calculator
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 279
- 137
Wana wa Kimandolu na JF kwa ujumla, Salaam.
Ama baada ya salaam naomba nijikite moja kwa moja kwa hoja yangu.
Diwani wa Kata ya Kimandolu (CHADEMA) Bw. Ngowi amekuwa kero na hakika tunajutia maamuzi yetu kumchagua mwaka juzi. Ana mihemko na anadaiwa madeni kila kona ya Kata. Amefikia mahali anamkashifu hadharani Mwenyekiti wetu wa chama wa Kata.
Amejijengea maadui wengi na wananchi wanamuona kama ni mjasiriamali wa siasa aliyekuja kwa siasa kwa maslahi yake binafsi.
Sisi wana wa Kimandolu tunakupa ujumbe huu kuwa safari yako ya kisiasa inaishia October hii. Rudi tu ukachunge kondoo wa bwana pale mlimani kwako.
Nawasilisha
Ama baada ya salaam naomba nijikite moja kwa moja kwa hoja yangu.
Diwani wa Kata ya Kimandolu (CHADEMA) Bw. Ngowi amekuwa kero na hakika tunajutia maamuzi yetu kumchagua mwaka juzi. Ana mihemko na anadaiwa madeni kila kona ya Kata. Amefikia mahali anamkashifu hadharani Mwenyekiti wetu wa chama wa Kata.
Amejijengea maadui wengi na wananchi wanamuona kama ni mjasiriamali wa siasa aliyekuja kwa siasa kwa maslahi yake binafsi.
Sisi wana wa Kimandolu tunakupa ujumbe huu kuwa safari yako ya kisiasa inaishia October hii. Rudi tu ukachunge kondoo wa bwana pale mlimani kwako.
Nawasilisha