Mzee wa Rula
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 8,171
- 3,346
Diwani wa CDM Ndg Nanyaro Ephata alitekwa yeye na mwenzake mmoja aitwaye Boniface na kupelekwa kusikojulikana. Wakiwa njiani kurudi hotelini ghafla walivamiwa na watu ambao walikuwa katika Toyota Landcruiser S/W T 203 BKW na kutekwa.
Huo ulikuwa ni usiku wa saa saba ambapo walikuwa wamemaliza kikao chao na kwenda kupaki magari mbali kidogo na hoteli waliyofikia ambayo haina parking. Wakiwa ndani ya gari, waliambiwa kuwa wasali sala zao za mwisho kwani kiherehere chao ndicho kilichowaponza! Baada ya kusikia hivyo Nanyaro ambae ni diwani wa Chadema Arusha kata ya Revolosi alijipanga ama afe yeye au wao nao wafe, hivyo alimrukia dereva na kuanza kung'an'gania steringi ili gari lipoteze mwelekeo. Kuona balaa limeanza jamaa mmoja alikimbia katika hao watekaji na kubaki watatu.
Dereva alipoona anashindwa kulimudu gari alimpa kipigo Nanyaro na kumsukuma nje ya gari yeye na mwenzake na kuondoka kwa kasi. Huo ulikuwa ni usiku na porini, kibaya zaidi katika purukushani ile jamaa walidondosha simu katika gari lile. Wakajitahidi kufika mjini na kupata msaada toka kwa viongozi wa CDM na kwenda kulipoti tukio hilo polisi ambapo walipofika walikuta tayari wameshafunguliwa kesi na wale jamaa kuwa walitaka kuwateka hao jamaa na wao walifanikiwa kuwadhibiti na kuwapora simu! Basi ikabidi nao watoe maelezo ambayo yalipelekea kurudishiwa simu zao!
Angalizo langu, tabia hii ya utekaji watu naona imeanza kushamiri, tabia hii ni mbaya na inapaswa kukomeshwa mara moja.
Huo ulikuwa ni usiku wa saa saba ambapo walikuwa wamemaliza kikao chao na kwenda kupaki magari mbali kidogo na hoteli waliyofikia ambayo haina parking. Wakiwa ndani ya gari, waliambiwa kuwa wasali sala zao za mwisho kwani kiherehere chao ndicho kilichowaponza! Baada ya kusikia hivyo Nanyaro ambae ni diwani wa Chadema Arusha kata ya Revolosi alijipanga ama afe yeye au wao nao wafe, hivyo alimrukia dereva na kuanza kung'an'gania steringi ili gari lipoteze mwelekeo. Kuona balaa limeanza jamaa mmoja alikimbia katika hao watekaji na kubaki watatu.
Dereva alipoona anashindwa kulimudu gari alimpa kipigo Nanyaro na kumsukuma nje ya gari yeye na mwenzake na kuondoka kwa kasi. Huo ulikuwa ni usiku na porini, kibaya zaidi katika purukushani ile jamaa walidondosha simu katika gari lile. Wakajitahidi kufika mjini na kupata msaada toka kwa viongozi wa CDM na kwenda kulipoti tukio hilo polisi ambapo walipofika walikuta tayari wameshafunguliwa kesi na wale jamaa kuwa walitaka kuwateka hao jamaa na wao walifanikiwa kuwadhibiti na kuwapora simu! Basi ikabidi nao watoe maelezo ambayo yalipelekea kurudishiwa simu zao!
Angalizo langu, tabia hii ya utekaji watu naona imeanza kushamiri, tabia hii ni mbaya na inapaswa kukomeshwa mara moja.