Dkt Bashiru Katibu Mkuu CCM awasili Kisisani Pemba

Egnecious

JF-Expert Member
Jul 8, 2015
875
960
TAARIFA

Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally, asubuhi ya leo tarehe 02 Desemba, 2019 amewasili kisiwani Pemba kwa ziara ya siku tatu akitokea Kisiwani Unguja alipohitimisha ziara yake jioni jana tarehe 01 Desemba, 2019.

Ziara hiyo inalenga kuimarisha Uhai wa Chama, kukagua miradi na kuimarisha mahusiano baina ya Chama na Serikali na kuendelea kukifanya Chama kuwa karibu zaidi na wananchi.

Imetolewa na;
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM).

IMG_20191202_100251_597.jpeg
IMG_20191202_100251_596.jpeg
 
Ila katibu mkuu wa CHADEMA akija huku LINGUSENGUSE nilipo mimi,ni amri tu inatolewa ya kutiwa ndani,kisa anatishia usalama wa nchi!!!muda ni ukuta yana mwisho na kuna siku upepo utavuma kutokea upande mwingine na nchi itavuta hewa safi ya kuwa huru kupigia kura chama unachokiamini,kuwa na freedom of speech,press freedom etc etc,muda huu magazeti yote yanaunga mkono juhudi moja,I feel sorry kwa gazeti la Mwananchi(nilikuwa mpenzi wao mkubwa)but now nalo limegeuka na mbaya zaidi limemtelekeza mwandishi wao aliyepotea katika mazingira ya utatanishi,shame on them ,angalia TV ya Aljeezera bado wanamkumbuka pressman wao aliyeko mahabusu pale cairo,mwananchi hata habari zake kuziandika wanaogopa kama pressman man wao alikuwa na ukoma.
 
TAARIFA

Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally, asubuhi ya leo tarehe 02 Desemba, 2019 amewasili kisiwani Pemba kwa ziara ya siku tatu akitokea Kisiwani Unguja alipohitimisha ziara yake jioni jana tarehe 01 Desemba, 2019.

Ziara hiyo inalenga kuimarisha Uhai wa Chama, kukagua miradi na kuimarisha mahusiano baina ya Chama na Serikali na kuendelea kukifanya Chama kuwa karibu zaidi na wananchi.

Imetolewa na;
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM).

View attachment 1279105View attachment 1279106
Hivi mikutano imeruhusiwa? Maana huku Polepole ,Kule Bashiru Wapinzani wao Mahakamani
 
I feel sorry kwa gazeti la Mwananchi(nilikuwa mpenzi wao mkubwa)but now nalo limegeuka na mbaya zaidi limemtelekeza mwandishi wao aliyepotea katika mazingira ya utatanishi,
Mkuu nakumbusha tu kwamba gazeti la Mwananchi ni mali ya CCM. Ndio wamiliki. Naomba hilo lijue.
 
Hivi mikutano imeruhusiwa? Maana huku Polepole ,Kule Bashiru Wapinzani wao Mahakamani
Hao hafanyi mikutano wanakangua utekelezaji Wa ilani yao kama inafikiwa kama kuna tatizo mahala wanachukuwa hatuna.tofauti na wapinzani wao wanafanya mikutano na kutoa matusi hawahamasishi maendeleo wakikuta kinafanyika kitu Kazi yao kupiga ndio maana wameambiwa siasa hadi 2020 ndio waseme mbona mliahidi jambo Fulani hamkufanya tupeni sisi tufanye hiyo ndio siasa. Sasa mambo yanafanyika wao wanapiga hata jambo halijaisha
 
Hao hafanyi mikutano wanakangua utekelezaji Wa ilani yao kama inafikiwa kama kuna tatizo mahala wanachukuwa hatuna.tofauti na wapinzani wao wanafanya mikutano na kutoa matusi hawahamasishi maendeleo wakikuta kinafanyika kitu Kazi yao kupiga ndio maana wameambiwa siasa hadi 2020 ndio waseme mbona mliahidi jambo Fulani hamkufanya tupeni sisi tufanye hiyo ndio siasa. Sasa mambo yanafanyika wao wanapiga hata jambo halijaisha
Watanzania sio wapumbavu ilani ni pamoja na kuwapokea Wabunge na Madiwani waliofikia bei?ilani ni miradi ,wangekuwa wanaongea na watekelezaji wa miradi,mikutano ya hadhara inayofanywa nayo ni ilani?
 
TAARIFA

Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally, asubuhi ya leo tarehe 02 Desemba, 2019 amewasili kisiwani Pemba kwa ziara ya siku tatu akitokea Kisiwani Unguja alipohitimisha ziara yake jioni jana tarehe 01 Desemba, 2019.

Ziara hiyo inalenga kuimarisha Uhai wa Chama, kukagua miradi na kuimarisha mahusiano baina ya Chama na Serikali na kuendelea kukifanya Chama kuwa karibu zaidi na wananchi.

Imetolewa na;
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM).

View attachment 1279105View attachment 1279106
Kwa Pemba anajisumbua tu wanaona uchaguzi tayar ndio wanajipeleka peleka.
 
Hao hafanyi mikutano wanakangua utekelezaji Wa ilani yao kama inafikiwa kama kuna tatizo mahala wanachukuwa hatuna.tofauti na wapinzani wao wanafanya mikutano na kutoa matusi hawahamasishi maendeleo wakikuta kinafanyika kitu Kazi yao kupiga ndio maana wameambiwa siasa hadi 2020 ndio waseme mbona mliahidi jambo Fulani hamkufanya tupeni sisi tufanye hiyo ndio siasa. Sasa mambo yanafanyika wao wanapiga hata jambo halijaisha

akili ya wapi hapo/.
soma juu kilichandikwa, anakwenda KUKAGUA UHAI WA CHAMA na sio ILANI.
mnatumia vitu gani kufikiri huko kwenu ?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom