Dkt. John Magufuli amekufa na deni letu, Rais Samia tunaomba suluhu yako

msovero

JF-Expert Member
Jun 30, 2019
839
1,472
Mama naomba niandike kifupi ili nisikuchoshe kusoma maana najua una majukumu mengi na mazito ya kuwatumikia Watanzania.

Mama, wakati hayati magufuli hajakumbwa na mauti alituahidi ajira 13529 za ualimu. Kati ya hizo ni ajira 8000 tu zimetolewa katika awamu ya kwanza nazo zilitolewa angali bado yu hai.

Leo hii hatuko naye lakini bado kuna kiporo cha ajira zaidi ya elfu 5000 zilizosalia bado hazijatoka na hatma haieleweki kama nazo zimekufa au laah!

Najua wewe ni mama mwenye huruma na upendo, hivyo naomba kukufikishia kilio hiki ukipatie suluhu maana miezi inaenda na matumaini yanazidi kupungua.

Mwisho, tuna imani na wewe mama tunaamini hautatuangusha. Kadhalika tunakutakia kila la heri katika majukumu yako mapya.
 
Pole sana kijana, ila nadhani umemsikia VP akilihutubia bunge.

...ni kuwa wanaendeleza na kuboresha yale aliyoishia njiani mwendazake, swali la kujiuliza, suala la ajira lipo?!
 
Waziri mkuu alishatangaza kuwa hizo 5,000 tayari toka mwezi wa pili kama siyo wa kwanza! Wewe hukupata?
Hazijawahi kutoka au pengine wakati waziri mkuu anatoa kauli hiyo hakuwa ametaarifa vyema na wizara ya tamisemi hivyo akapotosha umma
 
Mama naomba niandike kifupi ili nisikuchoshe kusoma maana najua una majukumu mengi na mazito ya kuwatumikia Watanzania.

Mama, wakati hayati magufuli hajakumbwa na mauti alituahidi ajira 13529 za ualimu. Kati ya hizo ni ajira 8000 tu zimetolewa katika awamu ya kwanza nazo zilitolewa angali bado yu hai.

Leo hii hatuko naye lakini bado kuna kiporo cha ajira zaidi ya elfu 5000 zilizosalia bado hazijatoka na hatma haieleweki kama nazo zimekufa au laah!

Najua wewe ni mama mwenye huruma na upendo, hivyo naomba kukufikishia kilio hiki ukipatie suluhu maana miezi inaenda na matumaini yanazidi kupungua.

Mwisho, tuna imani na wewe mama tunaamini hautatuangusha. Kadhalika tunakutakia kila la heri katika majukumu yako mapya.
Lakini shida ya vijana siku hizi wengi wanataka kupangiwa mijini wakati shule za vijijini hazina waalimu
 
Mama naomba niandike kifupi ili nisikuchoshe kusoma maana najua una majukumu mengi na mazito ya kuwatumikia Watanzania.

Mama, wakati hayati magufuli hajakumbwa na mauti alituahidi ajira 13529 za ualimu. Kati ya hizo ni ajira 8000 tu zimetolewa katika awamu ya kwanza nazo zilitolewa angali bado yu hai.

Leo hii hatuko naye lakini bado kuna kiporo cha ajira zaidi ya elfu 5000 zilizosalia bado hazijatoka na hatma haieleweki kama nazo zimekufa au laah!

Najua wewe ni mama mwenye huruma na upendo, hivyo naomba kukufikishia kilio hiki ukipatie suluhu maana miezi inaenda na matumaini yanazidi kupungua.

Mwisho, tuna imani na wewe mama tunaamini hautatuangusha. Kadhalika tunakutakia kila la heri katika majukumu yako mapya.
Da! so sad, kwahiyo ajira ni huruma ya mtawala na siyo hitaji la msingi la nchi? basi tuna katiba ya kijinga kabisa
 
Ndio kusema zimechinjiwa baharini?
 
Lakini shida ya vijana siku hizi wengi wanataka kupangiwa mijini wakati shule za vijijini hazina waalimu
Mkuu ungeanza kutafuta taarifa ujiridhishe kwanza kama hiki ulichokiandika kina ukweli bila hivyo haya maneno yako ni porojo tu ambazo hazina mantiki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom