Dkt. Anna P. Makakala ni kielelezo kwamba wanawake wakiaminiwa wanaweza

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Katika utawala wa JPM mwanamke aliyekabidhiwa kazi ngumu na akaimudu bila kujitutumua au kuonyesha ule uwanawake au kuonyesha kukwamishwa na mfumo dume ni Kamishna Jenerali wa Uahamiaji Dkt. Anna Makakala.

Nikiangalia taasisi anayoongoza hatua ilizopiga kwenye huduma, nikifuatilia kauli zake mbele ya vyombo vya habari na nikiangalia idadi ya malalamiko ya raia dhidi yake nataka nisema wanawake wanaweza.

Kwa mwonekano huyu Mama inaonyesha aliteuliwa akiwa bado mdogo sana, nadhani Hadi Sasa Hana miaka 50 lakini amesimama imara sana. Kuongoza vyombo vya dola ndani ya mkikimkiki wa JPM ukatoka bila kutunishiana misuli na wananchi ni busara kubwa sana.

Niliona tuhuma nyingi za uraia zikifikishwa kwake lakini sijawahi msikia akitoka adharani kutoa kauli zakutisha, always hoja zimekuwa zikijibiwa na wasaidizi wake hii ikiwa ni njia yakuepusha kuichafua taasisi.

Nimwombe mama Samia Suluhu, Rais wa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania ajipe muda kuibua akina Makakala wengi watakaomsaidia.

Hongera Makakala, umefanya kwa sehemu kubwa na umevuka salama endelea na busara hiyo hiyo kwa utumishi wako ndani na nje ya Idara ya Uhamiaji.
 
Huyu mama binafsi namkubali sana, ni mtu imara na anajua majukumu yake.
 
Nimpongeze kwa ushupavu, kukaa karibu na Rais non stop for five years mnaambatana naye na bado akaweza kusimamia ofisi ni ushujaa. Ila kingine ninaweza kusema amefanya Jambo kubwa kwenye pasipoti za electronic, tukienda huko duniani tunaheshimika

Ila bado ana kazi kwenye uraia, ajitaidi atafute Suluhu ya Mtanzania ni Nani. Watu wapewe vitambulisho waache kusumbuliwa, wasiofaa wafukuzwe au Wapewe mavibali Kama zamani huku Kagera mfugaji unamkuta anakibali Cha mgeni.

Hongera mama mtegemee Mungu usipate doa Wala dhambi yakiutawala.

Hapo tukimsifia wanaume lazima waone wivu washinikize atoke, aaahaaaaa hii nchi tunaijua
 
Huyu mama binafsi namkubali sana, ni mtu imara na anajua majukumu yake
Nini kinachosababisha vijana wengi mamia wa vijana wa kitanzania kushikwa Afrika ya kusini wakiwa hawana passport na kurudishwa nchini kisa hawana passport?
 
ninaweza kusema amefanya Jambo kubwa kwenye pasipoti za electronic,
Vipi wale mamia ya vijana ambao hushikwa Afrika ya kusini wakiwa hawana passport na kurudishwa nchini kisa hawana passport na kuishia mahakama kisutu msababishaji wa wao kukosa passport nani? Tuanzie hapo
 
Kwa hili Uhamiaji wako vizuri kwenye huduma na hata kazi zao na manadiliko tumeyaona mengi tu.

Ila tunaomba Uraia pacha walishughulikie kwani tuko nyuma sana.

Yaani viongozi wanaogopa hata kulizungumzia limekuwa kama taboo
 
Vipi wale mamia ya vijana ambao hushikwa Afrika ya kusini wakiwa hawana passport na kurudishwa nchini kisa hawana passport na kuishia mahakama kisutu msababishaji wa wao kukosa passport nani? Tuanzie hapo
Nilipotaka kwenda AK nilienda uhamiaji na kuomba pass kisha nikalipia na kupata nikapata VISA na kwenda na kurudi wale vijana huwa hawapendi kufata taratibu na baadhi pass zikiisha mda hawaendi HA kurenew nadhani wao wajitafakari.

Kama alivyosema mdau yule mama ni mstaraabu sana na anachapa kazi ila aongeze bidii zaidi kwenye swala la urahisishaji wa kupatikana kwa pass na kuzuia uhamiaji haramu
 
Nilipotaka kwenda AK nilienda uhamiaji na kuomba pass kisha nikalipia na kupata nikapata VISA na kwenda na kurudi wale vijana huwa hawapendi kufata taratibu na baadhi pass zikiisha mda hawaendi
Uzuri wote waliorudishwa wapo .Wakitapika nyongo zao hapo uhamiaji kitengo cha passport habaki mtu Hata yeye ataponea chupuchupu labda.

Unatoa jibu rahisi kwenye swali gumu
 
Usela wa kijinga....
Usela wa kizamani...

Wanadhani kuzamia ama kuondoka nchini is always about short cuts kama ilivyo zamani.

Mimeona mtu kaingia ubalozi wa US akiwa na passport fake ya Tanzania... kanyimwa... sasa huyu anafikilia nn?
Nini kinachosababisha vijana wengi mamia wa vijana wa kitanzania kushikwa Afrika ya kusini wakiwa hawana passport na kurudishwa nchini kisa hawana passport?
 
Passport kupata ni rahisi sana...
Usela umewazidi .. uhuni wa kizamani
Vipi wale mamia ya vijana ambao hushikwa Afrika ya kusini wakiwa hawana passport na kurudishwa nchini kisa hawana passport na kuishia mahakama kisutu msababishaji wa wao kukosa passport nani? Tuanzie hapo
 
Labda hatuelewi vingine... ila passport miaka hii sio ngumu.

Nashirikiana na mtu wa safari za nje anawaongoza watu kupata pass kwa wiki 1 ama 2 na hakuna ugumu na tip ni elfu 10 tu... sio rushwa..
Uzuri wote waliorudishwa wapo .Wakitapika nyongo zao hapo uhamiaji kitengo cha passport habaki mtu Hata yeye ataponea chupuchupu labda.

Unatoa jibu rahisi kwenye swali gumu
 
Passport kupata ni rahisi sana...
Usela umewazidi .. uhuni wa kizamani
Sio kweli kuna masharti ya kijinga ya kupata passport mtu anaambiwa lete barua ya mwaliko Fursa ina mwaliko ? .Kijana anaambiwa South Afrika kuna fursa anasema ngoja niende nikatizame fursa anaenda kuomba passport unamkomalia lete uthibitisho wa safari akili zimo wewe? nchi zote majirani wanatoa passport kwa raia mradi ana kitambulisho cha taifa

Kitengo cha passport ndio wanachafua jina la Tanzania Afrika ya kusini.Nchi mbili ndizo zinaongoza kuzalisha wasio na passport Afrika kusini nao ni Tanzania na Ethiopia kwa vigezo vyao vya kijinga vya kubania kutoa passport

Tatizo la wazamiaji wasio na Pasport muhusika mkuu ni uhamiaji kitengo cha passport
 
Labda hatuelewi vingine... ila passport miaka hii sio ngumu.

Nashirikiana na mtu wa safari za nje anawaongoza watu kupata pass kwa wiki 1 ama 2 na hakuna ugumu na tip ni elfu 10 tu... sio rushwa..
Issue sio muda ni vigezo walivyoweka ni vya kuombea visa ubalozini sio rafiki kwa vijana wengi.Wao wabaki kutoa passport tu maswali ya kijinga a kuuliza unaenda kufanya nini ziachiwe balozi husika zitoazo visa

Mfano mimi nataka kwenda kuangalia fursa kama za kufanya umachinga kama ziko kule unataka nikuthibitishiaje?

Capetown kuna masai kibao wanauza dawa za kimasai na viatu vya kimasai passport hawana ila fursa wamepata sasa ikitokea siku wakavurumishwa kwa kukosa passport wa kulaumiwa nani kama sio kitengo cha passport?
 
Back
Top Bottom