Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Dk Chami: Wafanyabishara ‘feki' wageni ondokeni nchini
Friday, 10 December 2010 20:49
Fidelis Butahe
WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyrill Chami jana alitangaza vita dhidi ya wafanyabishara wa kigeni wanaofanya shughuli kinyume na leseni zaao, akiwataka waanze kurejea kwao kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria. Chami ametoa agizo hilo wakati mitaa ya miji kadhaa nchini ikizidi kufurika wageni ambao wamejikita kuanzia kwenye biashara kubwa hadi ndogondogo, idadi kubwa ya wanaofanya kazi hizo ikiwa ni Wachina.
Chami, kama ilivyo kwa mawaziri wengine, ametoa kauli hiyo baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwatahadharisha kuwa hatakuwa na simile na waziri atakayeboronga katika utekelezaji wa majukumu yake. Kikwete, ambaye alikuwa akieleza majukumu ya mawaziri wanaounda baraza lake jipya, pia aliwataka kuwajibika, kufuata kanuni, sheria na pia kupambana na rushwa huku akisisitiza kuwa vita dhidi ya rushwa ni suala la kikatiba na kuwataka kuhakikisha kuwa Mpango wa Pili wa Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa (NACSAP-11) unatekelezwa.
Jana, Dk Chami alisema jijini Dar es Salaam kuwa wapo wafanyabiashara wa kigeni nchini wanaofanya shughuli zao kinyume cha sheria na taratibu za leseni na kuwataka wajisalimishe kabla ya kubainika na kuchukuliwa hatua. Bila ya kutaja aina ya wafanyabiashara hao, Dk Chami, ambaye alikuwa akizungumza na wafanyakazi wa ofisi ya Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela), alisema:
"Wapo wanaoingia nchini kwa mgongo wa kufanya kazi katika makampuni, lakini baada ya muda wanajitosa katika baishara mbalimbali katikati ya jiji.
Wapo wanaotoka katika nchi rafiki, lakini hatutasita kuwachukulia hatua kwa kuwa hata huko wanakotoka kuna sheria za kufanya biashara. "Huu ni mchakato ambao umeshaanza kazi; tunawafuatilia; ni vyema kumjulisha mtu kabla hujamchukulia hatua. Kwa hiyo wajue kuwa tunalifuatilia jambo hili na kama wapo wanaojijua, basi wafungashe virago mapema." Alisema kuwa kauli hiyo si ya kisiasa, utani wala kufurahisha wananchi na kusisitiza kuwa yeyote aliyeingia nchini kwa njia za panya, ajiandae kufungasha virago.
Alisema kuwa wingi wa wafanyabisahara hao umekuwa kero ya muda mrefu kwa Watanzania kwa kuwa wanauza bidhaa zao kwa bei ya chini hali inayowafanya wafanyabiashara wazawa kufanya kazi yao katika mazingira magumu. "Unaweza kukuta wanauza bidhaa zao kwa Sh2,000 wakati mfanyabiashara Mtanzania anauza bidhaa kama hiyo kwa Sh5,000. Wizara yangu kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani, Kituo cha Uwekezaji (TIC) tutazitazama leseni za biashara kwa hawa wageni kama kweli biashara walizosajili ndizo hizo wanazozifanya," alisema Dk Chami.
Dk Chami alisema: "Haiwezekani mtu aje kama mfanyabiashara wa madini halafu kesho tumkute Kariakoo akifanya shughuli nyingine kabisa. "Jambo hili tutalitazama pia hata kwa Watanzania wanaofanya biashara kinyume na leseni walizoomba." Alifafanua kuwa operesheni hiyo ya kuwabaini wafanyabiashara hao ni ya muda mfupi na kusisitiza kuwa serikali haitasita kumtimua nchini atayebainika hata kama atakuwa na biashara iliyotoa ajira kwa Watanzania kiwango kikubwa. "Ndio maana tumelizungumza hili jambo mapema ili kuepuka malalamiko, watu wenye hekima zao watajua nini cha kufanya ikiwa ni pamoja na kufanya biashara kulingana na leseni zao zinavyosema," alisema Dk Chami.
Dk Chami hakutaja ni wafanyabiashara wa asili gani, lakini kwenye miji mingi nchini Wachina wamekuwa wakiuza bidhaa kwa bei ya chini na kufanya zile zinazouzwa na wazalendo kukosa soko. Wachina, ambao wanakaribia 10,000 nchini kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2008 za Shirika la Habari la China (Xhinua), pia wamekuwa wakiuza bidhaa ambazo hazidumu kwa muda mrefu, zikiwemo tochi, taa, viatu, mapazia, nguo, samani na vitu vingine.
Dk Chami pia aliipongeza Brela kwa utendaji wake wa kazi pamoja na kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo jipya na kuwataka wananchi kusajili biashara zao ili kuweza kupanua wigo wa biashara na kuvutia uwekezaji. Naye mkurugenzi mtendaji wa Brela, Esteriano Mahingira alisema zoezi la kuhakiki makampuni yanayofanya shughuli zake kinyume na leseni husika bado linaendelea.
"Zoezi hili tuliliweka bayana mwishoni mwa mwaka jana na linaendelea. Yapo makampuni ambayo baada ya kupata taarifa hizi yemejisalimisha," alisema Mahingira.
Friday, 10 December 2010 20:49
Fidelis Butahe
WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyrill Chami jana alitangaza vita dhidi ya wafanyabishara wa kigeni wanaofanya shughuli kinyume na leseni zaao, akiwataka waanze kurejea kwao kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria. Chami ametoa agizo hilo wakati mitaa ya miji kadhaa nchini ikizidi kufurika wageni ambao wamejikita kuanzia kwenye biashara kubwa hadi ndogondogo, idadi kubwa ya wanaofanya kazi hizo ikiwa ni Wachina.
Chami, kama ilivyo kwa mawaziri wengine, ametoa kauli hiyo baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwatahadharisha kuwa hatakuwa na simile na waziri atakayeboronga katika utekelezaji wa majukumu yake. Kikwete, ambaye alikuwa akieleza majukumu ya mawaziri wanaounda baraza lake jipya, pia aliwataka kuwajibika, kufuata kanuni, sheria na pia kupambana na rushwa huku akisisitiza kuwa vita dhidi ya rushwa ni suala la kikatiba na kuwataka kuhakikisha kuwa Mpango wa Pili wa Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa (NACSAP-11) unatekelezwa.
Jana, Dk Chami alisema jijini Dar es Salaam kuwa wapo wafanyabiashara wa kigeni nchini wanaofanya shughuli zao kinyume cha sheria na taratibu za leseni na kuwataka wajisalimishe kabla ya kubainika na kuchukuliwa hatua. Bila ya kutaja aina ya wafanyabiashara hao, Dk Chami, ambaye alikuwa akizungumza na wafanyakazi wa ofisi ya Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela), alisema:
"Wapo wanaoingia nchini kwa mgongo wa kufanya kazi katika makampuni, lakini baada ya muda wanajitosa katika baishara mbalimbali katikati ya jiji.
Wapo wanaotoka katika nchi rafiki, lakini hatutasita kuwachukulia hatua kwa kuwa hata huko wanakotoka kuna sheria za kufanya biashara. "Huu ni mchakato ambao umeshaanza kazi; tunawafuatilia; ni vyema kumjulisha mtu kabla hujamchukulia hatua. Kwa hiyo wajue kuwa tunalifuatilia jambo hili na kama wapo wanaojijua, basi wafungashe virago mapema." Alisema kuwa kauli hiyo si ya kisiasa, utani wala kufurahisha wananchi na kusisitiza kuwa yeyote aliyeingia nchini kwa njia za panya, ajiandae kufungasha virago.
Alisema kuwa wingi wa wafanyabisahara hao umekuwa kero ya muda mrefu kwa Watanzania kwa kuwa wanauza bidhaa zao kwa bei ya chini hali inayowafanya wafanyabiashara wazawa kufanya kazi yao katika mazingira magumu. "Unaweza kukuta wanauza bidhaa zao kwa Sh2,000 wakati mfanyabiashara Mtanzania anauza bidhaa kama hiyo kwa Sh5,000. Wizara yangu kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani, Kituo cha Uwekezaji (TIC) tutazitazama leseni za biashara kwa hawa wageni kama kweli biashara walizosajili ndizo hizo wanazozifanya," alisema Dk Chami.
Dk Chami alisema: "Haiwezekani mtu aje kama mfanyabiashara wa madini halafu kesho tumkute Kariakoo akifanya shughuli nyingine kabisa. "Jambo hili tutalitazama pia hata kwa Watanzania wanaofanya biashara kinyume na leseni walizoomba." Alifafanua kuwa operesheni hiyo ya kuwabaini wafanyabiashara hao ni ya muda mfupi na kusisitiza kuwa serikali haitasita kumtimua nchini atayebainika hata kama atakuwa na biashara iliyotoa ajira kwa Watanzania kiwango kikubwa. "Ndio maana tumelizungumza hili jambo mapema ili kuepuka malalamiko, watu wenye hekima zao watajua nini cha kufanya ikiwa ni pamoja na kufanya biashara kulingana na leseni zao zinavyosema," alisema Dk Chami.
Dk Chami hakutaja ni wafanyabiashara wa asili gani, lakini kwenye miji mingi nchini Wachina wamekuwa wakiuza bidhaa kwa bei ya chini na kufanya zile zinazouzwa na wazalendo kukosa soko. Wachina, ambao wanakaribia 10,000 nchini kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2008 za Shirika la Habari la China (Xhinua), pia wamekuwa wakiuza bidhaa ambazo hazidumu kwa muda mrefu, zikiwemo tochi, taa, viatu, mapazia, nguo, samani na vitu vingine.
Dk Chami pia aliipongeza Brela kwa utendaji wake wa kazi pamoja na kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo jipya na kuwataka wananchi kusajili biashara zao ili kuweza kupanua wigo wa biashara na kuvutia uwekezaji. Naye mkurugenzi mtendaji wa Brela, Esteriano Mahingira alisema zoezi la kuhakiki makampuni yanayofanya shughuli zake kinyume na leseni husika bado linaendelea.
"Zoezi hili tuliliweka bayana mwishoni mwa mwaka jana na linaendelea. Yapo makampuni ambayo baada ya kupata taarifa hizi yemejisalimisha," alisema Mahingira.