Dk. Mwakyembe awapa polisi siku 14 kuwataja polisi wezi wa mafuta

Kwanini polisi huwa hawachukui hatua? Na kwanini asiwataje hao ambao wamekuwa wakitaka kuuondoa uhai wake?:llama::msela:
 
Jamaa anafaa, apewe muda kidogo. Maana sasa bandari panazidi kunyooka. mapato yaliyo kuwa yanapatikana kwa wiki sasa ni siku tatu tu. Tumpe support stahili. Ni viongozi wachache waliopo ktk serikali hii. Safi Mwakyembe.
 
Akili ni nywele! Dr. Mwakyembe alikuwa na nywele, baada ya maradhi, hana tena nywele.
Yeye ni Waziri, Kova ni mtu mdogo sana kwake, ilikuwa ni kumlima barua ya kujieleza kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake
 
Aaache unafiki kama anawajua kwanini asiwataje, ili tuwajue na hapo ndipo tutaanza kukomaa na mwema kama hatowachukulia hatua, kwani kwa ilivyo hivi sasa Mwema au Kova ( maana ndio aliowataja) wakisema hatua za uchunguzi bado zinaendelea na zikikamilika watafikishwa mahakamani ataridhika?
 
Alisema kuwa baada ya kutoka India matibabu angeyasema ya moyoni ikiwa ni pamoja na kuwataja walohusika hadi leo yuko India? Kwanini hakutoa siku moja kwa vile wahusika wanajulikana? Danganya toto tu hii. Na kwa ufupi hii movie imekwisha kama nyingine zinavyopita!!!!
 
Ok am counting for Kova to react

Umetendewa yooote hayo bado umo tu???

Kweli haya maneno yanaring kichwani

'Your JOB will not take care of you when you are SICK, your family will.'
 
Mh mwakyembe amesema kama mh igp mwema na kova amtowataja hadharani wahusika wa wizi wa mafuta bandarini na kuwashugulikia basi kazi hiyo nitaifanya baada ya wiki mbili na kuweka hadharani
siwezi kuona wezi wahalifu na ni polisi wa kulinda raia leo wanakumbatiwa kama watoto wa changa alilalama mh mwakyembe...


Ndugu zanguni nawambia sipepesi macho wala kumumunya mdomo nimewapa igp wiki mbilia ama awataje hadharani na kusema wamechukua hatua gani kama wataendelea kuwakumbatia kama wauwaji wengine wa mikoani basi mimi nitakuwa wa kwanza kuwataja na siogopi kufa walitaka kuniua siku nyingi mungu akanipitisha kwenye moto wa daniiel..sasa basi naawaambieni ujing mliokuwa mkifanya zamani sasa basi tunataka kazi kama mmeiba amjafanikiwa sahauni kuiba tena ...nitapiga kazi nitakaa na wale wanaotaka kufanya kazi tu alisema hon mwakyembe
hapo kwenye blue yaonye serikari(mwakyembe kama waziri) inatambua kuna mauji na watekelezaji wa mauaji hayo pia wanafahamika ila wanabebwa kuficha ushiriki wa serikali,na hapo mwakyembe ametoa siri.
 
Mr. President Umenena vyema mkuu, kama ushahidi wote anao, mbona haendi mahakamani?
Kulalamika leo kunasaidia nn?
Huo ndio unafiki,
kama alihongwa uwaziri akaamua kunyamaza angeendelea kupiga kimya tu, sio kubwabwaja kusiko saidia chochote.
 
Last edited by a moderator:
Dr, H.Mwakyembe hiyo ndiyo Serikali yako ya CCM ya maisha bora kwa kila Mtz wakisema akina Dr,W.P.Silaa kwamba serikali ni Mbovu inafanya maovu mengi sana kiasi wananchi tunaanza kuiogopa kwani hata mauuaji yanayojitokezza kwenye mikutano ya vyama vya upinzani kwa nini wananchi tusiwe na mashaka na serikali yetu kama kiongozi mwandamizi wa serikali hiyo anayaona anashindwa kuyasema???????? kibaya zaidi watu toka Mbeya au kusini mnaongoza kwa majaribio haya. tumeona kipigo cha Dr,Ulimboka kilivyoitikisa Tanzania na Dunia kwa ujumla??? Hivi Mwakyembe kutoa siku 14 kwa Polisi inamaana Waziri wa Mambo ya Ndani hayupo nchini na kama hayupo hakuna anayekaimu nafasi inaonyesha Serikali ya CCm ilivyo Dhaifu katika mambo ya Utawala.Ngojeni mnaodhani ni vipofu na hawana Elimu hawajui hata mnavyoneemeka siku wakipata ujasiri kila mtu ataumbuka mchana kweupe.
 
TATIZO KUBWA NI MWAKYEMBE MWENYEWE......
Habari ya Mwakyembe sitaki kusikiliza tena....
Nilitaka kuandika kama ulichoandika hapo kwenye rangi
KWA KUONGEZEA TU,MWAKYEMBE HUKUA NA 7BU YA KUONGELEA JIMBON KWAKO,UNGEMWANDIKIA BARUA BWANA AL-HAJI KOVA,
KWA SASA SITATILIA MAANANI CHOCHOTE UTAKACHOKIONGEA
 
Akili ni nywele! Dr. Mwakyembe alikuwa na nywele, baada ya maradhi, hana tena nywele.
Yeye ni Waziri, Kova ni mtu mdogo sana kwake, ilikuwa ni kumlima barua ya kujieleza kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake

aisee nami nimekoment hivo kwenye post ya mr president
 
kama anauwezo wa kuwaamuru polisi wataje wezi wa mafuta,anashindwa nini kuwaamuru wafanye uchunguzi kuhusu yeye kulishwa sumu.??
 
alililikologa la kutotaja mabaya zaidi ya richie wakamfuate alinywe akanusuriwa na Mungu kulinywa sasa watamwangosi live.
 
Hata mimi nimemshangaa sana kwanini Mwakyembe atoe agizo la kuwapa polisi wa kanda maalumu Dar es salaa siku 14 akiwa Kyela .Tumechoka na unafiki wake hilo swala alipaswa alisemee akiwa hukuhuku Dar es salaam.Aache kufanya kazi na magazeti kwani pamoja na matatizo yaliyoko bandari ya Dar es salaam na Kampuni ya Atcl mabadiliko aliyofanya hayajaleta tija huwezi kumwondoa meneja mkuu ukaacha bodi ya wakurugenzi kwani meneja mkuu anawajibika kwa bodi ya wakurugenzi hivyo kama meneja alifanya madudu na bodi ikakaa kimya ina maana bodi pia ni mbivu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom