Mlachake
JF-Expert Member
- Oct 13, 2009
- 4,412
- 4,558
MJUMBE wa Kamati ya Kuratibu Kampeni za Urais za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Raphael Chegeni amelisakama gazeti hili akidai lina agenda ya siri ya kukihujumu chama hicho na kuipendelea Chadema.
Dk Chegeni alitoa malalamiko hayo jana kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya chama hicho,yaliopo Lumumba jijini Dar es Salaam.
Mjumbe huyo, alitoa lawama hizo baada ya gazeti hili toleo la Jumatatu wiki hii kumnukuu Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe kwamba Kampuni Binafsi ya Synovate imeficha taarifa ya utafiti inayoonyesha mgombea urais wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa anaongoza kwa kura za maoni.
"Sisi (CCM) tunasikitika sana kwa gazeti la Mwananchi kuandika habari hiyo tena ukurasa wa mbele na kupotosha Watanzania. Tunaamini Mwananchi wanalo lao jambo. Limeonyesha dalili za wazi za kupinga CCM na kuunga mkono chama cha Chadema," alisema.
Alipoulizwa iweje kulishutumu gazeti la Mwananchi wakati lilizingatia kanuni za uandishi wa habari wakati wa kuandika habari hiyo, kwa kutoa fursa kwa pande zote kutoa maelezo, ikiwemo Synovate, Dk Chegeni alizidi kusisitiza kwamba CCM haikutendewa haki kwenye taarifa hiyo.
Alisema kwamba pamoja na gazeti hilo, kuzingatia kanuni za uandishi wa habari, jinsi habari hiyo ilivyotoka ilionyesha kuikandamiza CCM na kuifagilia Chadema.
Dk Chegeni ambaye alikuwa mbunge wa Busega, lakini alishindwa kwenye kura za maoni na Dk Titus Kamani, alidai kwamba Synovate imeliamuru Mwananchi kukanusha na kuomba radhi kwenye ukurasa wa mbele na kwamba wao wanasisitiza hilo kama sehemu ya kuisafisha CCM mbele ya wananchi.
Mhariri Mtendaji wa Mwananchi Communications Ltd (MCL), Theophil Makunga alisema hajapokea barua yoyote kutoka Synovate kutaka taarifa iliyoandikwa na Mwananchi ikanushwe na kuomba radhi.
Kuhusu habari inayolalamikiwa na CCM, Makunga alisema gazeti la Mwananchi lilitimiza wajibu wa kuuhabarisha umma.
Alifafanua kwamba mwandishi wa mwananchi akaripoti taarifa hizo zilizotolewa na Mbowe kwenye kampeni kama ilivyo kwa vyama vingine ambavyo vinatoa taarifa zao kwenye kampeni.
Makunga alisema habari hiyo iliandikwa kwa kuzingatia kanuni za uandishi wa habari ikiwa ni pamoja na Synovate kupewa fursa ya kujibu shutuma walizoelekezewa.
Kuhusu tuhuma kwamba Mwananchi limekuwa liiandika vibaya CCM na kuipendelea Chadema, Makunga alisema hiyo siyo kweli kwa sababu ripoti ya Synovate inaonyesha ni gazeti hili linaandika bila upendeleo kwa asilimia 97.
"Yeye (Dk Chegeni) anatoa mawazo yake kama mkereketwa wa CCM, lakini ukweli ni kwamba utafiti wa kisayansi uliotolewa na Synovate unaonyesha sisi tuko neutral (bila upendeleo) kwa asilimia 97," alisema Makunga.
Kwenye mkutano na waandishi wa habari jana, CCM ilionyesha kukerwa na taarifa hiyo ya Mbowe na kuingilia kati kauli hiyo licha ya kwamba Synovate walikanusha na vyombo vya habari vikaiandika kwa kina jana.
"Tunamtaka Mbowe aache kuwapotosha watanzania," alisema DK Chegeni ambaye baada ya kushindwa katika kura za maoni za kuwania kuwa mgombea wa CCM, Busega, aliripotiwa kutishia kuhamia Chadema kwa kile kilichoelezwa kutokubaliana na matokeo hayo.
Alipouilizwa kama haoni kitendo cha kuendelea kuvitaka vyombo vya habari vikanushe taarifa hiyo ya Mbowe kwa mara nyingine ni kuonyesha mchecheto wa upinzani wanaoupata kutoka Chadema, Dk Chegeni alisema taarifa hiyo, iliandaliwa kwa makusudi ili kushawishi wananchi kwamba Dk Slaa anaongoza wakati si kweli.
Alisema kinachowauma zaidi ni kwamba Mbowe alitumia taasisi inayoheshimika nchini ya Synovate, kumuibulia umaarufu Dk Slaa jambo ambalo ni si kweli.
Maelezo hayo ya Dk Chegeni yamekuja siku moja baada ya Meneja wa Synovate (T), Aggrey Oriwo kukanusha kauli iliyotolewa Jumapili na Mbowe katika mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi mkuu kwamba Synovate imeogopa kutangaza matokeo kuhusu umaarufu wa wagombea yaliyoonyesha Dk Slaa anaongoza.
"Taarifa hizo ambazo pia zimeripotiwa katika baadhi ya magazeti si za kweli. Mimi kama msimamizi mkuu wa Synovate Tanzania nimekerwa sana na nimeandika malalamiko yangu kwa Baraza la Habari Tanzania (MCT), kulalamikia vyombo vilivyoripoti," alisema Oriwo.
Alisema Synovate ni kampuni huru inayofanya kazi zake kwa ukweli na uwazi bila ya kushawishiwa au kulazimishwa na mtu au taasisi yoyote ya kisiasa.
"Kauli ya Mbowe imetukera sana na …tunamtaka kama ana uhakika na ushahidi wa aliyosema, autoe hadharani kama sisi tulivyotoa matokeo hadharani," alisema Oriwo.
Alisema hawana cha kuficha na kwamba hawajatishwa wala kulazimishwa na chama au taasisi yoyote kuzuia matokeo ya utafiti.
"Ubora wa kazi zetu unakubalika kitaifa na kimataifa kwa sababu hatushabikii chama chochote cha siasa na ndio maana mwaka jana tulifukuzwa Zanzibar kwa madai kuwa tulitoa matokeo ya uongo," alisema Oriwo.
Kuhusu tafiti za kisiasa, Oriwo alisema ni kawaida kwa kampuni yake kukusanya maoni kuhusu hali ya nchi kisiasa kila baada ya miezi mitatu na kwamba tafiti zote za kujua hali ya kisiasa nchini hazitokani na wateja wao bali wanajidhamini wenyewe, hivyo hazina aina yoyote ya upendeleo.
"Tunakusudia kufanya utafiti mwingine wa kukusanya maoni ya wananchi kuhusu hali ya siasa nchini kabla ya uchaguzi mkuu na matokeo yatatoka kabla uchaguzi huo wa Oktoba mwaka huu.
"Tukimaliza kazi ya kukusanya maoni hayo, tutatoa matokeo kwa wananchi bila ya kubania hata kama yataonyesha kuwa umaarufu mgombea wa CCM umeanguka kwa sababu hatushabikii siasa," alisema Oriwo.
SOURCE MWANANCHI:
Dk Chegeni alitoa malalamiko hayo jana kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya chama hicho,yaliopo Lumumba jijini Dar es Salaam.
Mjumbe huyo, alitoa lawama hizo baada ya gazeti hili toleo la Jumatatu wiki hii kumnukuu Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe kwamba Kampuni Binafsi ya Synovate imeficha taarifa ya utafiti inayoonyesha mgombea urais wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa anaongoza kwa kura za maoni.
"Sisi (CCM) tunasikitika sana kwa gazeti la Mwananchi kuandika habari hiyo tena ukurasa wa mbele na kupotosha Watanzania. Tunaamini Mwananchi wanalo lao jambo. Limeonyesha dalili za wazi za kupinga CCM na kuunga mkono chama cha Chadema," alisema.
Alipoulizwa iweje kulishutumu gazeti la Mwananchi wakati lilizingatia kanuni za uandishi wa habari wakati wa kuandika habari hiyo, kwa kutoa fursa kwa pande zote kutoa maelezo, ikiwemo Synovate, Dk Chegeni alizidi kusisitiza kwamba CCM haikutendewa haki kwenye taarifa hiyo.
Alisema kwamba pamoja na gazeti hilo, kuzingatia kanuni za uandishi wa habari, jinsi habari hiyo ilivyotoka ilionyesha kuikandamiza CCM na kuifagilia Chadema.
Dk Chegeni ambaye alikuwa mbunge wa Busega, lakini alishindwa kwenye kura za maoni na Dk Titus Kamani, alidai kwamba Synovate imeliamuru Mwananchi kukanusha na kuomba radhi kwenye ukurasa wa mbele na kwamba wao wanasisitiza hilo kama sehemu ya kuisafisha CCM mbele ya wananchi.
Mhariri Mtendaji wa Mwananchi Communications Ltd (MCL), Theophil Makunga alisema hajapokea barua yoyote kutoka Synovate kutaka taarifa iliyoandikwa na Mwananchi ikanushwe na kuomba radhi.
Kuhusu habari inayolalamikiwa na CCM, Makunga alisema gazeti la Mwananchi lilitimiza wajibu wa kuuhabarisha umma.
Alifafanua kwamba mwandishi wa mwananchi akaripoti taarifa hizo zilizotolewa na Mbowe kwenye kampeni kama ilivyo kwa vyama vingine ambavyo vinatoa taarifa zao kwenye kampeni.
Makunga alisema habari hiyo iliandikwa kwa kuzingatia kanuni za uandishi wa habari ikiwa ni pamoja na Synovate kupewa fursa ya kujibu shutuma walizoelekezewa.
Kuhusu tuhuma kwamba Mwananchi limekuwa liiandika vibaya CCM na kuipendelea Chadema, Makunga alisema hiyo siyo kweli kwa sababu ripoti ya Synovate inaonyesha ni gazeti hili linaandika bila upendeleo kwa asilimia 97.
"Yeye (Dk Chegeni) anatoa mawazo yake kama mkereketwa wa CCM, lakini ukweli ni kwamba utafiti wa kisayansi uliotolewa na Synovate unaonyesha sisi tuko neutral (bila upendeleo) kwa asilimia 97," alisema Makunga.
Kwenye mkutano na waandishi wa habari jana, CCM ilionyesha kukerwa na taarifa hiyo ya Mbowe na kuingilia kati kauli hiyo licha ya kwamba Synovate walikanusha na vyombo vya habari vikaiandika kwa kina jana.
"Tunamtaka Mbowe aache kuwapotosha watanzania," alisema DK Chegeni ambaye baada ya kushindwa katika kura za maoni za kuwania kuwa mgombea wa CCM, Busega, aliripotiwa kutishia kuhamia Chadema kwa kile kilichoelezwa kutokubaliana na matokeo hayo.
Alipouilizwa kama haoni kitendo cha kuendelea kuvitaka vyombo vya habari vikanushe taarifa hiyo ya Mbowe kwa mara nyingine ni kuonyesha mchecheto wa upinzani wanaoupata kutoka Chadema, Dk Chegeni alisema taarifa hiyo, iliandaliwa kwa makusudi ili kushawishi wananchi kwamba Dk Slaa anaongoza wakati si kweli.
Alisema kinachowauma zaidi ni kwamba Mbowe alitumia taasisi inayoheshimika nchini ya Synovate, kumuibulia umaarufu Dk Slaa jambo ambalo ni si kweli.
Maelezo hayo ya Dk Chegeni yamekuja siku moja baada ya Meneja wa Synovate (T), Aggrey Oriwo kukanusha kauli iliyotolewa Jumapili na Mbowe katika mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi mkuu kwamba Synovate imeogopa kutangaza matokeo kuhusu umaarufu wa wagombea yaliyoonyesha Dk Slaa anaongoza.
"Taarifa hizo ambazo pia zimeripotiwa katika baadhi ya magazeti si za kweli. Mimi kama msimamizi mkuu wa Synovate Tanzania nimekerwa sana na nimeandika malalamiko yangu kwa Baraza la Habari Tanzania (MCT), kulalamikia vyombo vilivyoripoti," alisema Oriwo.
Alisema Synovate ni kampuni huru inayofanya kazi zake kwa ukweli na uwazi bila ya kushawishiwa au kulazimishwa na mtu au taasisi yoyote ya kisiasa.
"Kauli ya Mbowe imetukera sana na …tunamtaka kama ana uhakika na ushahidi wa aliyosema, autoe hadharani kama sisi tulivyotoa matokeo hadharani," alisema Oriwo.
Alisema hawana cha kuficha na kwamba hawajatishwa wala kulazimishwa na chama au taasisi yoyote kuzuia matokeo ya utafiti.
"Ubora wa kazi zetu unakubalika kitaifa na kimataifa kwa sababu hatushabikii chama chochote cha siasa na ndio maana mwaka jana tulifukuzwa Zanzibar kwa madai kuwa tulitoa matokeo ya uongo," alisema Oriwo.
Kuhusu tafiti za kisiasa, Oriwo alisema ni kawaida kwa kampuni yake kukusanya maoni kuhusu hali ya nchi kisiasa kila baada ya miezi mitatu na kwamba tafiti zote za kujua hali ya kisiasa nchini hazitokani na wateja wao bali wanajidhamini wenyewe, hivyo hazina aina yoyote ya upendeleo.
"Tunakusudia kufanya utafiti mwingine wa kukusanya maoni ya wananchi kuhusu hali ya siasa nchini kabla ya uchaguzi mkuu na matokeo yatatoka kabla uchaguzi huo wa Oktoba mwaka huu.
"Tukimaliza kazi ya kukusanya maoni hayo, tutatoa matokeo kwa wananchi bila ya kubania hata kama yataonyesha kuwa umaarufu mgombea wa CCM umeanguka kwa sababu hatushabikii siasa," alisema Oriwo.
SOURCE MWANANCHI: