kazi kwa ajili ya wananchi kwani wamelala sana na hakuna wakuwapa changamoto, hawana mawazo mbadala ya kuleta maendeleo tofauti na mipango ya serikali kuu,
1. Mh. Margaret Simwanza Sitta mbunge wa jimbo la Urambo Mashariki
2. Mhe. Emmanuel Adamson Mwakasaka Mbunge wa Jimbo la Tabora mjini
3. Mhe. Munde Abdallah Tambwe mbunge wa viti maalum mkoa wa Tabora
4. Mhe. Joseph George Kakunda Mbunge wa Jimbo la Sikonge
5.Mhe. Selemani Jumanne Zeddy mbunge wa jimbo la Bukene
6. Mhe. Mussa Rashid Ntimizi mbunge wa jimbo la Igalula
7. John Peter Kadutu mbunge wa jimbo la Ulyankulu
8. Mhe. Seif Khamis Said Gulamali mbunge wa jimbo la Manonga
9. Mhe. Almas Athuman Maige Jimbo la Tabora Kaskazini
10 Mhe. Dkt Dalali Peter Kafumu Mbunge wa jimbo la Igunga
11. Mwanne Ismail Mchemba Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tabora
12. Mhe. Magdalena Hamis Sakaya mbunge wa jimbo la Kaliua
Ndugu wabunge niwakumbushe tu sisi warugaruga tunataka kwenda na kasi ya maendeleo ya Dkt John Pombe Magufuli, sisi warugaruga tunataka kwenda na maendeleo kutokana na dunia inavyotaka, hatujawachagua ili mpumzike, tumewachagua ili muwe chachu ya maendeleo, mpambane kutuonesha njia ya kuitambaua dunia inataka nini na tufanye nini, tunataka Tabora ya leo inayoendana na sayansi na teknolojia. Tusome kwa teknolojia, tulime kwa teknolojia, tufanye biashara kwa teknolojia, tutibiwe kwa teknolojia na tule kwa teknolojia.
Ujumbe uwafikie ndugu wabunge na viongozi wote kwa ujumla