Dk. Kigwangalla achukua fomu kuwania uenyekiti wa Jumuiya wa Wazazi Taifa

Fred Katulanda

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
374
509
Leo taarifa nilizopokea zinadai kuwa Dk. Kigwangala ametinga katika ofisi za CCM mkoa wa Mwanza (Jumuiya ya Wazazi) na kuchukua fomu kuwania Uenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa, huku akidai anaamini kuwa CCM ni chama makini na kwamba bado hakijapoteza mvuto.
 
Vijana wanatakiwa wakamate CCM ili waje kukifufua maana CDM anatakiwa apate mpinzani wa kweli atakapokuwa madarakani, chama peeke cha upinzania na chenye nguvu kitakuwa ni ccm pekee
 
Si alishawahi kusema kuwa ndani ya CCM anachukiwa kwa kuwa anasimamia ukweli na anaupeo mkubwa hivyo siku zote anaepukwa kuchaguliwa.

Yetu macho na masikio tunasubiri kuona na kusikia ili siku akija hapa JF tumfariji au kumpa hongera.
 
Du huyu jamaa ana ngozi ngumu kaa ya kenge-yee kila uchaguzi yumo na hawamchagui!!
 
ndo anaelekea kupotea kuutete tu ubunge 2015 ni ndoto....nway siasa ni ulevi kama ile msg ya kushndwa pan africa haijamfikia atakuwa kashaanza kulewa
 
Leo taarifa nilizopokea zinadai kuwa Dk. Kigwangala ametinga katika ofisi za CCM mkoa wa Mwanza (Jumuiya ya Wazazi) na kuchukua fomu kuwania Uenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa, huku akidai anaamini kuwa CCM ni chama makini na kwamba bado hakijapoteza mvuto.
Anayo haki kugombea cheo chochote kwenye chama chake. Hata hivyo, hilo la umakini na kutokupoteza mvuto kwa chama chake labda anaweza kulipima kwa njia ya kukutana na wananchi kama CDM wanavyofanya through M4C. Vinginevyo asubiri kampeni zikianza Igunga ndipo ataujua ukweli.
 
Umuri wake anafaa kuongoza wazazi, anyway magamba mtajibeba!
 
Linaloniuma zaidi ni kuwa, hata yule ambaye nilidhani yuko makini kwasababu ya elimu yake bado anadanganyika na mfumo huu wa thithiemu kuwa wana mvuto!
 
Huyu daktari ni mpambanaji mzuri sana, tatizo kwa kuwa ndani ya lichama lililooza la ccm. Asipoangalia na akachukua hatua mapema, kutokana na misimamo yake watamuua na kumzika kisiasa mapema sana.
 
11.jpg
DK. Kigwangalla akichukua fomu leo ofisi za Jumuiya ta wazazi mkoa wa Mwanza, kugombea Uenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa.
 
Mwacheni atafute aibu nyingine ile ya ubunge wa EAC haikumtosha. Ni dalili ya kuwa na kimbelembele!
 
Back
Top Bottom