Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi La kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, amewataka Waislamu nchini kushirikiana ili kujenga umoja thabiti kwa ajili ya kushughulikia masuala mbalimbali yanayohusu dini yao.
Dk. Mwinyi amewataka pia wanazuoni wa Kiislamu kufanya utafiti zaidi kwa lengo la kuusaidia Uislamu kusimama katika misingi yake kama ilivyokusudiwa na Mwenyezi Mungu.
Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Peacock Hotel, wakati akizindua kitabu chenye maudhui ya mwezi upi sahihi wa kitaifa au wa kimataifa kilichoandikwa na Profesa, Juma Mikidadi, ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kiislamu mkoani Morogoro (MUM).
Katika uzinduzi huo ulioratibiwa na Taasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania, Dk. Mwinyi, alisema suala la muandamo wa mwezi limekuwa likiwagawa Waislamu pasipo sababu za msingi hali inayosababisha umoja baina yao kutokuwepo.
Hili la mwezi tumekuwa tukitofautiana kwa muda mrefu, na sasa kuna hiki kitabu tunashukuru kitatoa mwanga kwetu kwa kuwa nina hakika mwandishi amefanya tafiti za kutosha hata akaamua kuja na hoja hii, alisema Waziri Mwinyi.
Alisema kutofautiana kusiwe sababu ya kugombana hivyo watumie nafasi hiyo ya kutofautiana kufahamishana zaidi juu ya maagizo ya Mwenyezi Mungu.
Huku akinukuu baadhi ya aya za Mwenyezi Mungu zinazohimiza kushirikiana Dk. Mwinyi alisema pamoja na mambo mengine kuna haja ya kuwakutanisha Waislamu na kuweka umoja wao.
Awali akizungumzia kuhusu kitabu hicho, Profesa Juma Mikidadi, alisema ni aibu kwa Waislamu kuitana majina mabaya kwa sababu ya kuhitilafiana katika kufunga na kufungua jambo ambalo alisema linawezekana likaongelewa na kupata muafaka wa kitu cha kufanya kwa ajili ya Waislamu.
Alisema ni jambo la kushangaza kuona Waislamu wakifikiria kutengana katika suala hilo wakati dunia inahimiza kuunganisha nguvu.
Source: http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=32711
Dk. Mwinyi amewataka pia wanazuoni wa Kiislamu kufanya utafiti zaidi kwa lengo la kuusaidia Uislamu kusimama katika misingi yake kama ilivyokusudiwa na Mwenyezi Mungu.
Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Peacock Hotel, wakati akizindua kitabu chenye maudhui ya mwezi upi sahihi wa kitaifa au wa kimataifa kilichoandikwa na Profesa, Juma Mikidadi, ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kiislamu mkoani Morogoro (MUM).
Katika uzinduzi huo ulioratibiwa na Taasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania, Dk. Mwinyi, alisema suala la muandamo wa mwezi limekuwa likiwagawa Waislamu pasipo sababu za msingi hali inayosababisha umoja baina yao kutokuwepo.
Hili la mwezi tumekuwa tukitofautiana kwa muda mrefu, na sasa kuna hiki kitabu tunashukuru kitatoa mwanga kwetu kwa kuwa nina hakika mwandishi amefanya tafiti za kutosha hata akaamua kuja na hoja hii, alisema Waziri Mwinyi.
Alisema kutofautiana kusiwe sababu ya kugombana hivyo watumie nafasi hiyo ya kutofautiana kufahamishana zaidi juu ya maagizo ya Mwenyezi Mungu.
Huku akinukuu baadhi ya aya za Mwenyezi Mungu zinazohimiza kushirikiana Dk. Mwinyi alisema pamoja na mambo mengine kuna haja ya kuwakutanisha Waislamu na kuweka umoja wao.
Awali akizungumzia kuhusu kitabu hicho, Profesa Juma Mikidadi, alisema ni aibu kwa Waislamu kuitana majina mabaya kwa sababu ya kuhitilafiana katika kufunga na kufungua jambo ambalo alisema linawezekana likaongelewa na kupata muafaka wa kitu cha kufanya kwa ajili ya Waislamu.
Alisema ni jambo la kushangaza kuona Waislamu wakifikiria kutengana katika suala hilo wakati dunia inahimiza kuunganisha nguvu.
Source: http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=32711