Francis12
JF-Expert Member
- Sep 30, 2016
- 7,533
- 22,276
-Anaandika Dr.Chriss Cyrilo (MD)
____________________
Mwongozo wa wizara ya Afya nchini Tanzania unasema hadi sasa hakuna dawa ya kutibu ugonjwa wa covid19. Wakati huohuo tunaarifiwa kuwa serikali imepokea shehena ya dawa ya kukinga na kutibu covid19 kutoka Madagascar. Je serikali kupitia wizara ya afya itabadili muongozo wake, iseme kuna dawa ya kutibu covid19 kutoka Madagascar?
Ijulikane kwamba kwa mujibu wa mwongozo wa WHO na tafiti zilizofanyika hadi sasa, asilimia 80 ya wagonjwa wa Covid19 hupona wenyewe bila kuhitaji matibabu. Asilimia 20 hulazimika kupatiwa matibabu (kutokana na kuwa na magonjwa mengine). Na miongoni mwao asilimia 2 hadi 5 hufariki dunia.
Kwa lugha rahisi ni kuwa, kati ya watu 100 wanaoambukizwa virusi vya Corona, watu 80 hupona wenyewe bila kupata matibabu yoyote. Na pengine bila kuhisi dalili zozote kwamba wana maambukizi. Watu 20 waliobaki hupata dalili na huhitaji matibabu. Miongoni mwa hao 20, watu wawili hadi watano hufariki dunia.
Inawezekana wewe msomaji wa andiko hili ukawa na maambukizi ya virusi vya corona na usiwe na dalili zozote na ukapona bila kutumia dawa yoyote. Ikitolea hivyo means upo kwenye lile kundi la asilimia 80.
Tunaposisitiza umuhimu wa tafiti, ni kuepuka kusema dawa imetibu watu ambao pengine wangepona wenyewe hata bila kuhitaji dawa. Je! Dawa kutoka Madagascar inatibu wale asilimia 2-5 wanaofariki? Au inatibu wale 15% ambao hupona kwa kutibiwa magonjwa nyemelezi? Au inatibu wale 80% ambao hupona wenyewe bila kuhitaji dawa yoyote. Hakuna jibu kwa sababu hakuna utafiti uliofanyika.
Madagascar wanaendelea na tafiti, WHO wanafanya utafiti na taasisi nyingine kubwa za afya duniani zinaendelea na utafiti kuhusu dawa hiyo. Kwahiyo sisi kusema dawa hii inakinga na kutibu corona maana yake ni kwamba tupo mbele ya majira kuliko WHO na taasisi nyingine za utafiti. Infact WHO wenyewe hawaiiti dawa bali kinywaji cha mitishamba (herbal drink).
_
Kwahiyo na sisi tunaweza kuisaidia Madagascar katika utafiti wa dawa hii kupitia taasisi zetu za utafiti wa tiba kama vile NIMR, kabla ya kusema hadharani kuwa dawa hii inatibu au kukinga.!
____________________
Mwongozo wa wizara ya Afya nchini Tanzania unasema hadi sasa hakuna dawa ya kutibu ugonjwa wa covid19. Wakati huohuo tunaarifiwa kuwa serikali imepokea shehena ya dawa ya kukinga na kutibu covid19 kutoka Madagascar. Je serikali kupitia wizara ya afya itabadili muongozo wake, iseme kuna dawa ya kutibu covid19 kutoka Madagascar?
Ijulikane kwamba kwa mujibu wa mwongozo wa WHO na tafiti zilizofanyika hadi sasa, asilimia 80 ya wagonjwa wa Covid19 hupona wenyewe bila kuhitaji matibabu. Asilimia 20 hulazimika kupatiwa matibabu (kutokana na kuwa na magonjwa mengine). Na miongoni mwao asilimia 2 hadi 5 hufariki dunia.
Kwa lugha rahisi ni kuwa, kati ya watu 100 wanaoambukizwa virusi vya Corona, watu 80 hupona wenyewe bila kupata matibabu yoyote. Na pengine bila kuhisi dalili zozote kwamba wana maambukizi. Watu 20 waliobaki hupata dalili na huhitaji matibabu. Miongoni mwa hao 20, watu wawili hadi watano hufariki dunia.
Inawezekana wewe msomaji wa andiko hili ukawa na maambukizi ya virusi vya corona na usiwe na dalili zozote na ukapona bila kutumia dawa yoyote. Ikitolea hivyo means upo kwenye lile kundi la asilimia 80.
Tunaposisitiza umuhimu wa tafiti, ni kuepuka kusema dawa imetibu watu ambao pengine wangepona wenyewe hata bila kuhitaji dawa. Je! Dawa kutoka Madagascar inatibu wale asilimia 2-5 wanaofariki? Au inatibu wale 15% ambao hupona kwa kutibiwa magonjwa nyemelezi? Au inatibu wale 80% ambao hupona wenyewe bila kuhitaji dawa yoyote. Hakuna jibu kwa sababu hakuna utafiti uliofanyika.
Madagascar wanaendelea na tafiti, WHO wanafanya utafiti na taasisi nyingine kubwa za afya duniani zinaendelea na utafiti kuhusu dawa hiyo. Kwahiyo sisi kusema dawa hii inakinga na kutibu corona maana yake ni kwamba tupo mbele ya majira kuliko WHO na taasisi nyingine za utafiti. Infact WHO wenyewe hawaiiti dawa bali kinywaji cha mitishamba (herbal drink).
_
Kwahiyo na sisi tunaweza kuisaidia Madagascar katika utafiti wa dawa hii kupitia taasisi zetu za utafiti wa tiba kama vile NIMR, kabla ya kusema hadharani kuwa dawa hii inatibu au kukinga.!