Dk Bana: Kuna tatizo ndani ya CHADEMA. Kama hawawezi kujifanyia tathimini, mimi niko tayari

View attachment 882409

Wachambuzi wa masuala ya siasa nchini kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, pamoja na RUCU, wamevitaka Vyama vya Upinzani nchini kujifanyia tathimini kufuatia hamahama ya Makada wao wa udiwani zaidi ya 100, pamoja na wa ubunge wapatao sita.
Dk. Benson Bana (UDSM) alisema huenda kuna tatizo linaloendelea ndani ya Upinzani na linatakiwa kutafutiwa ufumbuzi haraka. "CHADEMA iache kukimbia tatizo wanapaswa kujiuliza kwa nini yanatokea wakati huu?"
Dk. Bana alieleza kuwa, "Wajifungie wafanye tathimini, kama hawawezi kujifanyia wawatafute hata watu wa nje .... binafsi nipo tayari kufanya hivyo tena bure kabisa."

Naye Dk. Richard Mbunda (UDSM) alieleza kuwa, hakuna sababu ya Wapinzani kuendelea kulalamika bila kurudisha imani yake kwa wananchi. "Kuendelea kulalamika siyo suluhu, wanatakiwa kupambana, siasa ni mapambano."

Prof. Gaudence Mpangala (RUCU), alivishauri Vyama vya Upinzani kujiunga na kupambana na hali inayoendelea. "Hata CHADEMA wakija na Sera mpya hawatafanikiwa katika mazingira haya. Lazima watatue kiini cha tatizo."
Profesa Mpangala aliongezea kuwa, "Ni lazima watambue kuwa, mkakati uliopo ni kuua Upinzani nchini, Sasa wakitambua hilo ninaamini watachukua hatua stahiki."


‘Upinzani wajitathmini hamahama ya wabunge’
Dk. Banna aliwashauri kuwafanyia tathimini mkakataa. Haya sasa Lowassa kaondoka na wengine watafuatia. It's the matter of time.
 
Asiyemjua Mzee Bana anaweza kupata shida ktk mawazo yake. Jitahidi tuu kuto kupenda siasa za upande mmoja ndio ataonekana mchambuzi mahiri uwezi kumfananisha na Mzee Ulinwengu ambaye ni mkweli
Wahaya wanaheshimika kwa kuwa na busara na hekima. Ila huyu ameondoa taswira hiyo yeye kwake in cheo tu, heki.a na busara baadaye.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawo wasomi ni sasa na professor Ossoro tu naripoti ya makinikia. Watuachie Chadema NI chama cha wananchi tena tusioenda Shule na walioenda
 
Huyu Dr. Bana anaongea ugoro tu. Ni kama kwamba hajui hama hama ya wabunge na madiwani ilikuwa inachochewa na nini. Hebu yeye ajiulize kwa nini hio hama hama sasa haipo? Jibu ni rahisi tu. Ni kwa kuwa endapo mbunge au diwani akihama sasa hivi atakuwa amepoteza nafasi yake hio ya kuchaguliwa kwa kuwa muda wa kufanya chaguzi ndogo umekwishapita. Ajiulize pia kwa nini kila mbunge au diwani aliyejiuzulu alipitishwa kugombea nafasi hio hio? Au kwa upande mwingine kwa nini hao waliojiuzulu hawakubaki kuwa wanachama wa kawaida tu? Na kwa nini sababu zilikuwa zinatolewa zile zile. Pia kwa nini haya yalikuwa yanatokea kipindi hiki tu? Majibu ya maswali haya hayahitaji tathmini kwa kuwa majibu yake yako wazi kabisa. Labda ni Dr. Bana pekee ndio hajui sababu ya hama hama.
Tathmini ya Dr Bana? Si afadhali kwenda kupiga ramli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uwa navishangaa vyombo vya habari kumualika huyo bwana kuongelea mambo ya siasa. Ukimsikiliza kwa makini utagundua kwamba kichwani Ana gap
 
Wote nyie ni wajinga na wanafiki! Kinachofanywa na hawa wahuni ni rushwa na uhujumu uchumi kupitia hizi chaguzi zinazotafuna mabilioni.

Mnatumia njia haramu na wakati mwingine vitisho kulazimisha watu wahamie kwenye chama chenu na wako walioleza hujuma mnazofanya na hamjawahi kukana wala kukawakamata au kuwashitaki kwa kuwazushia.

In short you are hooligans!

Pool of hooligans
 
Back
Top Bottom