Dk. Mwele Ntuli Malecela ametoa somo kubwa kwenye vyombo vya usalama

Ni kweli tafiti husomwa na mtafititi, lkn kwa ugonjwa kama ZIKA ilikuwa lazima uwasiliane kwanza na uongozi wa juu yako(wizara). Iko hivi, kwa wataalam wa Maabara kama anampima mtu HIV huwezi ukatoa majibu kirahisi kama ya mgonjwa wa malaria, lazima ujiridhishe kwanza(utapima kwa vipimo zaidi ya kimoja kama unavyo),pia kama mko wawili utamshirikisha na mtaalam mwenzio naye ajaribu kupima kama majibu yatalingana, majibu yakiwapa matokeo Sawa sasa process ya kumpatia mgonjwa majibu hufuata kwa utaratibu. Sasa huyu mama kweli watalamu wake walifanya utafiti wakagundua kuna virus vya ZIKA ilitakiwa kwanza awasiliane na wizara ikiwezekana sample walizotumia zipelekwe hata kwenye Maabara zingne hata nje ya nchi kwa utambuzi zaidi, baada ya hapo ndio majibu yakilingana na ya kwake sasa watatangaza, sasa yeye kapita shortcut. ZIKA ni ugonjwa mkubwa sana kuuchukulia kama vile ni malaria utaleta tahaaruki.
 
fa840e62be0ccfb865b6d468c404f79f.jpg
ati walikua na ummy?
 
Kama china ananyongwa,hapa apewe kesi ya kuhujumu uchumi

Unajua hata maana neno kuhujumu uchumi?, halafu jifanye mwanasheria mkuu wa serikali au wakili halafu uframu shtaka dhidi yake tuone utaiwekaje. Wewe ni mjinga kama wa kwenu kwani hata kama zika lipo tz sisi ndiyo kwa kwanza kuwa nao au hata kama atashtakiwa ndiyo itaondoa zika tz? acheni ufala wa kuficha ukweli. Tafiti hupingwa kwa tafiti nyangumi wewe
 
Ukipewa kipimo kipya kuyapima hayo matende na manazi na maboga ili kuangalia ubora wake, utatangazaje matokeo ya ubora wa kipimo hicho kipya?
utapeleka taarifa kwa waliokupa hivyo vipimo matokeo ya utafiti wako.. sharia ndo inavyosema mkuu......
 
Kwa nini mtu unakimbilia kwenye media kutangaza magonjwa ambayo hawana ushahidi wa waathirika. Hivi Kuna cases za microcephaly kwa watoto wanaozaliwa ambazo ziliwasukuma kwenda kufanya utafiti huo? Na kama hakuna waathirika kwa nini wasifanye utafiti Zaidi hata kulinganisha vinasaba, phylogenetic na vile vya brazil na kuangalia mambo mengine kama population immunity. Nafikiri siyo kitu cha kujivunia kutangazia ulimwengu kwamba una kila aina ya magonjwa, wenye nia mbaya wanaweza wakatumia kama nafasi ya kuleta strains zao na kuzipandikiza halafu ndo tutaanza kutafutana hapa.
 
Kwa akili yako unafikili ZIKA ni malaria kwamba kila mtu atatangaza tu, huyo mama alikosea nakulikuwa na umuhimu wakujiridhisha na kushirikisha wizara husika ,angalia impact ya ZIKA wakati Brazil ilipokuwa inaandaa michuano ya Olyimpic najitihada walizotumia katika kuzima vyombo vya habari, maana ilitishia hata kunyang'anywa nafasi ya kuaandaa hiyo michuano
Mkuu kwa akili yako unawaza maslahi ya kiuchumi kulioo uhai wa watu.kwangu aliyetangaza ni mtu sahihi kuliko mwanasiasa muongo aje atangaze baada ya kumeza desa aweke na chumnvi.hivi hujui watu wanalipishwa gharama kibao mahospitalini na dawa hakuna.serikali inadai zipo? umesahau makamu wa Rais alisema dawa hakuna huku waziri wa afya kasema zipo?
 
Hii nchi ya ajabu sana yaani mtihani nimefanya mimi ,matokeo asome MTU mwingine.kupitia suala hili tutagundua madudu mengi sana ndani ya serikali inayojinasibishaI busha kuwa no serikali tukufu isiyohitaji kukosolewa.Tafiti za wasomi hazipaswi kuaminiwa kwa kuwa kumbe hadi zikaguliwe na usalama ndiyo zitoke.
 
Kweli na wapunguze kutoa matamko.heh basi wafanye mwisho wa mwezi kila mwenye tamko lake ndo aseme.heh kila ukiamka tamko,ukilala tamko.bora hata hayo matamko yangekuwa yakujenga yote tuu ya kutahamakisha watu
 
Dr. Mwele in shujaa ambaye alitaka kutumia taaluma yake kwa ufanisi na uwazi sio kwa kufuata maelekezo ya wakubwa. Serikali iuanbie ukweli umma wa watanzania je zika ipo au hakuna kwa ushahidi kama alivyosema Dr. Mwele kuwa kuna watu walipimwa.
 
Mwele mkweli ila nyie waficha ukweli ndio mtaisababishia nchi madhara kumtukana na kumkashifu hakutaisaidia nchi tunataka ukweli sio Kongo longo
 
Mimi nasema mficha ugonjwa ujue mauti yanamwita ila ipo Siku ukweli utajulikana nani mkweli na nano sio mkweli tusiingize siasa ktk uhai wa watanzania
 
Pamoja na kwamba siishabikii sana hii govt ya JPM lakini huyu dr Mwele kakosea sana tu yaani ametaka kuiingiza nchi kwenye janga ambalo kutoka ingeligharimu hii nchi miaka kibao.. kakosea sana na kuwajibishwa ilikua ni muhimu sana yaani ameropoka kama baba yake alivyowahi fanya alipokua waziri wa mawasiliano na uchukuzi kuwaambia wasafiri waende kuzimu, Baba wa Taifa hakumkawiza alimpiga ban mbaya hadi leo anauota urais wa Tz. Kuroporopoka katika kazi kwa masuala ya kitaifa ni utovu wa nidhamu kwa hio alichokipata anastahili 100%.
 
CV si utendaji, kumbuka hilo.

Itakuwa shule alienda kusomea ujinga.
Nakubaliana na wewe la kwamba CV si utendaji, lakini sikubaliani na wewe kwamba "uboya" wa Dk Mwele umethibitishwa tu na tukio la juzi, angalau tuwekee mifano zaidi ya kututhibitishia huo "uboya" maana wengine tunamwona kama mwanamke msomi aliyefanya kazi nzuri kiasi cha kutambulika na taasisi za nje ambazo ni nadra kusikia zikifanya shughuli zake kwa figisu figisu badala ya kujali uwezo wa kitaaluma.
 
Watu wa aina ya Malecela wanaitwa PROFESSIONAL ECONOMIC HITMAN.Hawa hutumia taaluma zao kuubamiza uchumi chini KWA SIRI na kustukiza.Anatoa news alert ya dakika inauulilia mbali uchumi kwa dakika.Matamko yote mazito inabidi yapitiwe na wizara husika na wizara ya ulinzi.

Nashauri hata kesi kubwa kubwa za uhujumu uchumi si vibaya hukumu zikapitiwa na wizara ya sheria na wizara ya ulinzi kabla ya kusomwa
Sasa uhuru wa mahakama utakuwa wapi kweli Tanzania tuna vilaza wengi
 
Nashauri hata kesi kubwa kubwa za uhujumu uchumi si vibaya hukumu zikapitiwa na wizara ya sheria na wizara ya ulinzi kabla ya kusomwa

Mwaka arobaini na Saba!
Je wakati taasisi inafanya utafiti je pesa za kufanya kazi hiyo imetoka wapi?
Nani kaidhinisha pesa hizo?
Mfumo wa ufuatiliaji kupitia Wizara ukoje? nk. Yako mengi ya kuhoji Yes
 
Kwangu Dr Mwele atabakia kuwa SHUJAA siku zote.

Report ya utafiti hutolewa na aliefanya utafiti..

Na siku zote tafiti zinazofanywa kuhusisha jamii ni Mali ya Jamii husika.

Report hii Dr Mwele angewapa serikali mpaka sasa ungekuta serikali ipo kimya na haijawaeleza lolote jamii ya Watanzania.

Hata kama taratibu/protocol inasema alipaswa kuwapa wizara utafiti then waziri ndio atangaze hizi ni protocol za KIJINGA na ambazo haziwezi kutusaidia chochote.

Tusiangalie tu maslahi sijui uchumi utashuka.. Sijui watalii hawatakuja..
Those are cheap arguments..

Uhai ni muhimu kuliko watalii waje waambukizwe ZIKA hapa.

Big up Dr Mwele...
Mungu anakwenda kukufungulia mlango mwingine mzuri zaidi na watawala hawa hawa watakukumbuka.
Hata kama ni protocal mbovu kiasi gani kama aliapa kuzitimiza na kuzilinda ukizikiuka ni kosa lazima upewe adhabu hata wachawi wanapeana adhabu wakikiuka maazimio yao kwa maana hiyo Dr Mwele ni Mtovu wa nidhamu dhidi ya serikali aliyokubali kuitumikia hana ushujaa wowote angekuwa shujaa kama angejiuzulu kwanza kisha kutoa sab ya kujiuzulu kwake. Kukiuka taratibu ulizoaidi kwa kiapo kuzitumikia hata kama ni za kijinga kiasi gani halafu unazikiuka hadharani makusudi huo ni ujuha wa kiwango cha lami.
 
Watu wa aina ya Malecela wanaitwa PROFESSIONAL ECONOMIC HITMAN.Hawa hutumia taaluma zao kuubamiza uchumi chini KWA SIRI na kustukiza.Anatoa news alert ya dakika inauulilia mbali uchumi kwa dakika.Matamko yote mazito inabidi yapitiwe na wizara husika na wizara ya ulinzi.

Nashauri hata kesi kubwa kubwa za uhujumu uchumi si vibaya hukumu zikapitiwa na wizara ya sheria na wizara ya ulinzi kabla ya kusomwa
Mbona jokolilo anaua uchumi wa nchi tena mchana kweupe na hausemi kitu? Hebu fikiria kidg kabla ya kuongea
 
Back
Top Bottom