Dk. Mwakyembe mambo mazito: Ripoti ya ugonjwa wake yaivuruga Serikali: Pinda

mimi kwa mawazo yangu huyu mama ataungwa mkono na watu wote kwani ana upeo na kipaji cha kuzaliwa, hayupo kwenye siasa za sana na vilevile atakuwepo kwa muda wote wa kamati kwani bado sio mzee na hii kamati inaweza kuchukua muda sana. Cha maana zaidi ni mwanasheria ambaye amesomea katiba na anajua katiba za nchi nyingine kwasababu ametoka un.

ebu kuwa mkweli na hakika na unachoandika. Kwamba ana kipaji cha kuzaliwa kwenye nini? Kwenye siasa si alipewa upendeleo kupitia viti maalumu vya vyuo vikuu? Toka lini amewahi kufanya siasa na kuonekana anaweza? Kuwa mwalimu chuo kikuu siyo kigezo bwana, kwani dr. Bana si senior lecturer udsm? Au prof. Mukandara si ni profesor? Je nini kinaendelea sasa pale udsm na serikali yetu wanayoishauri kupitia nafasi zao redet na kama washauri wa rais? Wewe hauoni kama nchi inamwelemea rais wetu kwa ushauri anaoupata toka kwa watu hao?

Kama ana uwezo na kipaji kikubwa, ni nini kimemshinda un? Je kasi ilikuwa kubwa sana? Kiasi kwamba kwake imekuwa vigumu kuendana nayo? Usilete hoja kwamba un kaacha yeye, hizo ni dhana za kuleta kupoteza hasa kilichotokea un kwa huyo mama. Mama aliomba lkn imeonekana hakuwepo kwenye lon-term plan ya utendaji wa katibu mkuu wa un. Isitoshe hiyo nafasi alipewa kama zawadi tu.

Kama hoja ni kufundisha sheria chuo kikuu hiyo isiwe dhana kwani walimu wako wengi sana na haimaanishi kwamba wote wana vipaji vya hali ya juu ndugu yangu. Wengine ni msuli sana tu ndiyo waweze kuperform, kwani iq zao si kubwa kiivyo. Na wote wakishabaki pale, inakuwa ni vigumu kutambua yupi ni mkali zaidi kuliko mwingine.

Sasa narudi kwenye point; kwenye kamati ya katiba hatuhitaji mtu anayekuja kujifunza siasa na utendaji kwenye public ambaye hana kasi itakayotusaidia sisi watanzania. Kumbuka, watanzania tunahitaji mtu mwenye uwezo mkubwa wa kufikiri na kasi ya ajabu kuliko hata ya un, kwani kwasasa tz ina hali mbaya sana kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hivyo, kama ameshindwa kasi ya un, then hata tz hatuhitaji mtu kama huyo.
 
Amefanya nini huko UN, ama amewahi kufanya nini ? Nafikiri tuwe na tabia ya kupima viongozi nini wamefanya kutokana na nafasi zao zilizopita/wanazo.

Tusiwape kwa umaarufu/ngekewa zao za kupendwa.
 
Amefanya nini huko UN, ama amewahi kufanya nini ? Nafikiri tuwe na tabia ya kupima viongozi nini wamefanya kutokana na nafasi zao zilizopita/wanazo.

Tusiwape kwa umaarufu/ngekewa zao za kupendwa.

Hakufanya kitu alikuwa anakaa tu na kulipwa bure, ndio maana wakamchagua MkamaP afanye kazi badala yake lol..wabunge kwa wivu ..
 
Mimi sijasema awe pekee lakini awe mojawapo wa wanakamati. Mimi kwa upande wangu nimesoma speech zake akiwa UN na kuangalia video pamoja na kusoma CV kwa mawazo yangu naona anafaa kuwa member. Dr Slaa naye anafaa lakini ningependa watu ambao hawako kwenye siasa kwa sasa.
 
Mimi nafikiri apewe padri Slaa; amelilia sana hiyo nafasi halafu katibu wake awe Pengo..tunawaamini sana.

kuna watu hawastahili kuwepo kwenye hili jukwaa maana uwezo wao wa kufikiri ni chini ya viwango vya JF unaacha kuchangia hoja iliyo mezani unakimbilia udini?? Tanzania we have an uphill task!!
 
Mimi kwa mawazo yangu huyu mama ataungwa mkono na watu wote kwani ana upeo na kipaji cha kuzaliwa, hayupo kwenye siasa za sana na vilevile atakuwepo kwa muda wote wa kamati kwani bado sio mzee na hii kamati inaweza kuchukua muda sana. Cha maana zaidi ni mwanasheria ambaye amesomea katiba na anajua katiba za nchi nyingine kwasababu ametoka UN.

Hivi kuna correlation ya kuwa naibu katibu mkuu UN na kujua katiba za nchi zote? Mbona mimi nikiamua nitajua za vyama vyote vya siasa duniani, je tafaa kuwa mwenyekiti wa tume ya wananchi (sio ya Rais) ya kuandika katiba mpya? Hivi hiyo position ya UN haina renewal kama ya katibu mkuu?
 
HATIMAYE Naibu Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa KyeLa, Dk Harrison Mwakyembe amejitokeza na kutoa kauli nzito kuhusu chanzo cha maradhi yanayomsibu, huku Serikali ikiendelea kukaa kimya hata baada ya washirika wake wa karibu kusisitiza kwamba alipewa sumu.

Itakumbukwa kwamba, Desemba 10 mwaka jana, Dk Mwakyembe akiwa na hali mbaya alipelekwa katika Hospitali ya Appolo, nchini India kwa matibabu baada ya kuugua maradhi yaliyosababisha ngozi yake kuharibika. Tangu arejee mwanzoni mwa mwezi uliopita alikuwa hajaonekana hadharani, mbali na kutoa tamko kwamba afya yake ilikuwa inaendelea vizuri.

Hata hivyo, muda wote huo aliokuwa nchini India na baada ya kurudi nchini, mazungumzo ya watu maofisini, nyumbani, mitaani na vijiweni yalitawaliwa na utata wa suala la afya ya Dk Mwakyembe, huku uvumi, tetesi na minong’ono kwamba maradhi yake yalisababishwa na hujuma za kisiasa vikitawala hisia za wananchi. Hisia hizo zilikuzwa na kauli ya mmoja wa washirika wake kisiasa, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta ambaye alimtembelea hospitalini nchini India na baadaye kukiambia kituo kimoja cha televisheni hapa nchini kwamba Dk Mwakyembe alikuwa amelishwa sumu kutokana na msimamo wake dhidi ya mafisadi.

Akizungumza huku akionyesha kujiamini, Waziri Sitta alisema muda wote aliokaa na naibu waziri huyo katika Hospitali ya Appolo alipata ushahidi wa kutosha kwamba maradhi yake ya kuharibika kwa ngozi ya mwili wake yalisababishwa na kulishwa sumu, huku ushuhuda wake ukiacha kitendawili cha nani hasa waliohusika na uhalifu huo pasipo kuteguliwa. Hata hivyo, kauli hiyo ya Waziri Sitta iliwaudhi viongozi wengi serikalini na katika chama chake cha CCM ambao walimtaka athibitishe tuhuma kwamba hujuma kwa Dk Mwakyembe ilikuwa ni kazi ya mafisadi.

Lakini jambo la kushangaza ni kwamba muda wote huo Serikali ilikataa kutoa tamko siyo tu kuhusu maradhi yanayomsumbua kiongozi huyo, bali pia kama ilikuwa imefanya upelelezi kuhusu kuwapo au kutokuwapo watuhumiwa wowote ambao walikuwa wanahusishwa na hujuma hiyo. Wananchi walishangazwa na hatua ya Serikali kuendelea kukaa kimya na kupiga danadana suala hilo, huku viongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani na Wizara ya Afya wakitupiana mpira.

Tunashangazwa na ukimya huu wa Serikali hata baada ya kupata ripoti ya madaktari wa Hospitali ya Appolo ambao walimtibu Dk Mwakyembe. Haki ya wananchi kujua maradhi yanayomsibu inapewa uzito na ukweli kwamba yeye siyo tu mbunge wa kuchaguliwa na wananchi, bali pia ni naibu waziri katika Serikali ya Awamu ya Nne. Tukitilia maanani kwamba gharama kubwa za matibabu yake zimelipwa kwa kodi za wananchi, ndipo tunaposhangaa kwa nini Serikali haioni uhalali wa wananchi kujua hali ya afya za viongozi wao kwa madai kwamba masuala ya afya zao ni masuala binafsi.

Alipojitokeza hadharani mwishoni mwa wiki akiwa na washirika wake wa kisiasa katika uzinduzi wa programu ya moja ya madhehebu ya Kikristo jijini Dar es Salaam, Dk Mwakyembe aliwaeleza waumini jinsi maradhi yake ilikuwa kazi ya mafisadi ambao walimsababishia mateso makubwa na kuahidi kuzungumzia suala hilo kwa undani katika siku za usoni, huku Waziri Samwel Sitta akisimama na kuwaeleza waumini kwamba Dk Mwakyembe alilishwa sumu.

Sisi tunadhani ukimya huu wa Serikali umeiletea aibu kubwa na kuibua hisia kwamba, pengine nayo ni sehemu ya tatizo. Vinginevyo haiingii akilini jinsi Serikali siyo tu inavyoweza kupata ujasiri wa kuficha ripoti iliyotolewa na Hospitali ya Appolo, bali pia kushindwa angalao kutoa tamko kama Dk Mwakyembe alilishwa sumu au la.

Kwa kuwa Dk Mwakyembe anajua fika nini kilichomo katika ripoti iliyotolewa na hospitali hiyo ya nchini India, tunamshauri ajitokeze hadharani awaeleze wananchi ukweli kwa lengo la kumaliza uvumi, tetesi na minong’ono kuhusu maradhi yanayomsibu.


 
Mimi kwa mawazo yangu huyu mama ataungwa mkono na watu wote kwani ana upeo na kipaji cha kuzaliwa, hayupo kwenye siasa za sana na vilevile atakuwepo kwa muda wote wa kamati kwani bado sio mzee na hii kamati inaweza kuchukua muda sana. Cha maana zaidi ni mwanasheria ambaye amesomea katiba na anajua katiba za nchi nyingine kwasababu ametoka UN.

Hivi nyie watu wa Chama cha Magamba mnadanganyana kuwa kwa vile Migiro aliteuliwa kwenda UN kama msaidizi wa Katibu Mkuu basi mnaona ana upeo kihivyo? You must wasting your time.

Watu tunajua aliteuliwa kwenda UN kwa recommendations za Jk kwa vile alikuwa mshikaji wake na bado ni mshikaji wake. Tatizo la Chama cha Mafisadi a.k.a Magamba mna tabia za kuwaamini sana Wanawake. Tumeshayaona ya Kigagula Anne Mikanda kwa kupewa Kiti cha Usupuka ili kuongoza Bunge la MBU+NGE=MBUNGE(CCM).
 
Hivi kilichomwondoa kwenye nafasi yake UN kumrudisha nyumbani ni nini? Japo kumekuwa na siasa nyingi kwenye hili lakini kiuhakika ame-underperform! Hata tangu mwanzo alipopewa hiyo nafasi ilikuwa kisiasa zaidi badala ya uwezo. Hapa hakuna cha jinsia wala nini, pamoja na u-profesa alio nao huyu mama siyo competent ila kama tunataka kurudia makosa kama ya akina madame Speaker, tunaweza kufanya hivyo.

Kama tunadhani walioshindwa ku-perform UN hapa nyumbani ni lulu bado tunaweza kufanya hivyo lakini matokeo yake yataonekana huko mbeleni. Tukitaka tuchezee mambo mengine yote lakini sio "roho" ya taifa - KATIBA.
 
Waliomuwekea sumu dr mwakyembe sio kikwete lowasa na rostam bali ni sisi watz wote. Sijawahi kuona linchi la ajabu km tz na mijitu ya ajabu km mitanzani. Mnatajiwa kabisa wezi wa mali zenu alafu mnakaa kimya eti mwakyembe angewakamata kabisa wahusika,kweli? Hii ingekuwa nchi yenye watu wenye akili timamu wangeshukuru ripot ya dr. Na kukatisha ajira za wote waliotajwa. Mbaya zaidi mpaka rais katajwa na mwenzake kuhusika kwa kina bado mitz imelala usingizi wa pono eti inataka dr. Amkamate na kumfung
 
Waliomuwekea sumu dr mwakyembe sio kikwete lowasa na rostam bali ni sisi watz wote. Sijawahi kuona linchi la ajabu km tz na mijitu ya ajabu km mitanzani. Mnatajiwa kabisa wezi wa mali zenu alafu mnakaa kimya eti mwakyembe angewakamata kabisa wahusika,kweli? Hii ingekuwa nchi yenye watu wenye akili timamu wangeshukuru ripot ya dr. Na kukatisha ajira za wote waliotajwa. Mbaya zaidi mpaka rais katajwa na mwenzake kuhusika kwa kina bado mitz imelala usingizi wa pono eti inataka dr. Amkamate na kumfung

wat measures have you taken wewe kama wewe apart from being a complainant?! It begins with you!
 
Ni Tanzania hii hii?Haya wacha tusubiri kama tunavyomsubiri yesu ashuke kwa mara ya pili

Naitamani hii siku, naamini tu itakuja............MUngu atupendaye hawezi kutuachia mateso milele..tutazidi kumwomba na iko siku atajibu maombi yetu!
 
Polisi wetu wanatia aibu kwa kushindwa kutimiza wajibu. Polisi wa Tanzania ndio wauaji wakubwa, ndio majambazi wenyewe na ndio wala rushwa.
Heri jeshi letu la polisi livunjwe kwani ni aibu kubwa kwa nchi yetu, idara nyeti kama ya polisi kuongozwa kwa utashi wa kisiasa
 
Una chuki sana wewe hata hivyo hui. Ukombozi fake unaotafuta utasubiri sana pole sana
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom