"Wasemaji ninaowaongoza, wazingatie kuna maadili ya kuwa Msemaji kama vile taaluma ya habari ambayo inatuongoza, tumeshatoa mafunzo kwa Wasemaji wa Vilabu vya Mpira, tumeona kuna changamoto kweli wakati mwingine badala ya kuhamasiha Watu kwenda viwanjani unakuta Msemaji anahamasisha vurugu, Msemaji anasema Watu fulani wasije uwanjani ukija tutakutoa”- Dk. Hassan Abbas, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali
“Wasemaji wafahamu usemaji sio kuropoka, usemaji una maadili yake kwahiyo tumeshatoa mafunzo kwa Wasemaji wa Vilabu vyote vya michezo mbalimbali, huku tunakokwenda tunataka kuona mabadiliko kwahiyo ni muhimu kwa Viongozi na Vyama vya Michezo kuhakikisha Wasemaji wao sio waropokaji isipokuwa ni Watu wanatimiza wajibu wa kitaaluma na kikatiba lakini sio porojo na uropokaji"-Dr.Abbas
“Wasemaji wafahamu usemaji sio kuropoka, usemaji una maadili yake kwahiyo tumeshatoa mafunzo kwa Wasemaji wa Vilabu vyote vya michezo mbalimbali, huku tunakokwenda tunataka kuona mabadiliko kwahiyo ni muhimu kwa Viongozi na Vyama vya Michezo kuhakikisha Wasemaji wao sio waropokaji isipokuwa ni Watu wanatimiza wajibu wa kitaaluma na kikatiba lakini sio porojo na uropokaji"-Dr.Abbas