kisugujira
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 774
- 196
Jamani viongozi wetu jaribuni kufunguka kwa kuwa wakweli na wawazi! Kama kweli mtu unamjua mbaya wako aliyetaka kukuua na ushahidi upo kwa nini unaogopa kumsema au kumtaja ili achukuliwe hatua? Au nanyi mnataka kulipiza visasi kimya kimya?
Dr. Mwakyembe na Dr. Ulimboka wanatakiwa kuuambia umma wa watanzania nini kilichowasibu. Kukaa kwao kimya bila kusema kitu cha kuwapa imani wananchi kunasababisha watu kusema mambo mengi hata wakati mwinginie kutukana kama walivyofanya wachangiaji wengine katika thread hii.
Kwa nini mnakaa kimya mmefungwa midomo msiseme mmepewa nini? Kumbukeni sala za watu kwenu kwa yaliyowapata, michango (hata kama pesa zilitoka serikalini ni mali ya watanzania), upendo na uzalendo wao kwenu. Mnataka waseme au wafanye nini ili mujue hawayapendi mambo yaliyowasibu?
Dr Ulimboka ndio kawa kimya kabisa! Hasikiki kanisani wala kwenye vikao vya moja moto, moja baridi na nyama choma. Vitabu Vitakatifu vinatuambia tusiseme uongo. FUNGUKENI.
Dr. Mwakyembe na Dr. Ulimboka wanatakiwa kuuambia umma wa watanzania nini kilichowasibu. Kukaa kwao kimya bila kusema kitu cha kuwapa imani wananchi kunasababisha watu kusema mambo mengi hata wakati mwinginie kutukana kama walivyofanya wachangiaji wengine katika thread hii.
Kwa nini mnakaa kimya mmefungwa midomo msiseme mmepewa nini? Kumbukeni sala za watu kwenu kwa yaliyowapata, michango (hata kama pesa zilitoka serikalini ni mali ya watanzania), upendo na uzalendo wao kwenu. Mnataka waseme au wafanye nini ili mujue hawayapendi mambo yaliyowasibu?
Dr Ulimboka ndio kawa kimya kabisa! Hasikiki kanisani wala kwenye vikao vya moja moto, moja baridi na nyama choma. Vitabu Vitakatifu vinatuambia tusiseme uongo. FUNGUKENI.