nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Edward Kinabo, Mufindi
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amewataja vigogo na watendaji wa serikali wakiwamo mawaziri wawili na wabunge akiwatuhumu kufanya ufisadi wa kujigawia vitalu vya uvunaji magogo katika msitu wa taifa uliopo Mufindi mkoani Iringa.
Miongoni mwa aliowataja ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami, huku akisisitiza kuwa wamepata vitalu hivyo kifisadi.
Dk. Slaa aliwataja mawaziri hao na watuhumiwa wengine wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Mafinga katika mfululizo wa mikutano ya hadhara na maandamano ya chama hicho yaliyoingia mkoani hapa jana.
Alisema hatua ya mawaziri hao kumiliki vitalu hivyo si haki, kwani inasababisha kuwapo mgongano wa kimasilahi baina yao na msitu huo ambao kwa nafasi zao kama viongozi wa kiserikali walipaswa kuusimamia kwa haki na uwazi ili uwanufaishe wananchi, hususan wakazi wa Mufindi.
Akifafanua hoja yake hiyo, Dk. Slaa alisema Dk. Chami kwa nafasi yake kama Waziri wa Viwanda na Biashara, ndiye mwenye jukumu la moja kwa moja kusimamia haki kwenye msitu huo unaotumiwa pia na Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi Paper Mills, lakini naye amechukua vitalu tena katika utaratibu aliosema si wa wazi.
Alisema mwaka jana waziri huyo akiwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara ndiye aliyeongoza kamati maalumu ya serikali iliyokwenda Mufindi kuchunguza mgogoro wa kiwanda hicho pamoja na msitu kinaoutumia, lakini kinyume cha kanuni za kibunge, kiongozi huyo wa serikali sawa na wenzake akiwamo William Lukuvi aliowataja, hawakusema wazi kama wana masilahi katika msitu huo.
Naitaka serikali ieleze ugawaji huu wa vitalu vya msitu wa Mufindi ulitangazwa lini na utaratibu gani wa uwazi ulitumika ili kila Mtanzania wakiwamo wananchi wenyewe wa Mufindi wawe na haki ya kushindania vitalu hivyo.
Pili, namtaka Chami na viongozi wengine wa kiserikali waliochukua vitalu vya msitu huo wajieleze kwa nini wasiwajibishwe kwa kumiliki vitalu vya msitu bila kutangaza wazi masilahi waliyonayo ya kiuongozi katika msitu huo.
Tutawasha moto bungeni mpaka haki ya wananchi na msitu wao ipatikane, hawa ni mafisadi. Wakituzidi kwa wingi wao bungeni, basi tutafanya maandamano yasiyokoma nchi nzima hadi mafisadi hawa wawajibishwe na haki za wananchi zitimizwe, alisema Dk. Slaa na kushangiliwa na umati wa watu.
Katika orodha hiyo Dk. Slaa alimtaja pia Mbunge wa Kibakwe, Geogre Simbachawene (CCM) kugawiwa vitalu vya msitu huo.
Alisema kwa ujumla anayo orodha ya vigogo na watendaji 540 ambao wamegawiwa vitalu vya msitu huo na kuwanyima fursa wananchi wa Mufindi kumiliki vitalu hivyo kinyume cha taratibu.
Wakati huo huo, Dk. Slaa alisema wabunge wa chama hicho akiwamo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Zitto Kabwe, wataongoza mashambulizi ya chama hicho bungeni kuhakikisha wananchi wakiwamo wafanyakazi walioachishwa kazi katika kiwanda cha karatasi Iringa wanalipwa mafao na stahili zao zote.
Alisema wafanyakazi wa kiwanda hicho wanaidai serikali mafao ya jumla ya sh bilioni tano ambayo yalipaswa kulipwa mara baada ya serikali kuuza kiwanda hicho kwa wawekezaji lakini hadi leo hayajalipwa.
Alisema CHADEMA itahakikisha inapigania masilahi ya wafanyakazi hao pamoja na wengine nchi nzima huku akisisitiza kuwa kama wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanatumia ubunge wao bungeni, CHADEMA itafanya maandamano yasiyokoma nchi nzima kuhakikisha haki zao zinalipwa. Alisema maandamano hayo pia watayafanya kama serikali haitasikiliza hoja nyingine zitakazowasilishwa na wabunge hao bungeni za kupigania wananchi, kama kupigania kushushwa kwa kodi, Katiba na nyinginezo.
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amewataja vigogo na watendaji wa serikali wakiwamo mawaziri wawili na wabunge akiwatuhumu kufanya ufisadi wa kujigawia vitalu vya uvunaji magogo katika msitu wa taifa uliopo Mufindi mkoani Iringa.
Miongoni mwa aliowataja ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami, huku akisisitiza kuwa wamepata vitalu hivyo kifisadi.
Dk. Slaa aliwataja mawaziri hao na watuhumiwa wengine wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Mafinga katika mfululizo wa mikutano ya hadhara na maandamano ya chama hicho yaliyoingia mkoani hapa jana.
Alisema hatua ya mawaziri hao kumiliki vitalu hivyo si haki, kwani inasababisha kuwapo mgongano wa kimasilahi baina yao na msitu huo ambao kwa nafasi zao kama viongozi wa kiserikali walipaswa kuusimamia kwa haki na uwazi ili uwanufaishe wananchi, hususan wakazi wa Mufindi.
Akifafanua hoja yake hiyo, Dk. Slaa alisema Dk. Chami kwa nafasi yake kama Waziri wa Viwanda na Biashara, ndiye mwenye jukumu la moja kwa moja kusimamia haki kwenye msitu huo unaotumiwa pia na Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi Paper Mills, lakini naye amechukua vitalu tena katika utaratibu aliosema si wa wazi.
Alisema mwaka jana waziri huyo akiwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara ndiye aliyeongoza kamati maalumu ya serikali iliyokwenda Mufindi kuchunguza mgogoro wa kiwanda hicho pamoja na msitu kinaoutumia, lakini kinyume cha kanuni za kibunge, kiongozi huyo wa serikali sawa na wenzake akiwamo William Lukuvi aliowataja, hawakusema wazi kama wana masilahi katika msitu huo.
Naitaka serikali ieleze ugawaji huu wa vitalu vya msitu wa Mufindi ulitangazwa lini na utaratibu gani wa uwazi ulitumika ili kila Mtanzania wakiwamo wananchi wenyewe wa Mufindi wawe na haki ya kushindania vitalu hivyo.
Pili, namtaka Chami na viongozi wengine wa kiserikali waliochukua vitalu vya msitu huo wajieleze kwa nini wasiwajibishwe kwa kumiliki vitalu vya msitu bila kutangaza wazi masilahi waliyonayo ya kiuongozi katika msitu huo.
Tutawasha moto bungeni mpaka haki ya wananchi na msitu wao ipatikane, hawa ni mafisadi. Wakituzidi kwa wingi wao bungeni, basi tutafanya maandamano yasiyokoma nchi nzima hadi mafisadi hawa wawajibishwe na haki za wananchi zitimizwe, alisema Dk. Slaa na kushangiliwa na umati wa watu.
Katika orodha hiyo Dk. Slaa alimtaja pia Mbunge wa Kibakwe, Geogre Simbachawene (CCM) kugawiwa vitalu vya msitu huo.
Alisema kwa ujumla anayo orodha ya vigogo na watendaji 540 ambao wamegawiwa vitalu vya msitu huo na kuwanyima fursa wananchi wa Mufindi kumiliki vitalu hivyo kinyume cha taratibu.
Wakati huo huo, Dk. Slaa alisema wabunge wa chama hicho akiwamo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Zitto Kabwe, wataongoza mashambulizi ya chama hicho bungeni kuhakikisha wananchi wakiwamo wafanyakazi walioachishwa kazi katika kiwanda cha karatasi Iringa wanalipwa mafao na stahili zao zote.
Alisema wafanyakazi wa kiwanda hicho wanaidai serikali mafao ya jumla ya sh bilioni tano ambayo yalipaswa kulipwa mara baada ya serikali kuuza kiwanda hicho kwa wawekezaji lakini hadi leo hayajalipwa.
Alisema CHADEMA itahakikisha inapigania masilahi ya wafanyakazi hao pamoja na wengine nchi nzima huku akisisitiza kuwa kama wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanatumia ubunge wao bungeni, CHADEMA itafanya maandamano yasiyokoma nchi nzima kuhakikisha haki zao zinalipwa. Alisema maandamano hayo pia watayafanya kama serikali haitasikiliza hoja nyingine zitakazowasilishwa na wabunge hao bungeni za kupigania wananchi, kama kupigania kushushwa kwa kodi, Katiba na nyinginezo.