nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2][/h]JUMAPILI, SEPTEMBA 02, 2012 07:44 NA ABDALLAH AMIRI, IGUNGA
SIKU chache baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Tabora kutengua ubunge wa Mbunge wa Igunga, Dk Dalaly Kafumu, baadhi ya wananchi wamekumbwa na taharuki kutokana na ahadi kwa wakazi hao.
Wakizungumza na MTANZANIA, baadhi ya wananchi jimboni humo wamesema kabla ya kutenguliwa ubunge, Dk. Kafumu alikuwa amewaambia wananchi kuunda vikundi aweze kuwapatia mikopo kwa ajili ya biashara zao.
Wanasema waliitikia wito huo na walifungua akaunti zao katika tawi la NMB Igunga, lakini cha kushangaza baada ya hatuam hiyo, kesi ya kupinga ubunge ikiendelea, Dk. Kafumu aliwaomba wasubiri mikopo hiyo baada ya kesi hiyo.
Hata hivyo, baada ya kutenguliwa ubunge, Dk. Kafumu hakuweza kuonana na kikundi chochote, jambo ambalo wamesema wanahisi wametelekezwa.
Wanavikundi wamedai kitendo alichofanya Dk. Kafumu kimewavunja moyo kwa vile fedha walizofungulia akaunti walikuwa wamezikopa kwa imani ya kupewa mikopo ambayo ingewainua uchumi.
Naye Dk. Kafumu alikiri kuahidi mikopo kwa vikundi hivyo lakini akasema hawezi kuitoa kwa kuwa yeye si mbunge tena wa Igunga.
Siwezi tena kutoa mikopo kwa vikundi hivyo kwa sababu mimi si mbunge tena wa Igunga. Hata hivyo kuna baadhi ya vitu nilivyokuwa nimetoa katika jimbo hili vinatosha, siwezi kuongeza tena kitu chochote, alisema Dk Kafumu.
Mwezi uliopita, mahakama Kuu kanda ya Tabora ilimvua Ubunge Dk Kafumu kutokana ukiukwaji wa taratibu na sheria za uchaguzi zilizofanywa na baadhi ya viongozi waandamizi wa CCM na serikali
SIKU chache baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Tabora kutengua ubunge wa Mbunge wa Igunga, Dk Dalaly Kafumu, baadhi ya wananchi wamekumbwa na taharuki kutokana na ahadi kwa wakazi hao.
Wakizungumza na MTANZANIA, baadhi ya wananchi jimboni humo wamesema kabla ya kutenguliwa ubunge, Dk. Kafumu alikuwa amewaambia wananchi kuunda vikundi aweze kuwapatia mikopo kwa ajili ya biashara zao.
Wanasema waliitikia wito huo na walifungua akaunti zao katika tawi la NMB Igunga, lakini cha kushangaza baada ya hatuam hiyo, kesi ya kupinga ubunge ikiendelea, Dk. Kafumu aliwaomba wasubiri mikopo hiyo baada ya kesi hiyo.
Hata hivyo, baada ya kutenguliwa ubunge, Dk. Kafumu hakuweza kuonana na kikundi chochote, jambo ambalo wamesema wanahisi wametelekezwa.
Wanavikundi wamedai kitendo alichofanya Dk. Kafumu kimewavunja moyo kwa vile fedha walizofungulia akaunti walikuwa wamezikopa kwa imani ya kupewa mikopo ambayo ingewainua uchumi.
Naye Dk. Kafumu alikiri kuahidi mikopo kwa vikundi hivyo lakini akasema hawezi kuitoa kwa kuwa yeye si mbunge tena wa Igunga.
Siwezi tena kutoa mikopo kwa vikundi hivyo kwa sababu mimi si mbunge tena wa Igunga. Hata hivyo kuna baadhi ya vitu nilivyokuwa nimetoa katika jimbo hili vinatosha, siwezi kuongeza tena kitu chochote, alisema Dk Kafumu.
Mwezi uliopita, mahakama Kuu kanda ya Tabora ilimvua Ubunge Dk Kafumu kutokana ukiukwaji wa taratibu na sheria za uchaguzi zilizofanywa na baadhi ya viongozi waandamizi wa CCM na serikali