Zanzibar 2020 Dkt. Hussein Mwinyi akijibu maswali ya moja kwa moja kutoka kwa wananchi - Oktoba 23, 2020

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,190
4,103
Dkt. Hussein Mwinyi yupo LIVE anajibu maswali ya moja kwa moja kutoka kwa wananchi.

Barabara na uchumi mkubwa
Amesema Swala la barabara Unguja na Pemba ni swala muhimu na pia wanapozungumzia uchumi mpya ina maana watahitaji umeme mwingi zaidi na wanatafuta njia ya kuweza kuwa na uchumi mkubwa zaidi na kwa kuwa na umeme mkubwa na wa uhakika .

Utalii

Amesema bado wana fursa kubwa ya kuongeza utalii mwingine kama utalii wa historua katika maeneo ya kale, utalii wa fukwe za baharini na kuhakikisha utalii unakuwa wa aina yake yaani unakuwa utalii wenye tija kubwa.

Ajira
Amesema watazalisha ajira laki tatu kutoka kwenye uchumi mpya wanaotaka kuujenga kutoka kwenye uvuvi, barabara, viwanda, mafuta na gesi hivyo ni imani yake ajira zitapatikana na huduma za jamii zitaboreshwa kama umeme na maji na huko kote ajira zitazalishwa.

Diaspora
Amesema ili uchumi uweze kukua ni lazima sekta binafsi zishiriki hivyo hata hao watanzania wanaoishi nnje watashirikiana nao a yeye anaahidi iwapo atakuwa Rais wa awamu ya nane basi atawatumia hao maana ni sekta muhimu.

Ardhi ya kilimo
Amesema Zanzibar hawana ardhi kubwa ya kilimo lakini wana zao lenye thamani kubwa zao la karafuu na wana mazao ya viungo ambayo yanasoko kubwa hivyo watayatumia hayo kukuza uchumi na pia amedI muda umefika wa kujenga viwanda ili kuliongezea thamani zao hilo kuliko kuliuza likiwa zao ghafi.

Swala la maendeleo ya kisiwa cha Pemba
Amesema lengo ni kuhakikisha na Pemba inapiga hatua na serikali ya awamu ya nane wataweka juhudi za makusudi ili na Pemba ipige hatua za maendeleo kama Unguja.

Ajira kwa vijana
Amesema kuhusu swala la kuwakomboa vijana na ukosefu wa ajira amedai kuwa ataborsha mfuko kwa ajiri ya kuwawezesha vijana kujiajiri na atatoa mafunzo kwa vijana ili wawweze kukidhi vigezo vya kuweza kuajiriwa.

 
Anapiga Kelele tu. Zanzibar haiwezi endelea ndani ya Muungano, muarubani wa maendeleo ya Zanzibar ni kuvunja Muungano.
 
Bia yetu

Kama kudai nchi yetu ni uhizbu, basi mahizbu ni wengi sanaa na twachukuwa safari hii.
Oman mtakwenda nyie kuchuna uso muombe msaada.
 
Bia yetu

Kama kudai nchi yetu ni uhizbu, basi mahizbu ni wengi sanaa na twachukuwa safari hii.
Oman mtakwenda nyie kuchuna uso muombe msaada.
Natuone

(Zanzibar ni sehemu ya Tanzania na itabaki hivyo)

(Watu weusi waliopo Zanzibar wengi asili yao ni Tanzania bara, na wachache waliobaki maeneo mengine ya Africa bara)
 
Hivi Unguja ina maendeleo? kwa hiyo pemba bado ndio kwanza wanaitafuta Unguja kimaendeleo(sijui maendeleo yapi). Kama ni hivyo hawa wa pemba wanahaki ya kudai haki. Yale yakuwa kama Dubai sasa hakuna tena. Ukweli Zanzibar CCM wameiuwa kwa makusudi kabisa wala sio bahati mbaya miaka ya 90 kulikuwa na biashara sana kama kawaida CCM haraka wakaingia kuuwa uchumi kulikuwa na mzunguko sana wa pesa biashara zilikuwa zinafanyika sana wakaona tuweke kodi ukija Bongo kodi tena tuwasumbue watu wasiende kununua Zanzibar ndio biashara zikapotea.
 
Mbona hawamuulizi kuwa yeye ni mamluki kutoka Mkuranga- Tanganyika?
 
Dkt. Hussein Mwinyi yupo LIVE anajibu maswali ya moja kwa moja kutoka kwa wananchi.

Barabara na uchumi mkubwa
Amesema Swala la barabara Unguja na Pemba ni swala muhimu na pia wanapozungumzia uchumi mpya ina maana watahitaji umeme mwingi zaidi na wanatafuta njia ya kuweza kuwa na uchumi mkubwa zaidi na kwa kuwa na umeme mkubwa na wa uhakika .

Utalii

Amesema bado wana fursa kubwa ya kuongeza utalii mwingine kama utalii wa historua katika maeneo ya kale, utalii wa fukwe za baharini na kuhakikisha utalii unakuwa wa aina yake yaani unakuwa utalii wenye tija kubwa.

Ajira
Amesema watazalisha ajira laki tatu kutoka kwenye uchumi mpya wanaotaka kuujenga kutoka kwenye uvuvi, barabara, viwanda, mafuta na gesi hivyo ni imani yake ajira zitapatikana na huduma za jamii zitaboreshwa kama umeme na maji na huko kote ajira zitazalishwa.

Diaspora
Amesema ili uchumi uweze kukua ni lazima sekta binafsi zishiriki hivyo hata hao watanzania wanaoishi nnje watashirikiana nao a yeye anaahidi iwapo atakuwa Rais wa awamu ya nane basi atawatumia hao maana ni sekta muhimu.

Ardhi ya kilimo
Amesema Zanzibar hawana ardhi kubwa ya kilimo lakini wana zao lenye thamani kubwa zao la karafuu na wana mazao ya viungo ambayo yanasoko kubwa hivyo watayatumia hayo kukuza uchumi na pia amedI muda umefika wa kujenga viwanda ili kuliongezea thamani zao hilo kuliko kuliuza likiwa zao ghafi.

Swala la maendeleo ya kisiwa cha Pemba
Amesema lengo ni kuhakikisha na Pemba inapiga hatua na serikali ya awamu ya nane wataweka juhudi za makusudi ili na Pemba ipige hatua za maendeleo kama Unguja.

Ajira kwa vijana
Amesema kuhusu swala la kuwakomboa vijana na ukosefu wa ajira amedai kuwa ataborsha mfuko kwa ajiri ya kuwawezesha vijana kujiajiri na atatoa mafunzo kwa vijana ili wawweze kukidhi vigezo vya kuweza kuajiriwa.


Nimdokeze tuu, utalii kama ulivyo sasa (idadi) unatoa pato la kutosha. Kilichopo ni udhibiti wa mapato ya utalii kuwa mbovu. Ukiuliza serekali imefanyaje kudhibiti pato la utalii utaona madudu tuu. Sidhani kama SMZ ina uwezo hata wa kufanya makadirio ya wageni wanaongia nchini wanakaa wapi ? Na wanalipia kiasi gani katika hoteli, ili kujua kodi kiasi gani inatarajiwa n.k.

Hapo kwenye utalii, Zanzibar kujitangaza katika nyanja ya kimataifa kuna pia ukakasi wa muungano. Ukienda pale Berlin kwa mfano, utaona bila ya tochi. Zanzibar itasukumwa kama sehemu ya Tanganyika basi vurugu mechi tuu.

Sidhani kama waandishi wetu mnafanya kazi zetu vizuri. Yaani masuala ya Zanzibar kwa sasa yapo zaidi katika mamlaka kuliko mjadala wa kuongeza ajira!
 
Tunawasihi watanzania kufuata sheria, kutofanya fujo wala kuharibu mali. Tuwe watulivu muda wote huku tukisimamia haki zetu. Tupige na kulinda kura zetu bila hofu wala woga wowote hii ni Haki zetu kisheria. Ukipiga kura kaa umbali wa mita 200 kutoka kituo cha kura. TUTASHINDA!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom