Dk Bilal naye ataka 'mafisadi' wang'atuke!

NakuliliaTanzania

JF-Expert Member
Sep 24, 2007
555
7
Naona kumekucha wandugu!



Dk Bilal: Waliotuhumiwa kwa ufisadi wajiuzulu


*Asema hakuna sababu ya wao kubakia madarakani

*Ashauri viongozi kuacha ubinafsi kwenye mikataba

*Atahadharisha hali hii ikiendelea vurugu zitatokea

*Asema CCM upande wa Zanzibar imedorora


Na Salma Said, Zanzibar


WAZIRI Kiongozi Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk Mohammed Gharib Bilal, amesema kiongozi anayetuhumiwa kwa ufisadi anapaswa kuchukua uamuzi wa kujiuzulu ili kutoa nafasi ya uchunguzi kufanyika juu tuhuma zinazomkabili.


Alisema uamuazi wa kujiuzulu ni muhimu hasa kama tuhuma hizo zinahatarisha amani katika nchi.
Dk Bilal alisema hivi karibuni wakati wa mahojiano maaluum na Mwananchi nyumbani kwake Migombani Mkoa wa Mjini Magharibi.


Alisema iwapo tuhuma zinazoelekezwa ni kubwa ambazo zinaweza kuhatarisha usalama na amani ya nchi basi hakuna sababu ya kiongozi kubakia katika madaraka.


�Kwenye tuhuma kubwa ambazo zinahatarisha hata amani ya nchi, ni bora kiongozi akachukua uamuzi wa kisiasa wa kujiuzulu ili atoe nafasi ya kuchunguzwa tuhuma hizo,� alisema Bilal.


Alisema endapo kiongozi amepatikana na hatia katika suala la rushwa basi sheria ifuate mkondo wake na sio kuwekewa kinga kwa sababu aliyepatikana na tuhuma hizo ni mtu mkubwa.


�Kiongozi achunguzwe na akibainika kama amefanya vitendo vya kupokea au kutoa rushwa, nadhani sheria ndio iachiwe ichukue mkondo wake na isiingiliwe,� alishauri.


Alisema iwapo sheria zitafuatwa bila ya upendeleo zitawasafisha wanaotuhumiwa na kurejesha imani ya wananchi kwa viongozi hao.


Hivi karibuni, Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa alitaja majina 11 ya viongozi wa serikali ambayo alidai kuwa wanatuhumiwa kwa ufisadi.


Dk Bilal aliwatahadharisha viogozi wa serikali kuwa makini na mikataba wanayosiani kwani inaweza kusababisha mifarakano katika nchi kama inavyojitokea hivi sasa, ambapo baadhi ya mikataba inadaiwa kuwa na matatizo.


Alisema lazima tahadhari ichukuliwe kuweza kuepukana na matatizo kama hayo yanayojitokeza na kudai kuwepo kwa udhaifu katika baadhi ya mikataba.


�Inaonekana udhaifu upo, hata kushutumiwa kwa baadhi ya viongozi wa CCM kuwa wametoa rushwa wakati wa uchaguzi huko ni kukiri kuwa kuna tatizo maana lisemwalo lipo na kama halipo laja, basi lishughulikiwe�,� alisema huku akitumia methali za kiswahili.


Waziri Kiongozi huyo Mstaafu alishauri kurekebishwa kwa mfumo utaoaji maamuzi ili kuongeza idadi ya watu wanaotoa maamuzi ili kupanua demokrasia ya kweli badala ya kuachiwa wachache kuwaamulia walio wengi.


Alisema hali hiyo inaweza kusaidia kuondoa malalamiko kwa wananchi kutokana na maamuzi yanayoamuliwa na watu wengi tofauti ya maamuzi yanayotolewa na wachache ambayo mara nyingi husababisha migogoro na kutoelewana.


Dk Bilal alisema Tanzania ina wataalamu wengi wa fani mbalimbali tangu zamani, lakini jambo la kusikitisha ni kuwa wataalamu hao hawatumiki ipasavyo.


Kuhusu nguvu za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Bilal alisema bado kina nguvu kutokana na kufanya vizuri katika chaguzi zote zinazofanyika nchini na kudai kuwa CCM Zanzibar imedorora.


Alisema kwamba tatizo kubwa linaloikabili Zanzibar ni tofauti ya uongozi na kwamba hivi sasa Zanzibar hakuna mwamko katika chama na kusababisha kidorore.


�CCM Zanzibar imedorora na inatokana na kuuliwa kwa maskani, hivi sasa hakuna maskani kama zilivyokuwapo. CCM kilikuwa kinapata msukumo kutoka uongozi wa juu, lakini sasa aina ya uongozi imechangia kwa kiasi kikubwa kudorora kwa chama,� alisisitiza Dk Bilal.

Dk Bilal alisema ingawa baadhi ya wana CCM Zanzibar hawapendi kuisikia kauli hiyo, alisisitiza kuwa huo ndiyo ukweli. "Hakuna mwamko wowote wa kuhamasisha vijana katika chama...," alisisitiza.


Aliahidi baada ya kumalizika Uchaguzi wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) wataanza kuhamasisha wanachama.


�Ukija uchaguzi kunakuwa na mwamko kidogo, lakini kukiwa hakuna chaguzi, chama kinalala watu wanasahau kama chama kipo, tukimaliza chaguzi tutaanza kuhamasisha wanachama,� alisema.


Dk Bilal aliwahi kutoa kauli kama hiyo ya kudorora kwa CCM Zanzibar wakati alipokuwa akijaza fomu ya kuwania nafasi ya Rais wa Zanzibar na kwamba kauli hiyo ilizusha gumzo kubwa visiwani hapa na kusababisha makundi mawili ndani ya chama hicho, moja likiwa nyuma yake na lingine kwa Amani Abeid Karume ambaye kwa sasa ni Rais wa Zanzibar.


Kuhusu maoni yake juu ya uongozi wa Dk Salmin Amour, alisema mara zote alikuwa tayari kukubali kushauriwa licha ya kuwa maamuzi ya mwisho kuwa yake mwenyewe.


Akizungumzia hali ya maisha, alisema sasa yamekuwa magumu zaidi na kumekuwapo na kasoro nyingi katika serikali ambazo zinahitaji kupatiwa ufumbuzi licha ya kuwepo mafanikio kadhaa.


�Hapo nje kuna mfereji (bomba la maji) mwaka wa nne huu hautoi maji, hata hivyo maji hapa kwetu tunapata kwa njia nyingi. Mafanikio yapo katika baadhi ya mambo, lakini matatizo yapo mengi na yanahitaji kurekebishwa. Kwa mfano huduma za afya bado ni mbaya ...,� alisisitiza Dk Bilal.

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=2460
 
mmhh kazi hiyo, mkuu ndio anajiandaa kwa kugombea urahisi mwakani aua vipi? hata hivyo mie nnamkubali sana tu mkuu huyu na nitafurahi ukiongoza nchi yetu ktk kipindi kijacho
 
haya ndio matokeo ya siasa za majungu,kama hao sisiemu walimkataa kipindi kile unategemea yeye awatete.moto ulishaanza kuchochewa,mie naamini sisiemu hapatoshi manaake utasikia mwanri akimhoji Dk bilali kwanini akuwasilisha mawazo yake katika vikao vya chama..

tusubiri mengi yatakuja,hata magufuli alimuuliza Mkandara siku ya maadhimisho ya miaka minane ya mwalimu..Kwanini walimzuia zitto kuhutubia pale chuo?
 
Tatizo la viongozi wengi ni wanafiki. Naona taratibu unafiki unaanza kuondoka ktk CCM

Chama changu kinaanza kugeuka na kuelekea inapopaswa ielekee.

Swali: Je wenye fedha waioiteka chama watakubali mageuzi ya kweli?
 
Tatizo la viongozi wengi ni wanafiki. Naona taratibu unafiki unaanza kuondoka ktk CCM

Chama changu kinaanza kugeuka na kuelekea inapopaswa ielekee.

Swali: Je wenye fedha waioiteka chama watakubali mageuzi ya kweli?

FD,

Inabidi kukirudisha chama kwa wenye nacho, ili angalau 2010 ije ile CCM ya Nyerere na sio hii ya Mtandao inaokumbatia matajiri.

Vijana jiandaeni kwa mapambano mwaka 2010. Mapambano ya hoja na fikra na wala sio bunduki au matusi.
 
Tatizo la viongozi wengi ni wanafiki. Naona taratibu unafiki unaanza kuondoka ktk CCM

Chama changu kinaanza kugeuka na kuelekea inapopaswa ielekee.

Swali: Je wenye fedha waioiteka chama watakubali mageuzi ya kweli?

Ni kweli kabisa politicians wengi ni wanafiki na pia ni ma-opportunists. Ni kweli unafiki unapungua sababu ya makundi ambayo yako ndani CCM. CCM ya Visiwani iligawanyika tangu 2000 wakati Komandoo akiwa anataka katiba ibadilishwe na/au Bilal aongoze nchi, badala yake Karume alipitia geti la uani na kutwaa uongozi.

Wenye fedha wanaweza kukubali mageuzi if and only if pressure itakuwa kubwa sana na hasa kama kundi la wana CCM walio nje ya mtandao wataungana pamoja na kuanza kusema ukweli na pia kama wabunge wa CCM watakubali kuishikisha adabu serikali ya CCM kwa kuondoa nidhamu ya woga na kuacha unafiki. Nina uhakika si wabunge wote ni wana mtandao, hivyo sasa hivi ni rite time ya kuleta mageuzi ya kweli, lakini inahitaji ujasiri na determination. Maana unapopambana na wenye fedha unatakiwa uwe tayari kwa lolote. Tatizo la wanasiasa wetu ambao bado wako active wanaangalia sana 2010 na 2015 badala ya kuangalia maslahi ya Taifa.
 
Inabidi kukirudisha chama kwa wenye nacho, ili angalau 2010 ije ile CCM ya Nyerere na sio hii ya Mtandao inaokumbatia matajiri.

Vijana jiandaeni kwa mapambano mwaka 2010. Mapambano ya hoja na fikra na wala sio bunduki au matusi.

Tatizo ni kwamba wanaopiga kelele za kukemea maovu ya wanamtandao wote ni wazee, sijaona hata kijana mmoja ambaye kajitokeza kukemea wana mtandao jinsi walivyokumbatia matajiri. Je, ndani ya CCM kuna vijana walio na guts za kuwakemea akina RA, EL na JK ambao ndiyo wameshikilia CC na NEC?
 
Tatizo ni kwamba wanaopiga kelele za kukemea maovu ya wanamtandao wote ni wazee, sijaona hata kijana mmoja ambaye kajitokeza kukemea wana mtandao jinsi walivyokumbatia matajiri. Je, ndani ya CCM kuna vijana walio na guts za kuwakemea akina RA, EL na JK ambao ndiyo wameshikilia CC na NEC?

Vijana hawana media ya kutolea hoja zao na kusikilizwa. Mwaka 2010 nafasi zote zitakuwa wazi, mwamuzi ni wananchi wenyewe.
 
..naye ni fisadi tuu na tunakumbuka alivyokuwa pale Sayansi jinsi rushwa na wizi ulivyokuwa umekithiri under his watch na tunajua jinsi alivyotumia pesa zetu kuwapendelea ndugu na ukoo wake kuwaleta US bila kujali wengine wenye qualifications za kweli...upuuzi mtupu lakini kama amebadilika tunashukuru!
 
..naye ni fisadi tuu na tunakumbuka alivyokuwa pale Sayansi jinsi rushwa na wizi ulivyokuwa umekithiri under his watch na tunajua jinsi alivyotumia pesa zetu kuwapendelea ndugu na ukoo wake kuwaleta US bila kujali wengine wenye qualifications za kweli...upuuzi mtupu lakini kama amebadilika tunashukuru!

Unafikiri fisadi anabadilika? Wanasema hayo wayasemao kwasababu tu sasa hawana ulaji.

Kuna watu kama Salim, Warioba na hata Butiku, wakisema nitaamini maana hata walivyokuwa na nafasi, hawakufanya madudu mengi. Lakini Dr. Bilal napata kigugumizi. Alivyokuwa sayansi, alivyokuwa anamzunguka Mkapa na akina mahalu kwasababu tu Ikulu
kulikuwa na rais Mzazibari mwenzake nk.

Tanzania tunahitaji mabadiliko ya nguvu, sio hii viraka kila sehemu. Mabadiliko ya watu bila mabadiliko ya sheria na katiba hayatatusaidia. Hata kama kila mtu atachapa kazi ipasavyo lakini kama matumizi ndio hayo ya magari ya 100M kila waziri, kila katibu mkuu, kila msemaji wa upinzani, hapo kazi tunayo.
 
Mimi nadhani tujadili yale aliyoyazungumza badala ya kum attack yeye kama Bilal.
Kama wengi wetu tulivyowahi kujadili huko nyuma, kwamba tukielekeza michango yetu kwa kujadili mtoa hoja, haitusaidii, na zaidi tutajikuta hakuna msafi hata mmoja katika Taifa letu miongoni mwa wale tunaowaona kama key figures.
Kujitokeza kwa Bilal ni jambo zuri kwa sababu naye pia anao wanomuunga mkono nyuma yake, tena si kidogo ni wengi. kwa maana nyingine hii ni pressure nyingine kwa serikali ya JK kuweza kufanya mabadiliko.
Itafika mahali atajikuta amebaki yeye na wanamtandao wake ndani ya ccm. sidhani kama hii itamsaidia kuvuka 2010
 
Tatizo la viongozi wengi ni wanafiki. Naona taratibu unafiki unaanza kuondoka ktk CCM

Chama changu kinaanza kugeuka na kuelekea inapopaswa ielekee.

Swali: Je wenye fedha waioiteka chama watakubali mageuzi ya kweli?

[COLOR=[B]Mkuu ni mwelekeo mzuri huu maana CCM itamalizwa na wanaCCM wenye. Kila siku tutashuhudia wengi wakija na kusema hayo hayo. Iwe kwa unafiki au kwa njia ya nitoke vipi na mimi. Wameanza wazee na naamini watakuja hadi vijana watasema yao. CCM kazi mnayo nani wa kuwaziba hawa wazee mdomo? Hamna. Tuendeleze mapambano ya kifikira na wananchi waendeleze mapambano kwa kutumia haki yao na silaha yao ya kura. Mungu isaidie Tanzania.[/B]
 
Mtanzania, Keil, Field Marshall ES,

Unajua unaweza kutaka kutoa dukuduku lakini ukahofia matokeo yake. Kwakuwa wengi wanaongea kwa sasa inaonyesha kuwa kuna tatizo ndani ya chama.

Hii ni nafasi pekee kwa kila mwenye nyongo ATEME. Tukianza kutema cheche kila kona hata hao wenye fedha itabidi washtuke.
Maana wamelala usingizi mzito mno!

Tutafika tu.
 
Ina wezekana Watanzania wote ni wafisadi!!Mbona hatushituki...
Yesu alisema Yeyote anaye dhani hana Dhambi na awe wakwanza Kurusha jiwe- kumpiga mwanamke Mzinzi hakuna alie weza kufanya hivyo!!- Mafisadi hawawezi kuwatoa mafisadi wenzao...

Kazi ipo...
 
kumuongelea mtu ni jambo zuri,kwa sababu historia huwa inajirudia kila mara nyingi,wengi wanaotoa malalamiko kwa sasa ni waathirika kwa namna moja au nyingine hiyo kujua past ni jambo muhimu.

Kwa kufanya hivyo wanasaidia kutupa sisi yale tusiyoyajua kutoka upande wapili.
 
Sasa mnaposema waliotuhumiwa wajiuzuru, mnataka JK ajiuzuru kupisha uchunguzi kwani naye ni mmoja kati ya waliotuhumiwa. Nafikiri km JK asingekuwamo kwenye list angechukua hatua kuwapiga chini basing on Slaa findings, na yeye yumo. Atamwachia Shein, thubutu hawezi, ataendelea KUWABEBA.
 
kumuongelea mtu ni jambo zuri,kwa sababu historia huwa inajirudia kila mara nyingi,wengi wanaotoa malalamiko kwa sasa ni waathirika kwa namna moja au nyingine hiyo kujua past ni jambo muhimu.

Kwa kufanya hivyo wanasaidia kutupa sisi yale tusiyoyajua kutoka upande wapili.

Lakini pia nadhani basi ingeanziswa thread yake ya kumjadili DK Bilal...hapa hoja siyo yeye binafsi, hoja ni alichosema, mintarafu hali ya kisiasa nchini kwa kipindi hiki!

Kwa maoni yangu naona kuna upinzani wa hali ya juu dhidi ya wanamtandao, na kama Nyerere alikuwa sahihi, upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM yenyewe na dalili ndo kama hizo!
 
vyote hivi ni viinimacho.. yaani treni la wapinzani leo wana CCM wanalidandia...! Hivi muda wote huo hakuna kiongozi wa CCM aliyejua uzito wa tatizo? Leo hii wamezukiwa na "mwanga mtakatifu" na sasa wameanza "kuona". Mazingaombwe ni mazingaombwe tu!!
 
chama Cha Mapinduzi Si Mama Yangu....ni Njia Nzuri Aliyoitumia Dk Bilal Katika Kumuenzi Mwalimu
 
vyote hivi ni viinimacho.. yaani treni la wapinzani leo wana CCM wanalidandia...! Hivi muda wote huo hakuna kiongozi wa CCM aliyejua uzito wa tatizo? Leo hii wamezukiwa na "mwanga mtakatifu" na sasa wameanza "kuona". Mazingaombwe ni mazingaombwe tu!!

Hata Sauli Mkuu, alikuwa akiwatesa wakristo wa mwanzo kabla hajaongoka, sasa huwezi kujua labda ndo mwanzo wa ushindi wa fikra....ya Mungu mengi!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom