Dk. Slaa: UCHAGUZI WIZI MTUPU

Mzito Kabwela

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
18,857
7,614
Matokeo ya Uchaguzi mkuu yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yalijaa utata, Mwanahalisi limegundua.

Taarifa kutoka ndani ya NEC, vyama vya siasa na baadhi ya wagombea, zinasema matokeo yaliyotolewa yanatofautianma na kura halisi zilizopigwa.

Kwa mujibu wa baadhi ya mawakala wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), matokeo mikononi mwao yanatofautiana sana na yale yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)

Matokeo mikononi mwa mawakala kutoka mikoa 18 ya Tanzania Bara na mitatu ya Zanzibar, hadi juzi jumatatu yanathibitisha kuwepo kwa tofauti kati ya idadi ya vituoni na ile iliyotangazwa na NEC.

Katika jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro matokeo yaliyotangazwa na NEC yanaonyesha kuwa CCMimepata kura za Urais 35,910 huku Chadema ikionyeshwa kupata kura 18,513. Lakini matokeo ambayo yamekusanywa na mawakala wa Chadema yanaonyesha CCM imepata kura 20,120 huku Chadema ikipata kura 26,724.

Katika jimbo la Karatu Mkoani Arusha, hesabu za NEC zinaonyesha CCM imepata kura za urais 24,382 huku Chadema ikipata kura 41 tu angalau kwa mujibu wa matangazo ya Televisheni. Bali kwa mujibu wa matokeo yaliyokusanywa na mawakala ambayo yamesainiwa na mawakala wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo CCM imepata kura 24,364 na Chadema ilipata kura 43,137

Jimbo jingine ambalo matokeo yake yamejaa utata ni Geita, mkoani Mwanza. Matokeo yaliyotangazwa na NEC katika jimbo hilo yanaonyesha kuwa CCM imepata kura 17,792 na Chadema imeambulia 3,989. Lakini Matokeo mikononi mwa mawakala yanaonyesha kuwa CCM imepata kura 30,960 na Chadema kura 15,736. NEC ilikiri kuwapo kwa kasoro katika jimbo la Geita na ilikubali kufanyia Marekebisho.

Katika jimbo la Ubungo Mkoani Dar es salaam matokeo ya NEC yameipa CCM kura 68,727 na Chadema kura 65,450. Hata hivyo kwa mujibu wa matokeo mikononi mwa mawakala yanaonyesha kuwa Chadema imepata kura 72,252 na CCM kura 70,472.


Uchunguzi wa Mwanahalisi umebaini kuwa licha ya tofauti ya matokeo ya vituoni na yale ya NEC, matokeo katika baadhi ya maeneo hayakurekodiwa kwenye karatasi za tume, rasmi kwa shughuli hiyo. Gazeti limeona matokeo yaliyorekodiwa kwenye karatasi za kawaida na magamba magumu ya makasha, ingawa zimegongwa mhuri inayoonekana kuwa ni ya Tume. Matokeo ya aina hii yanashurutisha kuwepo ujenzi wa shaka juu ya usalama wa kura na uwezekano wa matokeo kughushiwa

Mwanahalisi limeelezwa kuwa mbali na kasoro hiyo ya kutokuwapo kwa fomu za kurekodia matokeo, katika baadhi ya majimbo yaliyofanya uchaguzi, majumuisho ya kura za urais hayakufanyika.

Gazeti hili lilitaka kujua maoni ya Dk. Slaa juu ya taarifa kuwa kuna maeneo ambako majumuisho ya kura za urais hayakufanyika naye alijibu " wewe unazungumza hilo; matatizo yaliyopo katika uchaguzi huu ni mkubwa sana. Kuna Uchafu mwingi. Ndio maana sisi tunasisitiza kuwa hatuwezi kukubaliana na matokeo yaliyotangazwa" Anasema " Tunaendelea kukusanya nyaraka zote za uchaguzi na si muda mrefu ujao, tutaeleza dunia ni kitugani kilifanyika, wapi na akina nani walihusika. Tutaeleza pia hatua gani itafuata baada ya hapa"

Gazeti hili lina taarifa kuwa baadhi ya majimbo ambako matokeo ya Urais hayakutangazwa ni Kiteto, Segerea, Muheza, Kibakwe, Kinondoni, Ilala na Moshi Vijijini.

Kutoka Morogoro taarifa zinaeleza utata wa aina yake. Kati ya wapiga kura 422 waliotarajiwa kupiga kura katika kituo cha shule ya msingi Msufini, kata ya Msufini Manispaa ya Morogoro HAKUNA HATA MMOJA ALIYEKUWA NA SHAHADA YA KUPIGIA KURA

NUNUA MWANAHALISI LA LEO TAREHE 10/11/2011 UONE JINZI CCM WALIVYO NA TAALUMA YA MWAKA 47 YA KUIBA
 
HALAFU ETI CCM WANATHUBUTU KUSEMA WAMESHINDA KWA KISHINDO!!!!!!!!!! NI AIBU KUBWA SANA HII....MIMI NASEMA IPO SIKU!!!!!!! ATAWAMALIZA HAWA MAFISADI WA CCM ......IPO SIKU NA INAKUJA UPESI......MNYONGE MNYONGENI LAKINI HAKI YAKE MPENI....MAANA SIKU....ATAKAPOAMUA KUIDAI KWA NGUVU......WATU KAMA HAWA MAFISADI WATATAFUTA MVUNGU WA KUJIFICHA....ole wao ccm Siku inakuja! yaja upesi...Watu wanamuona Dr Slaa kwamba Mzushi lakini hawajui kuwa CCM imechakachua kwa kiwano cha kutisha....
 
kaka nchi hii hata tembo anawezatambulishwa simba na ikasimamiwa hivyo. aibu tupu !!
 
Hivi CCM wataacha lini kuchakachua? Mimi nazani mwaka 2015 Wadau tufanye kama watu wa Nyamagana na Ilemela. Hakuna kura itakayoibwa
 
Jamani mimi nilijua Kikwete hakushinda ,hata kama angeshinda siyo kama tulivyotangaziwa, yaani sisiemu wanataka kututania kiasi hiki wanadhani
tutaendelea kukubali upuuzi wa namna hii!!!!;
Watanzania tuamke tuache mzaha nchi inaagamia kwa sababu ya upole watu na kusema ndiyo katika kila japo pasipo kuuliza kwa nini!!!!!!!!!!!?
 
nimeamini " kweli sikio la binadamu haliwezi kuzidi kichwa"
labda yuchukue la tembo
 
Walikuwa wamezoea kumnyonga Maalim seif huko zanzibar.Safari hii wamekwaa kisiki cha mpingo, hadi kieleweke, wamezoea vya kunyonga.Sasa hivi wanagombania cheo cha Spika ni hulka yao wamezoea kula vilivyopakwa DAMU YA MWANADAMU .Nyerere aliwahi kusema" ukila nyama ya mtu utaendelea kula nyama ya mtu maisha yako yote" wametenda dhambi ya ubaguzi dhambi hiyo itaendelea kuwatafuna mpaka iwamalize, Wamembagua Dr.slaa na chama chake, leo wanaanza kumbagua Sitta wakitoka kwa Sitta hawabaki salama hao mapambafuuuu
 
Wizi wa kura kura umekuwa dhahiri, ila nasikitika tumekuwa mno very slow kukusanya ushahidi na kurespond....
 
CCM mnajisikiaje jamani ndio maana akina Kibaki na Mugabe waliudhuria kushuhudia jinsi technologia ya wizi wa kura ilivyokomaa.
 
kikwete alijua hali ni ngumu, si alisema watashinda kwa asilimia zaidi ya walizopata awamu ya kwanza... sasa kikowapi? wamezidiwa mpaka wakajitahidi kuiba ili wapate japo hizo 61% ambazo si sahihi kwakuwa zimefanyiwa ubadhilifu na NEC, ki msingi hapo hakuna uchaguzi huru
 
Sasa nini kifanyike wadau?
Tusiishie kulalamika tu kwani tunazidi kupata vidonda vya tumbo.
Tufanye nini?
 
Biharamulo JK hakufikisha hata kura 5000, na bukombe hardly JK alikuwa na kura 3000 tu, hizo wilaya hali ilikuwa tete kwa CCM na JK, nguvu ya ziada kubwa sana imetumika kumpa kura JK, yaani hakubaliki kabisa mpaka kesho
nadhani Tanzania tunashida/tatizo la waandishi wa habari za kichunguzi, zaidi ni za udaku tu, lakini kama kungekuwa na waandishi wa aina hiyo kama Kubenea na MWanahalisi kwa ujumla wake, uchafu mwingi wa uchaguzi ungepatikana,
 
matokeo ya uchaguzi mkuu yaliyotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi (nec) yalijaa utata, mwanahalisi limegundua.

Taarifa kutoka ndani ya nec, vyama vya siasa na baadhi ya wagombea, zinasema matokeo yaliyotolewa yanatofautianma na kura halisi zilizopigwa.

Kwa mujibu wa baadhi ya mawakala wa chama cha demokrasia na maendeleo (chadema), matokeo mikononi mwao yanatofautiana sana na yale yaliyotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi (nec)

matokeo mikononi mwa mawakala kutoka mikoa 18 ya tanzania bara na mitatu ya zanzibar, hadi juzi jumatatu yanathibitisha kuwepo kwa tofauti kati ya idadi ya vituoni na ile iliyotangazwa na nec.

katika jimbo la hai, mkoani kilimanjaro matokeo yaliyotangazwa na nec yanaonyesha kuwa ccmimepata kura za urais 35,910 huku chadema ikionyeshwa kupata kura 18,513. Lakini matokeo ambayo yamekusanywa na mawakala wa chadema yanaonyesha ccm imepata kura 20,120 huku chadema ikipata kura 26,724.

katika jimbo la karatu mkoani arusha, hesabu za nec zinaonyesha ccm imepata kura za urais 24,382 huku chadema ikipata kura 41 tu angalau kwa mujibu wa matangazo ya televisheni. Bali kwa mujibu wa matokeo yaliyokusanywa na mawakala ambayo yamesainiwa na mawakala wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo ccm imepata kura 24,364 na chadema ilipata kura 43,137

jimbo jingine ambalo matokeo yake yamejaa utata ni geita, mkoani mwanza. Matokeo yaliyotangazwa na nec katika jimbo hilo yanaonyesha kuwa ccm imepata kura 17,792 na chadema imeambulia 3,989. Lakini matokeo mikononi mwa mawakala yanaonyesha kuwa ccm imepata kura 30,960 na chadema kura 15,736. Nec ilikiri kuwapo kwa kasoro katika jimbo la geita na ilikubali kufanyia marekebisho.

katika jimbo la ubungo mkoani dar es salaam matokeo ya nec yameipa ccm kura 68,727 na chadema kura 65,450. Hata hivyo kwa mujibu wa matokeo mikononi mwa mawakala yanaonyesha kuwa chadema imepata kura 72,252 na ccm kura 70,472.


uchunguzi wa mwanahalisi umebaini kuwa licha ya tofauti ya matokeo ya vituoni na yale ya nec, matokeo katika baadhi ya maeneo hayakurekodiwa kwenye karatasi za tume, rasmi kwa shughuli hiyo. Gazeti limeona matokeo yaliyorekodiwa kwenye karatasi za kawaida na magamba magumu ya makasha, ingawa zimegongwa mhuri inayoonekana kuwa ni ya tume. Matokeo ya aina hii yanashurutisha kuwepo ujenzi wa shaka juu ya usalama wa kura na uwezekano wa matokeo kughushiwa

mwanahalisi limeelezwa kuwa mbali na kasoro hiyo ya kutokuwapo kwa fomu za kurekodia matokeo, katika baadhi ya majimbo yaliyofanya uchaguzi, majumuisho ya kura za urais hayakufanyika.

gazeti hili lilitaka kujua maoni ya dk. Slaa juu ya taarifa kuwa kuna maeneo ambako majumuisho ya kura za urais hayakufanyika naye alijibu " wewe unazungumza hilo; matatizo yaliyopo katika uchaguzi huu ni mkubwa sana. Kuna uchafu mwingi. Ndio maana sisi tunasisitiza kuwa hatuwezi kukubaliana na matokeo yaliyotangazwa" anasema " tunaendelea kukusanya nyaraka zote za uchaguzi na si muda mrefu ujao, tutaeleza dunia ni kitugani kilifanyika, wapi na akina nani walihusika. Tutaeleza pia hatua gani itafuata baada ya hapa"

gazeti hili lina taarifa kuwa baadhi ya majimbo ambako matokeo ya urais hayakutangazwa ni kiteto, segerea, muheza, kibakwe, kinondoni, ilala na moshi vijijini.

kutoka morogoro taarifa zinaeleza utata wa aina yake. Kati ya wapiga kura 422 waliotarajiwa kupiga kura katika kituo cha shule ya msingi msufini, kata ya msufini manispaa ya morogoro hakuna hata mmoja aliyekuwa na shahada ya kupigia kura

nunua mwanahalisi la leo tarehe 10/11/2011 uone jinzi ccm walivyo na taaluma ya mwaka 47 ya kuiba

sema dk usiogope sema! Sisi watanzania hatuogopi mafashisti.
 
CCM is Tanzania's greatest enemy.
Kwa wizi huu wa kutisha CCM ijiandae kuondoka madarakani kwa aibu kabla ya 2015,haiwezekani kuongozwa na wezi na siku si nyingi nchi hii italipuka.Watanzania hawawezi kukubali kuendelea kuongozwa na mtandao wa wezi.JK nusuru nchi kwa kutafuta suluhu na Mshindi halali(Slaa) acha ubabe kwani wanaokulinda wamekuchoka.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom