Nimesikia kupitia vyombo mbalimbali vikimnukuu Dk. Slaa jinsi alivyolielekeza kanisa lisikubali kupokea michango ya mafisadi na kudai kuwa fedha hizo ni najisi. Siamini kabisa kuwa Dk Slaa anaweza kusema maneno hayo ukizingatia kuwa yeye alikuwa Padri aliyekuwa anaongoza waumini wengi tu ambao kwa namna moja au nyingine sitaki kuamini kuwa wakati huo aliwahi kukataa sadaka za waovu ambao hata kwa jicho la nyama kwa mtu makini anaweza kuwabaini kwenye hizo nyumba za ibada.
Mafundisho ya kanisa wakati wote nijuavyo mimi si kuwahukumu waovu bali kuwafundisha kutubu na kuacha uovu wao ili kama kuna namna ambayo walikuwa wanafanya isivyo halali, iwe ni kujipatia fedha, au ujanja wowote watubu ili wawe waumini wazuri. Leo hii Dk. Slaa anapojaribu kufunga mlango wa waovu kufika kanisani kwa namna yeyote kwangu mimi huko ni kupotoka na kuchanganya mambo. Kanisa haliongozwi kwa taratibu za kisiasa na wala haliwezi kuchukulia mambo kama dunia ifanyavyo au kwa matakwa ya kisiasa. Kanisa wakati wote husisitiza msamaha na utakaso, hakuna sehemu nyingine Fisadi,mwizi, jambazi, kibaka pamoja na waovu wengize wanaweza kuhurumiwa na kupata msamaha wa kweli hadi kuwa viumbe vipya nje ya mafundishi ya kiimani.
Dk Slaa aelewe wazi kuwa hao mafisadi anaowajua kwa majina ni wachache sana, ila kuna idadi kubwa ya waovu wanaopeleka michango yao makanisani huku wakiwa wamejaa uovu, kanisa halina muda kabisa wa kufanya kazi ya kuhukumu mtu maana kazi hiyo ni ya Mungu.
Nahisi Dk slaa anahofu na nguvu ya hao anaowaita mafisadi endapo watajaribu kugombea nafsi ambayo Dk slaa naye anaimezea mate.Dk Slaa ni mtu makini ambaye naamini anabusara za kutosha kuwasaidia wananchi wa Tanzania, kama anauhakika na ushahidi angewafikisha mahakamani hao mafisadi wote ili sheria za kibinadamu zichukuwe mkondo wake? Sioni mantiki ya kulalamika pembeni kwa kuyashawishi makanisa wakati yeye anauwezo wa kudhihirishia umma uovu uliopo. vinginevyo naona huu ni unafiki tu. Sijawahi kusikia hata siku moja kanisa likihakiki vyanzo vya mapato vya waumini wao na usafi wao, nijuavyomimi kila siku kanisa huhamasisha watu waache dhambi, je Slaa anauhakika hao anaodai ni mafisadi hawajatubu? kwahiyo Dk slaa ni mwanadamu msafi anayeweza kukemea usafi wa watu wengine? Nijuavyo mimi masuala ya Mungu yeye yalimshinda ndiyo maana akavua joho na kujiunga na siasa, ingekuwa ni busara akaachana na kanisa maana hata yeye anamengi ya kuhojiwa juu ya uchamungu wake nafikiri haya mambo ya kiroho angekaa tu pembeni.
Mafundisho ya kanisa wakati wote nijuavyo mimi si kuwahukumu waovu bali kuwafundisha kutubu na kuacha uovu wao ili kama kuna namna ambayo walikuwa wanafanya isivyo halali, iwe ni kujipatia fedha, au ujanja wowote watubu ili wawe waumini wazuri. Leo hii Dk. Slaa anapojaribu kufunga mlango wa waovu kufika kanisani kwa namna yeyote kwangu mimi huko ni kupotoka na kuchanganya mambo. Kanisa haliongozwi kwa taratibu za kisiasa na wala haliwezi kuchukulia mambo kama dunia ifanyavyo au kwa matakwa ya kisiasa. Kanisa wakati wote husisitiza msamaha na utakaso, hakuna sehemu nyingine Fisadi,mwizi, jambazi, kibaka pamoja na waovu wengize wanaweza kuhurumiwa na kupata msamaha wa kweli hadi kuwa viumbe vipya nje ya mafundishi ya kiimani.
Dk Slaa aelewe wazi kuwa hao mafisadi anaowajua kwa majina ni wachache sana, ila kuna idadi kubwa ya waovu wanaopeleka michango yao makanisani huku wakiwa wamejaa uovu, kanisa halina muda kabisa wa kufanya kazi ya kuhukumu mtu maana kazi hiyo ni ya Mungu.
Nahisi Dk slaa anahofu na nguvu ya hao anaowaita mafisadi endapo watajaribu kugombea nafsi ambayo Dk slaa naye anaimezea mate.Dk Slaa ni mtu makini ambaye naamini anabusara za kutosha kuwasaidia wananchi wa Tanzania, kama anauhakika na ushahidi angewafikisha mahakamani hao mafisadi wote ili sheria za kibinadamu zichukuwe mkondo wake? Sioni mantiki ya kulalamika pembeni kwa kuyashawishi makanisa wakati yeye anauwezo wa kudhihirishia umma uovu uliopo. vinginevyo naona huu ni unafiki tu. Sijawahi kusikia hata siku moja kanisa likihakiki vyanzo vya mapato vya waumini wao na usafi wao, nijuavyomimi kila siku kanisa huhamasisha watu waache dhambi, je Slaa anauhakika hao anaodai ni mafisadi hawajatubu? kwahiyo Dk slaa ni mwanadamu msafi anayeweza kukemea usafi wa watu wengine? Nijuavyo mimi masuala ya Mungu yeye yalimshinda ndiyo maana akavua joho na kujiunga na siasa, ingekuwa ni busara akaachana na kanisa maana hata yeye anamengi ya kuhojiwa juu ya uchamungu wake nafikiri haya mambo ya kiroho angekaa tu pembeni.