Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,813
- 4,545
Dkt. Cassian Nyandindi, Kamishna Msaidizi wa Tiba na Huduma za Utengamao akiwa kwenye mahojiano East Afrika Radio amegusia mambo mengi kuhusu madawa ya kulevya.
Akifafanua kuhusu kukithiri kwa matumizi ya bangi katika baadhi ya mikoa nchini Tanzania amesema
"Kutokana na ukamataji na jinsi ambavyo mamlaka inafanya kazi tatizo la bangi lipo maeneo mengi nchini lakini Arusha kuna tatizo kubwa zaidi na Mara pia kuna tatizo kubwa" .
"Vijana wanaingia kwenye dawa za kulevya kutokana na kukosa elimu sahihi, na wengi huwa wanaenda kwa kujaribu kwa mfano vijana wadogo anaona mwenzake anatumia anajikuta na yeye anajaribu".
"Bangi ni dawa ya kulevya na kwa kawaida tunaongozwa na sheria ya nchi na sheria yetu ya Tanzania ambayo imepelekea kuundwa kwa mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya inatambua kuwa bangi ni dawa za kulevya kwa yoyote atakayejihusisha ni kosa".
"Bangi inachangia sana kwenye kuleta matatizo ya akili, kuna shirika la umoja wa mataifa ambalo linajihusisha na madawa ya kulevya na uhalifu, taarifa yao inaonesha kwamba bangi ndio dawa iliyochangia kuleta matatizo ya akili zaidi duniani kwa mwaka 2021".