Dk. Mtaki: Usagaji Ni Starehe Kama Zingine ; Asema Ikizidishwa Inaharibu Saikolojia Ya Mchezaji

PISTO LERO

JF-Expert Member
Mar 8, 2011
2,819
1,454
GUMZO juu ya wachezaji wa timu ya taifa ya wanawake ya Twiga Stars kufanya vitendo vya kustareheshana, limetetewa na baadhi ya wataalam kuwa ni tendo linaloweza kufanyika kama lilivyo tendo lingine.

Mjadala ulizuka wiki mbili zilizopita juu ya kufanya vibaya kwa Twiga Stars kwa kufungwa jumla ya mabao 3-1 na Ethiopia katika mechi za kuwania kucheza Fainali za Afrika zitakazofanyika Equatorial Guinea baadaye Novemba.

Mkwasa alisema kuwa kufanya vibaya kwa timu hiyo kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo kuendekeza vitendo vya kusagana, lakini akasema kuwa waliokuwa wakifanya 'hayo mambo' (bila kuwataja) walitimuliwa.

Lakini vitendo hivyo vimetajwa kushamiri hasa katika timu zinazojumuisha wanawake ama wasichana wengi kwani kila mmoja anakuwa na tabia na mihemko yake kiasi cha kuwaathiri wengine.

Spoti Mikiki ilifanya mahojiano na Dk. Magreth Mtaki, daktari wa michezo wa siku nyingi kutoka Kurugenzi ya Michezo ambaye anasema kuwa kusagana (lesbianism) ni kama starehe nyingine ambayo watu wa jinsi mbalimbali wanafanya.

Anasema kuwa tatizo linakuja kuwa ni suala linalohusisha wasichana ama kinamama ndiyo maana linaleta mshangao, lakini hakuna tofauti na matendo mengine ama kustareheshana kwa watu wawili.

Dk. Mtaki ambaye pia ni Makamu wa Chama cha Soka ya wanawake Tanzania, TWFA, anasema kuwa kitendo cha kusagana, kwa upande mwingine kina athari kubwa kwenye timu kwani endapo kitafanywa kwa kuzidisha, inamaliza nguvu mchezaji.

"Hata ingekuwa wewe na mke wako, una mechi ya kimataifa ama ligi, halafu ukafanya tendo la ndoa kupitiliza, ni wazi itapunguza uwezo wako uwanjani, basi hata hawa wanaosagana, wakizidisha, lazima uwezo utapungua.

"Kingine ambacho naweza kusema, lakini sasa hii ni kwa mchezaji mwenyewe...hali hii itamfanya hatokuwa na hamu ya mwanaume akiamini kuwa mwanamke mwenzake anakata kiu.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom