Dkt. James Alex Msekela ateuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia

Katika taarifa yake, Katibu Mkuu Kiongozi Sefue amesema kuwa Rais Kikwete amemteua Dkt. James Alex Msekela kuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia.

Kabla ya hapo Mheshimiwa Msekela alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Aidha, taarifa hiyo ya Bwana Sefue imesema kuwa Rais Kikwete amemteua Bwana Ramadhani Muombwa Mwinyi kuwa Naibu Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York.

Kabla ya hapo, Bwana Mwinyi alikuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Katibu Mkuu kiongozi amesema katika taarifa yake kuwa wateuliwa hao wawili wataapishwa keshokutwa, Alhamisi, Januari 5, 2012.

Imetolewa na
:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM
.
Hivi inakuaje kuna mahari nimeona uteuzi huu unaanza October 2011? anaapisha tarehe 5 January , 2011? au ni sehumu tu ya kumuongezea marupurupu baada ya kuakaaa kijiweni kwa miezi mitatu?
 
Sidhani kama kutochaguliwa kwenye ubunge ni disqualification kwa kazi nyingine za kuteuliwa. Tufahamu kuwa siasa za uchaguzi hazizingatii sifa na ubora wa wagombea. Mf. wako wabunge waliochaguliwa kwa vigezo vya kugawa ela,kanga,pombe,ukabila, udini n.k Tuwe makini tunapopinga uteuzi kwa kigezo kuwa mteuliwa alikataliwa na wananchi.
 
Alisahaulika siku ile akina Buriani, Kamala,... wanatajwa? Vipi maDC watateuliwa lini?
 
mawe wanayo yakataa waashi ndio yanawekwa kuwa mawe ya kwenye pembe, KAZI KWELIKWELI
 
Kuna kitu huwa kinanipa shida kuelewa toka uteuzi wa mabalozi au makatibu wote wanakuwa ni wanachama wa ccm mbaya zaidi wengi wao ni wale walishindwa na kuonekani ni dhaifu na wanaccm wenyewe kwenye michakato ya uchaguzi lakini baada ya muda rais anawateua kuwa mabarozi. Barozi anawakilisha nchi nzima na mbunge anawakilisha jimbo, rais anapomteua mtu ambaye wananchi waliona hafai kuwa mbunge lakini rais anaona anafaa kuwa barozi ni udhaifu mkubwa.
SISI-EM ina wenyewe, na wenyewe ndo hao. Hata kama wananchi watakukataa lakini ukawa ni mmoja wao ambao ndo WENYEWE( WENYE SISI-EM) mkulu atakuweka katka orodha ya WATAWALA. Maana wao wameamua kutawala na sio kuongoza.
 
Wana JF sijawahi kumpongeza Rais Jakaya Mrisho Kikwete, lakini kwa uteuzi ninampongeza kwani amezingatia sifa na uwezo. Dr. James Nsekela ni mtu wa watu hana makuu. Kushindwa kwake kwenye kura za maoni ni kwa sababu alikuwa anashindana na Mhindi ambaye alionga ela nyingi na hivyo kuwa mgombea kwa tiketi ya CCM.
 
Wana JF sijawahi kumpongeza Rais Jakaya Mrisho Kikwete, lakini kwa uteuzi ninampongeza kwani amezingatia sifa na uwezo. Dr. James Nsekela ni mtu wa watu hana makuu. Kushindwa kwake kwenye kura za maoni ni kwa sababu alikuwa anashindana na Mhindi ambaye alionga ela nyingi na hivyo kuwa mgombea kwa tiketi ya CCM.
Kuwa mtu wa watu unamaanisha kuwa ana ujuzi na uzoefu wa mambo ya kimataifa? mbona tunao watu wengi wenye sifa hizo, wenye uzoefu wa kutoshakatika sector hiyo. Na je kuna ulazima gani kuwa nafasi zote anazoteua raisi ziend CCM?

Mie si mwanachama wa chama chochote, mie ni mtanzania, lakini nahisi Raisi alitakiwa kuteua watu(watanzania) wenye elimu ya diplomasia, na uzoefu katika kazi hiyo regardless ya itikadi, kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu changa (50 years of age), na si kuangalia kuwa huyu ni mtu wa watu au ni m-CC
 
kipya kinyrmi ukimwacha wenzio wanasema tutampata lini
big up kamanda alex kabadilishe hewa bana
 
Hivi inakuaje kuna mahari nimeona uteuzi huu unaanza October 2011? anaapisha tarehe 5 January , 2011? au ni sehumu tu ya kumuongezea marupurupu baada ya kuakaaa kijiweni kwa miezi mitatu?
Nimewahi kuambiwa kwamba, ubalozi hautolewi kama zawadi kama bwana mkubwa anavyofanya. Nimeambiwa kwamba kiutaratibu, mtu anatakiwa awe amefanya Wizara ya Mambo ya Nje na awe anapanda vyeo vya u-diplomasia Grade III, II, I, n.k. Sasa huyu jamaa anateua vyovyote! Tusaidieni wataalamu. Au hata mimi ninaweza kuwa balozi siku moja?
 
Naona ni wale wale tu............ WALIOANDIKIWA!!!

VICIOUS CIRCLE

Inaelekea Mkweree bado waziri wa mambo ya nje; maana huyu wa sasa alituambia kuwa tokea sasa mabalozi watakuwa VIJANA lakini inaelekea mkuu wake na yeye sera zao haziendani sawa sawa!! Angekuwa na akili Membe angejiuzuru kwa kudharauliwa kwani wote wanaoteuliwa ubalozini ni vijeba tena waliokataliwa na wananchi!!
 
Mpiga Box kule Sweden miaka ya 90', naona mambo yanaendelea kumnyookea! Hongera kaka Alex (DR. wa ukweli)
 
Sidhani kama kutochaguliwa kwenye ubunge ni disqualification kwa kazi nyingine za kuteuliwa. Tufahamu kuwa siasa za uchaguzi hazizingatii sifa na ubora wa wagombea. Mf. wako wabunge waliochaguliwa kwa vigezo vya kugawa ela,kanga,pombe,ukabila, udini n.k Tuwe makini tunapopinga uteuzi kwa kigezo kuwa mteuliwa alikataliwa na wananchi.

Mkuu hapa umesema kweli tena kweli tupu. Tena hao wengi walishindwa kwenye kura za maoni ambazo ziligubikwa na rushwa ya kila aina. Huenda ambao hawakuchaguliwa ni wasafi; hawakutoa mlungula wakati wa zoezi lile. Hivyo kama ilivyosema kutochaguliwa si kigezo pekee. Mchakato wa uchaguzi wa wabunge Tanzania hautuhakikishii kupata watu walio bora.
 
Wananchi including JF members wanalalamika JK kuteua watu waliokataliwa na wapiga kura, lakini wanasahau kuwa hata JK mwenyewe alikataliwa na wapiga kura na Tume ya Uchaguzi ikamuingiza ikulu kwa nguvu. Hivyo kwa yeye kuendelea na hillo zoezi la kuwaweka watu waliokataliwa kwenye nafasi mbalimbali ni BIG DEAL kwake binafsi na familia yake. Ndiyo hao watamtafutia njia ya kuchomoka baada ya kuondoka madarakani.....watch.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom