Dk. Slaa aliipatia CHADEMA wabunge zaidi ya 30, Lowassa ameipatia CHADEMA wabunge 22

Yethero Mgale

JF-Expert Member
Apr 19, 2012
525
228
Wakati aliyekuwa katibu mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbrod Slaa anagombea Urais mwaka 2010, CHADEMA ilikuwa na wabunge wa kuchaguliwa na viti maalumu wasiozidi 10 ( Ndesamburo, Zitto Kabwe, Dk. Slaa, Halima Mdee na wengineo) baada ya uchaguzi CHADEMA ilivuna viti vya ubunge zaidi ya 30 na kuifanya iwe na wabunge wa kuchaguliwa na viti maalumu wapatao 48 na hivyo kuunda kambi ya rasmi ya upinzani bungeni.

Lakini hali ya mambo imekuwa tofauti kabisa mwaka huu wa 2015 ambapo CHADEMA ilimsimamisha ndugu Edward Lowassa kama mgombea wa Urais huku akiungwa mkono na vyama vya CUF, NCCR na NLD kwani CHADEMA imepata wabunge wa kuchaguliwa na viti maalum wapatao 70 ambalo ni ongezeko la wabunge 22 tu kutoka wabunge 48 waliowapata mwaka 2010.

Hivyo basi CHADEMA kwa kumsimamisha Lowassa mwaka 2015 kama mgombea wake kimepata wabunge wachache ukilinganisha na wabunge waliowapata mwaka 2010 kwa kumsimamisha Dk. Slaa kama mgombea wake bila ya kuungwa mkono na chama chochote.
 
Hivi wewe ni mzima kwel hata huna aibu unaona hizo namba zinalingana au ni kutaka kujitoa ufahamu..?

Kwa akili yako dr. Slaa angeweza leta hao wabunge ambao wamepatikana sasa hivi?

Tena kwa wizi ambao serikal yako ya ccm imeufanya kuhakikisha inashinda unaona hao wabunge ni wachache embu jitafakari hao wabunge ni wengi mno na nina hakika kama uchaguzi ungekuwa hauna figisu chadema ingepata wabunge wengi zaid acha kujipa matumaini
 
Hivi wew ni mzima kwel hata huna aibu unaona hizo namba zinalingana au ni kutaka kujitoa ufahamu..?

Kwa akili yako dr cassava angeweza leta hao wabunge ambao wamepatikana sasa hivi?

Tena kwa wizi ambao serikal yako ya ccm imeufanya kuhakikisha inashinda unaona hao wabunge ni wachache embu jitafakari hao wabunge ni wengi mno na nina hakika kama uchaguzi ungekuwa hauna figisu chadema ingepata wabunge wengi zaid acha kujipa matumaini
Tatizo lako wewe umesombwa na mafuriko ya Lowassa kwenda CHADEMA, hujui chochote kuhusu CHADEMA zaidi ya kutokwa povu.
 
nadhani Ruzuku huangaliiii kabisa ya 40% sijui umataka chama kibaki na ruzuku 26%
 
Kwa kumsimamisha EL kama mgombea inaashiria kuwa Chadema walikuwa na washauri wabovu sana kwenye upande wa reputation risk...it was clear kuwa hiyo pekee ingewafanya waanguke
 
hivi kutoka kura ml 2 mpaka kura ml 6 kama kichwani ni mzima utajua kati ya dr slaa na lowassa nani kakiletea chama faida? kutoka 48 wabunge mpaka 70 kama uoni tofauti kamwone dr wa Akili Ndugu.
 
Tatizo lako wewe umesombwa na mafuriko ya Lowassa kwenda CHADEMA, hujui chochote kuhusu CHADEMA zaidi ya kutokwa povu.

Wewe unajua nini kuhusu chadema:what: au povu linakutoka bure kama ngiri aliekoswa na chui, inamaana wabunge 70 kwa 48 wengi wepi:what: au nyie ndio wale mliopunguziwa maksi ili mfaulu:what:
 
Kuna watu wanaficha ukweli fulani. Wanasema EL aliungwa mkono na vyama vingine vitatu, lakini hawasemi kuwa pia naye aliviunga mkono vyama vingine vitatu ktk ubunge. Je, kwa kuviunga mkono katika ubunge, mbona hawasemi kuwa CHADEMA ilisacrifice kura za ubunge ambazo zingeongeza viti maalum?
 
Mleta mada ni mpuuzi tu na anatakiwa puuzwa huu ujinga aliondika hapa anatakiwa akajadiliane na watu wa lumumba wenzie maana hao ndo wanaweza danganyana na kufarijiana wakiamini uwepo wa lowasa haujafanya lolote lakini ukweli wanaujua
 
Wakati aliyekuwa katibu mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbrod Slaa anagombea Uraisi mwaka 2010, CHADEMA ilikuwa na wabunge wa kuchaguliwa na viti maalumu wasiozidi 10 ( Ndesamburo, Zitto Kabwe, Dk. Slaa, Halima Mdee na wengineo) baada ya uchaguzi CHADEMA ilivuna viti vya ubunge zaidi ya 30 na kuifanya iwe na wabunge wa kuchaguliwa na viti maalumu wapatao 48 na hivyo kuunda kambi ya rasmi ya upinzani bungeni. Lakini hali ya mambo imekuwa tofauti kabisa mwaka huu wa 2015 ambapo CHADEMA ilimsimamisha ndugu Edward Lowassa kama mgombea wa Urais huku akiungwa mkono na vyama vya CUF, NCCR na NLD kwani CHADEMA imepata wabunge wa kuchaguliwa na viti maalum wapatao 70 ambalo ni ongezeko la wabunge 22 tu kutoka wabunge 48 waliowapata mwaka 2010. Hivyo basi CHADEMA kwa kumsimamisha Lowassa mwaka 2015 kama mgombea wake kimepata wabunge wachache ukilinganisha na wabunge waliowapata mwaka 2010 kwa kumsimamisha Dk. Slaa kama mgombea wake bila ya kuungwa mkono na chama chochote.

kumbe kuwamjinga cyo kazi ...huyo dk.slaa wako kaifanyia nn chadema wakati kipindi yupo kambi ya upinzani walikuwa wabunge 48 ....wakati Leo hii lowasa kaipa chadema wabunge 39 kutoka 25 ,cuf 22 kutoka 10 na na vyama vingine pia kufikia wabunge 74...wakati viti maaluma CCM 66,cuf 10 na chadema 36 .......harafu ww unaropokaropoka tu na utakubali wakati huo soda imepanda bei.......
...
 
Unapowashindanisha EL na Dr. Mihogo katika kuongeza kura na viti vya ubunge CHADEMA, ujue automatically kwa upande wa pili unawashindanisha JK na JPM katika kupoteza kura na viti vya ubunge. Kwa hiyo tungependa tuone pia thread za nani mkali wa kupoteza kura na viti kwa wapinzani kati ya JK na JPM.
 
Back
Top Bottom