Waziri wa Uchukuzi Dk. Mwakyembe ameliambia Bunge punde kuwa kulikuwa na dili la kujenga gati mpya bandarini Dar kwa dola milioni 523 lakini yeye alipoingia madarakani ameachana na mpango huo na kuzungumza na kampuni nyingine mahiri ya kigeni kujenga gati hilo hilo kwa dola milioni 160 tu! Je kuna dola milioni 363 zilipangwa kutafunwa na mafisadi? Wale wanaoitwa Takukuru wamesikia hilo???