Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,205
- 4,695
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally amewahimiza wanaCCM wa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam kuenzi miaka 100 ya fikra za Mwalimu Nyerere, Aprili 2022.
Ameysema hayo leo tarehe 21 Februari, 2021 akizungumza na Umoja wa Vijana wa CCM Chuo Kikuu Cha Dar es salaam.
"Mwaka kesho Aprili, Baba wa Taifa Mwl. Nyerere atatimiza miaka 100 ya uhai wake tangu Aprili, 2022 azaliwe mpaka sasa. Kutakua na sherehe kubwa katika nchi yetu, na kwa Chama Chetu lazima tudhihirishe kabisa kwamba tunamuenzi baba wa Taifa mwaka kesho mwezi Aprili."
"Na mimi nipendekeze hapa mbele yenu kwamba, WanaCCM hapa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam, muwe mstari wa mbele katika maandalizi ya sherehe hizo, kwa sababu miaka 100 ya utoto wake, malezi yake, maisha yake ya kisiasa, maisha yake ya kiraia, mpaka anafariki na hadi sasa yamebeba urithi mkubwa wa Taifa letu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kikiwepo"
Aidha, Katibu Mkuu pamoja na mambo mengine amesisitiza umuhimu wa Utunzaji wa mazingira kutokana na kutoridhishwa na usafi katika Jiji la Dar es Salaam.
Imetolewa na;
Said Said Nguya
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
Ameysema hayo leo tarehe 21 Februari, 2021 akizungumza na Umoja wa Vijana wa CCM Chuo Kikuu Cha Dar es salaam.
"Mwaka kesho Aprili, Baba wa Taifa Mwl. Nyerere atatimiza miaka 100 ya uhai wake tangu Aprili, 2022 azaliwe mpaka sasa. Kutakua na sherehe kubwa katika nchi yetu, na kwa Chama Chetu lazima tudhihirishe kabisa kwamba tunamuenzi baba wa Taifa mwaka kesho mwezi Aprili."
"Na mimi nipendekeze hapa mbele yenu kwamba, WanaCCM hapa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam, muwe mstari wa mbele katika maandalizi ya sherehe hizo, kwa sababu miaka 100 ya utoto wake, malezi yake, maisha yake ya kisiasa, maisha yake ya kiraia, mpaka anafariki na hadi sasa yamebeba urithi mkubwa wa Taifa letu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kikiwepo"
Aidha, Katibu Mkuu pamoja na mambo mengine amesisitiza umuhimu wa Utunzaji wa mazingira kutokana na kutoridhishwa na usafi katika Jiji la Dar es Salaam.
Imetolewa na;
Said Said Nguya
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)